Historia ya kina Zanzibar

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,595
215,272
1592717849721.png

Zanzibar mwaka 1200

HISTORIA YA NENO ZANZIBAR:Ukweli ni kwamba kila kilichopo hapa duniani kina historia yake. Na ifahamike kuwa kabla ya kuja kwa wageni katika bara la Afrika, kila kitu kIlikuwa na jina lake. Na majina mengi yaliyokuwepo na mengine bado yalikuwa na huhusiano wa karibu sana na jamii za kiafrika.

Lakini mara baada ya ujio wa wageni kulikuwa na utajaji mpya wa baadhi ya maeneo . Na hii ilisababishwa na wageni kuwa na taaluma ya uandishi. Na zaidi ya hapo kulikuwa na maeneo ambayo yalipata majina mengi kwa wakati tofautitofauti kulingana na ujio wa wageni. Mfano ,mzuri ni kisiwa cha Zanzibar.

Hapa inatupasa tuelewe kuwa tunachokiangalia hapa ni neno Zanzibar na habari za Unguja tutaangalia kwa upande mwingine. Ifahamike kuwa wakazi wa kwanza kuishi kisiwa cha Zanzibar ni Wabantu, na kwa mujibu wa Prof. Chami aliyefanya tafiti zake Zanzibar alitoa ushahidi wa uwepo kwa makabila ya kibantu katika maeneo hayo kabla ya wageni miaka ya 600 BK/BM.

Neno Zanzibar lina maana ya eneo lote la Pwani linalopatikana kuanzia kusini mwa Somalia( Mto Juba) hadi maeneo ya Msumbiji. Kabla ya kuitwa Zanzibar, hapo mwanzoni kwa mujibu wa wageni walipaita Zanji/Zenji/Zinji kwenye miaka ya 1200 bila kuongeza “Bar”, wakiwa na maana ya Watu Weusi.

Na kwenye vita vya Kiislamu huko Asia miaka ya 700, kulichukuliwa Waafrika zaidi ya 400 kutoka Pwani ya Zanji na walifahamika kwa jina la Wazanji. Kwa uchanganuzi tu neno zanji kwa Kiswahili ni Zanchi yaani nchi ya Za. Ikiwa na maana ya Za- maeneo yote yaliyozunguukwa bahari ya Hindi. Na neno Chi au Nji lina maana ya ardhi.

Kwa hapo tukapata maana ya watu weusi walikuwa wakiishi kwenye ardhi (kisiwa) kilichozunguukwa na bahari ya Hindi. Na baadae kwenye maiaka ya 1200/1300 Waarabu walitaka kutofautisha baadhi ya watu wakaongeza neno “Bar” ikiwa na maana ya ardhi inayomilikiw na wa Zanji. Na hivyo kupata Zanjibar au Zanjbar.

Na hata ushahidi wa maandiko ya Ibn Hawqal yalionesha kuwa mji huo ulifahamika kama Zangbar kutokana na maandishi na matamshi yake. Na hata kwenye karne ya 12 sawa na miaka ya 1100 kwenye maandiko ya Al-Idris aliandika Zangbar ikiwa na maana ile ile.

Na hata Wachina walipofika maeneo hayo waliyatambua kwa jina la (Ts’ong-pa) ikiwa na maana ya Zangbar. Na mpaka Wareno walipofika maeneo hayo kama Vasco Da Gama na Marco Polo walitambua eneo kama Unguja. Hivyo neno Unguja lilikuja kufahamika mara baada ya ujio wa Wareno.

Tukiachan na habari za Unguja, turudi kwenye suala zima la Zangbar. Historia inafafanua kuwa Zanzibar ilikuwa chini ya uangalizi wa Mwingereza kuanzia miaka 1890, na wakati huo Wazungu walipatambua kama Zanzibar, ili kurahisisha matamshi ya kiingereza. Zanzibar ilipata uhuru mwaka 1963 na uhuru huo ulikuwa wa wachache. Mnamo miaka ya 1964 kulifanyika mapinduzi kisiwani hapo. Na mwaka huohuo mwezi wa 4, Zanzibar iliungana na Tanganyika na kuunda Tanzania.

Mchakato ulikuwa hivi, zilichuliwa herufi 3 za mwanzo kutoka kwenye kila neno, yaani Tan-kutoka Tanganyika na Zan –kutoka Zanzibar na kupata Tan+zan-. Na mwisho kuchua herufi zilizobakia yaani kutoka Zanzibar tukapata –a- na Tanganyika tukapata –i- na mwisho tukapata –ia- na kuzaa neno Tanzania. Na hii ilifanywa na Hayati, Julius Kambarage Nyerere na Hayati Aman Abeid Karume. Ukweli ni kwamba licha ya changamto nyingi muungano huu una faida sana kwa nchi hizi.
 
Tukiachan na habari za Unguja, turudi kwenye suala zima la Zangbar. Historia inafafanua kuwa Zanzibar ilikuwa chini ya uangalizi wa Mwingereza kuanzia miaka 1890, na wakati huo Wazungu walipatambua kama Zanzibar, ili kurahisisha matamshi ya kiingereza. Zanzibar ilipata uhuru mwaka 1963 na uhuru huo ulikuwa wa wachache. Mnamo miaka ya 1964 kulifanyika mapinduzi kisiwani hapo. Na mwaka huohuo mwezi wa 4, Zanzibar iliungana na Tanganyika na kuunda Tanzania.

Huo uhuru wa wachache ni upi? Acha kuishi kwa propaganda za CCM dada
 
Mzee aliwahi kuufananisha muungano kama koti, akadai kwamba unapovaa koti halafu jua likawa kali sana basi unalivua koti na kulitundika kwenye msumari.

Maskini ya Mungu mzee wa watu alipohisi joto ni kali na kutaka kulivua koti alitundike kwenye msumari akajikuta yeye ndie ametundikwa msumarini.

Mzee alichokua hakitambui kua anaingia rasmi kwenye ndoa ya kikristo, ndoa ya shida na raha mpaka kifo kitutenge.
 
Why tunalazimisha huu Muungano I don't know.
Pole yao wanaohisi joto kali na kulazimishwa kuvaa Koti.

Mkataba walioingia babu yao na babu yetu hauna tofauti na ule mkataba alioingia chifu Mangungo na wajeremani (Karl Peter's)

Babu yao aliwauzia wakoloni ardhi yao bila ya kujua.
 
Na hii ikoje mkuu kihistoria, watu wa Pemba na unguja kuna chuki Fulani ya ndani ya nafasi zao? Hebu nipe history yao mkuu, kabla ya ukoloni na baada ya kuja sultani.

Chuki za upemba na Unguja zimeletwa na CCM mkuu hazikuepo huko nyuma, na sababu kuu ni kuwa wapemba wameikataa CCM hilo ndi kosa laao na ndio sababu ya kubaguliwa.
 
Na hii ikoje mkuu kihistoria, watu wa Pemba na unguja kuna chuki Fulani ya ndani ya nafasi zao? hebu nipe history yao mkuu, kabla ya ukoloni na baada ya kuja sultani.
Kikubwa wapemba wengi wanawachukulia waunguja kama wasaliti, hii ni kutokana na yale mapinduzi ambayo yaligharimu damu za ndugu zao wengi.
 
Kikubwa wapemba wengi wanawachukulia wazanzibari kama wasaliti, hii ni kutokana na yale mapinduzi ambayo yaligharimu damu za ndugu zao wengi.
Mkuu sijakuelewa,,, kwani mpemba ni nani na mzanzibar ni nani? Ninachofahamu unguja na Pemba ndy imezaa Zanzibar.. kwahyo unataka kunambiya wapemba na waunguja ni wapi walioumizwa na mapinduzi Yale? ndy nataka kujifunza chuki yao imeletwa na nn?
 
Chuki za upemba na Unguja zimeletwa na CCM mkuu hazikuepo huko nyuma, na sababu kuu ni kuwa wapemba wameikataa CCM hilo ndi kosa laao na ndio sababu ya kubaguliwa.
Kwahyo mkuu unataka kunambiya wakati wa ASP hakukuwa na chuki hizo?
 
Kwahyo mkuu unataka kunambiya wakati wa ASP hakukuwa na chuki hizo?

Hazikuepo mkuu, na ASP ilikwishwa kataliwa Pemba, uchaguzi wa mwisho kabla ya uhuru iliishia kupata majimbo mawili tu tena ya ushindi mwembamba sana. na ndio mana baada ya mapinduzi wapemba walianza kutengwa kwenye uongozi wa ASP kichinichini mpaka yalipokuja kuwa ya dhahiri miaka ya 80.
 
Mkuu sijakuelewa,,, kwani mpemba ni nani na mzanzibar ni nani? Ninachofahamu unguja na Pemba ndy imezaa Zanzibar.. kwahyo unataka kunambiya wapemba na waunguja ni wapi walioumizwa na mapinduzi Yale? ndy nataka kujifunza chuki yao imeletwa na nn?

Samahani mkuu kwa kuchanganya ila tayari hapo juu nimesahihisha.
Nilimaanisha baina ya wapemba na waunguja.
Kikubwa chuki ipo kimremngo wa kisiasa zaidi, wapemba wengi wanawatuhumu waunguja katika usaliti wa kuipindua serikali iliyokua madarakani na kuungana na Tanganyika.
Wapemba wengi hawakuona umuhimu na sababu za msingi katika mapinduzi yale yaliosababisha damu za watu kupotea.
 
Mkuu sijakuelewa,,, kwani mpemba ni nani na mzanzibar ni nani? Ninachofahamu unguja na Pemba ndy imezaa Zanzibar.. kwahyo unataka kunambiya wapemba na waunguja ni wapi walioumizwa na mapinduzi Yale? ndy nataka kujifunza chuki yao imeletwa na nn?

ASP chama kilichokua kina nguvu Unguja, Pemba kulikua na chama cha ZPPP ndicho kilichokua na nguvu, Huku chama cha ZNP kikiwa na wafuasi sehemu zote Unguja na Pemba. ZNP na ZPPP viliunguna na wakawa wanasimamisha mgombea mmoja kwenye majimbo kama walivofanya UKAWA 2015. mapinduzi ya 64 yalikua ni kupindua serekali ya ZPPP/ZNP nasio sultan kama tunavyoaminishwa. Sultan alikua ni mkuu wa nchi tu bali kiongozi wa Serekali alikua Mohamed Shamte ambaye anatoka kwenye muungano wa vyama hivyo.
Kwahiyo wapemba hawakuyasapoti mapinduzi ya 64 kwa kuwa serekali iliyopinduliwa wao walikua wakiisapoti na wao ndio walioipigia kura kuiweka madarakani.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom