Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 57,595
- 215,272
Zanzibar mwaka 1200
HISTORIA YA NENO ZANZIBAR:Ukweli ni kwamba kila kilichopo hapa duniani kina historia yake. Na ifahamike kuwa kabla ya kuja kwa wageni katika bara la Afrika, kila kitu kIlikuwa na jina lake. Na majina mengi yaliyokuwepo na mengine bado yalikuwa na huhusiano wa karibu sana na jamii za kiafrika.
Lakini mara baada ya ujio wa wageni kulikuwa na utajaji mpya wa baadhi ya maeneo . Na hii ilisababishwa na wageni kuwa na taaluma ya uandishi. Na zaidi ya hapo kulikuwa na maeneo ambayo yalipata majina mengi kwa wakati tofautitofauti kulingana na ujio wa wageni. Mfano ,mzuri ni kisiwa cha Zanzibar.
Hapa inatupasa tuelewe kuwa tunachokiangalia hapa ni neno Zanzibar na habari za Unguja tutaangalia kwa upande mwingine. Ifahamike kuwa wakazi wa kwanza kuishi kisiwa cha Zanzibar ni Wabantu, na kwa mujibu wa Prof. Chami aliyefanya tafiti zake Zanzibar alitoa ushahidi wa uwepo kwa makabila ya kibantu katika maeneo hayo kabla ya wageni miaka ya 600 BK/BM.
Neno Zanzibar lina maana ya eneo lote la Pwani linalopatikana kuanzia kusini mwa Somalia( Mto Juba) hadi maeneo ya Msumbiji. Kabla ya kuitwa Zanzibar, hapo mwanzoni kwa mujibu wa wageni walipaita Zanji/Zenji/Zinji kwenye miaka ya 1200 bila kuongeza “Bar”, wakiwa na maana ya Watu Weusi.
Na kwenye vita vya Kiislamu huko Asia miaka ya 700, kulichukuliwa Waafrika zaidi ya 400 kutoka Pwani ya Zanji na walifahamika kwa jina la Wazanji. Kwa uchanganuzi tu neno zanji kwa Kiswahili ni Zanchi yaani nchi ya Za. Ikiwa na maana ya Za- maeneo yote yaliyozunguukwa bahari ya Hindi. Na neno Chi au Nji lina maana ya ardhi.
Kwa hapo tukapata maana ya watu weusi walikuwa wakiishi kwenye ardhi (kisiwa) kilichozunguukwa na bahari ya Hindi. Na baadae kwenye maiaka ya 1200/1300 Waarabu walitaka kutofautisha baadhi ya watu wakaongeza neno “Bar” ikiwa na maana ya ardhi inayomilikiw na wa Zanji. Na hivyo kupata Zanjibar au Zanjbar.
Na hata ushahidi wa maandiko ya Ibn Hawqal yalionesha kuwa mji huo ulifahamika kama Zangbar kutokana na maandishi na matamshi yake. Na hata kwenye karne ya 12 sawa na miaka ya 1100 kwenye maandiko ya Al-Idris aliandika Zangbar ikiwa na maana ile ile.
Na hata Wachina walipofika maeneo hayo waliyatambua kwa jina la (Ts’ong-pa) ikiwa na maana ya Zangbar. Na mpaka Wareno walipofika maeneo hayo kama Vasco Da Gama na Marco Polo walitambua eneo kama Unguja. Hivyo neno Unguja lilikuja kufahamika mara baada ya ujio wa Wareno.
Tukiachan na habari za Unguja, turudi kwenye suala zima la Zangbar. Historia inafafanua kuwa Zanzibar ilikuwa chini ya uangalizi wa Mwingereza kuanzia miaka 1890, na wakati huo Wazungu walipatambua kama Zanzibar, ili kurahisisha matamshi ya kiingereza. Zanzibar ilipata uhuru mwaka 1963 na uhuru huo ulikuwa wa wachache. Mnamo miaka ya 1964 kulifanyika mapinduzi kisiwani hapo. Na mwaka huohuo mwezi wa 4, Zanzibar iliungana na Tanganyika na kuunda Tanzania.
Mchakato ulikuwa hivi, zilichuliwa herufi 3 za mwanzo kutoka kwenye kila neno, yaani Tan-kutoka Tanganyika na Zan –kutoka Zanzibar na kupata Tan+zan-. Na mwisho kuchua herufi zilizobakia yaani kutoka Zanzibar tukapata –a- na Tanganyika tukapata –i- na mwisho tukapata –ia- na kuzaa neno Tanzania. Na hii ilifanywa na Hayati, Julius Kambarage Nyerere na Hayati Aman Abeid Karume. Ukweli ni kwamba licha ya changamto nyingi muungano huu una faida sana kwa nchi hizi.