Historia ya Majini

Historia ya Majini

Kuna Sura katika Uisilamu ukisomewa jina anatoka tena ataungua vibaya maana jini anawagopa sana binadamu
nayale majini yanayomkomalia binadamu hata uyasomee vip hayatoki yakikuheshim yatajifanya yametoka ikipita miezi au mwaka yanapanda tena hayo yanakuwa yametokea wapi? Sikwama shekhe wa wachungaji hayatoki mpaka mtu yule afe.
 
maandamano
Umesema majin yako mabaya na mazuri.
Je haya mazuri ndio hawa yalioslim na kuwa waislam?.

Maana naona Watu wote wanaopandisha majini.
yale yanaowasumbua kwa maradh nk. Yote huwa yakitolewa yanasema majina ya Kiislam.
Kwahiyo Hata majini mabaya ni ya kiislam?.

Maana kama ya kiislam ni mazuri. Kwanini huvagaa watu na kuwatesa?.

Au majini yote ni ya kiislam?.

Hebu niwekee sawa hapo.
Kwa ninavyoelewa mimi hayo majina ni majina ya jamii za majini au ni majina yenye kukusudia aina fulani ya majini, ukisikia hayo majina si kwamba huyo jini hilo ndio jina lake bali hilo jina huwakilisha jamii ya huyo jini na kuna jamii nyingi tu za majini.

Chengine hayo majina ni binaadamu wenyewe tu ndio hutunga hayo majina na ndio maana utaona unaweza kukuta mkoa fulani wao majini aina fulani wanajina lao wanalowaita na kuna sehemu nyengine nao wanatumia jina lengine, na ukienda nchi zengine utakuta ni hivyo hivyo huwezi kukuta muarabu au mzungu anatumia jina cheketu au makata kumzungumzia jini.
 
Jini lako ni we mwenyewe aloo,ukienda kwa ustaadh ubwabwa akipata nyota yako anapakua anaauza kwa mwengine anasema ni majini yameleta barka.
Ni wanga tu
 
Je kuna mapepo?.
Majini na mapepo ndio hayo hayo, vyote ni imagination ya mwanadamu hasa pale anapokuwa amekosa maelezo ya jambo fulani. In reality, they don't exist. Imani kuhusu uwepo wa hivyo vitu imeletwa na kusambazwa zaidi na hizi dini mbili. Nje ya hizi dini mbili, hakuna hivyo vitu.
 
Yule alomwambia Yesu ajitupe mnarani alikuwa kuku?. Wale walotolewa na kuwaingia nguruwe walikuwa kenge?.

King Suleiman alikuwa anawamiliki na kumjengea kasri wale walikuwa sisimizi?.

Adam alikataliwa kushjudiwa na Kunguru?.
Hawa alishawishiwa na msukule?.
Uislamu ni laana, ukiwa mwislamu umelaaniwa.
 
nayale majini yanayomkomalia binadamu hata uyasomee vip hayatoki yakikuheshim yatajifanya yametoka ikipita miezi au mwaka yanapanda tena hayo yanakuwa yametokea wapi? Sikwama shekhe wa wachungaji hayatoki mpaka mtu yule afe.
Kuna mtu namjua yamemfanya kiziwi na haongei labda aongee mwenyewe mwaka wa 10 huu na ni binti yamemuachisha na shule halafu mtu anasema ni fikra zetu tu hivi wengine mnaishi mitaa ipi haya hayawapati na sisi tuje🙄
 
Nitumie jini moja kama unalo wewe mwenye akili.

Think out of the box.

Story za majini asili yake ni middle east. Sehemu nyingine za dunia hawakuwa na uzushi huo.

Watu wanaofikiriwa kuwa na majini huwa ni wagonjwa wa afya ya akili wakiwemo wenye Dissociative identity disorder (jaribu kusoma kuhusu hii) na hata wenye dissociative fugue. Matibabu yake yanaweza kufanyika kwa kuhusisha hypnosis na exorcism
Katika hao wenye kufikiriwa kuwa wana majini sio wote wanakuwa wanapitia hali ya kama kupatwa na ukichaa yani kupiga kelele,kufanya fujo au kuongea ongea yasiyoeleweka. Je hao nao ni vp? Maana unaweza ukaongea na huyo mtu kwa kawaida tu kama unavyoengea kawaida na mtu mwengine.
 
Jini mzuri anafanya kama wanavyofanya wale Wisilamu wa Swala tano,yaani Anaswali,hanywi pombe wala hamuingii mtu na kumtesa na mambo mengi na majini yapo ya aina nyingi kutoka na sehemu husika hubadilika kutokana na majina wengine huita kinyamkela au hujawahi kuona Mmasai kapandisha mori?
Kwahiyo ili jini awe jini mzuri sharti awe muislamu na ni mchamungu na sio muislamu jina?
 
Ukimaanisha unapata! Kaa hapo uanze kuongea haya maneno mwenyewe hutojutia kamwe
Ninamaanisha vibaya mbo. Nimechoma misgumaa na ubani usiku wa manane nawaita hawaji. Choma saana udi mpaka nikaambulia mafua makali lakini kweupe.. Nisaidieni jamani ndugu yenu nipate jini zurii la kike,
Vigezo..
Liwe jeupe
Jembamba
Refu kidogo
Lenye nywele ndefu
Liwe na asili ya kiratini
Lisiwe na nyash kubwa sana.

Yeyote atakaeliona hili jini anicheki. Donge nobo la pesa litatilewa.
 
Ninamaanisha vibaya mbo. Nimechoma misgumaa na ubani usiku wa manane nawaita hawaji. Choma saana udi mpaka nikaambulia mafua makali lakini kweupe.. Nisaidieni jamani ndugu yenu nipate jini zurii la kike,
Vigezo..
Liwe jeupe
Jembamba
Refu kidogo
Lenye nywele ndefu
Liwe na asili ya kiratini
Lisiwe na nyash kubwa sana.

Yeyote atakaeliona hili jini anicheki. Donge nobo la pesa litatilewa.
Nenda baharini mida hiyo! Hukosi chochote kitu! Kuna mdada hivi tiktok mbona alipata linalofanana naye!
 
Nenda baharini mida hiyo! Hukosi chochote kitu! Kuna mdada hivi tiktok mbona alipata linalofanana naye!
Nisije nikaenda huko nikakutana na vibaka wakanipora INIFINIKISI yangu.

Au nikakutana na majini ya kiume mambo yakawa si mambo.
 
maandamano
Kuna majini ya kiafrika. Ya kizungu na ya kijapan?.

Maana kama binadam kuna weusi , weupe nk..wao wakoje?.

Wana makabila,
Je kuna majini yana amini dini nyingne ukiacha Uislam?.

Maana yana free will.
Je kuna majini hayaamini kama kuna allah (Atheist) kama Kiranga .

Usichoke maswal..tupe ilmu dyunia ya hawa viumbe vya mnyenz Mungu subihala wa taala.
Kama kuna mizimu(majini) na mambo yao ni tofauti na dini basi kutakuwepo majini wengine ambao wana dini mbalimbali, maana kama binaadamu wanafuata dini tofauti tofauti sioni kwanini majini nao wasiwe hivyo pia.
 
Kwahiyo ili jini awe jini mzuri sharti awe muislamu na ni mchamungu na sio muislamu jina?
Ndiyo ukweli wenyewe yaani nao walidanganywa na mashetani kama tulivyodanganywa kabla ya kuja Mtume Muhammad (S.A.w)kama Mwenyezi Mungu ana mtoto au Mungu alikuwa na msaidizi lakini nao wakaongoka kupitia Quruani wakasamehe wanashika ibada kama Waisilamu tunaswali nao misikitini na kufunga na kuhiji Makka
 
Majini na mapepo ndio hayo hayo, vyote ni imagination ya mwanadamu hasa pale anapokuwa amekosa maelezo ya jambo fulani. In reality, they don't exist. Imani kuhusu uwepo wa hivyo vitu imeletwa na kusambazwa zaidi na hizi dini mbili. Nje ya hizi dini mbili, hakuna hivyo vitu.
Nje hizi dini kuna imani ya kwamba kila mtu huwa na spirit guide wake, kuna imani ya kuamini uwepo wa malaika na roho za watu waliyokufa n.k na yote hayo nje ya hizi dini kwa maana kuna watu hawaamini dini ila wanaamini hivyo vitu.
 
Ninamaanisha vibaya mbo. Nimechoma misgumaa na ubani usiku wa manane nawaita hawaji. Choma saana udi mpaka nikaambulia mafua makali lakini kweupe.. Nisaidieni jamani ndugu yenu nipate jini zurii la kike,
Vigezo..
Liwe jeupe
Jembamba
Refu kidogo
Lenye nywele ndefu
Liwe na asili ya kiratini
Lisiwe na nyash kubwa sana.

Yeyote atakaeliona hili jini anicheki. Donge nobo la pesa litatilewa.
Ushawahi kusikia kuhusu Lucid dreaming? Kwanini usijaribu hiyo njia maana utaweza ku experience chochote kile unachotaka kwenye ndoto yani vile unavyotaka ndio inavyotokea bila mipaka hata ukimtaka mwanamke yeyote yule.
 
Watu hujiuliza wana uhusiano na Waisilamu,Waisilamu Wanafuga Majini?

Majini ni viumbe wa Mwenyezi Mungu wameumbwa miaka 2000 iliyopita kabla ya kuumbwa mwanadamu,wao wanatuona sisi hatuwaoni,Jini ameumbwa kutokana na moto binadamu ameumbwa kutokana na mchanga na maraika wameubwa kutokana na nuru na kuna tofauti kati ya jini na shetani,jini akiwa mbaya anaitwa shetani

Majini huka wapi?majini wanapenda kuishi sehemu tulivu ambazo hawakai watu,vilevile wanapenda kukaa katika misitu mikubwa na majabali,vilevile wanaweza kukaa pamoja na watu majumbani mwao. Wengine wanapendelea kukaa chooni, lakini hawakai chooni wale majini waisilamu bali ni wale makafiri wachafu ambao wanapenda vitu najisi vichafuvichafu. Ndiyo maana kwa Waisilamu kuna dua huwa inafundishwa ambayo unapoingia chooni inabidi uisome ili usipatwe na jini, na sehemu za baharini majini wanapendelea sana kuishi

Na kuna aina tatu ya majini aina ya kwanza majini wenye mabawa na wanaweze kuruka,
aina ya pili ni wale ambao unaweza kuona joka au ng'e,. Aina ya tatu ni wale ambao wana hamahama kwenda maumbile mengine na majini nao wana sheria ambazo zinawabana kama binadamu. Mfano wanapaswa kumtii Mungu na kuswali. Wanapaswa kumtii mtume kama vile binadamu tunavyofanya, kwenda Makka kama sisi tunavyofanya, kama vile Muisilamu inavyobidi kufanya na majini nao inabidi kufanya hivyo

Majini wanawagopa sana binadamu tofauti na binadamu wanavyowagopa, na ukiwaogopa unawapa kichwa, na ndiyo maana katika Uisilamu kuna dua za kujikinga na majini, na wana tabia kama unavyoziona za wanadamu. Kuna majini wacha Mungu, wezi, malaya mashoga, na hata washirikina. Yaani kila tabia uliyonayo mwanadamu basi na majini wanayo
Sawa
 
Back
Top Bottom