Meja M
JF-Expert Member
- Oct 4, 2016
- 628
- 560
Habarini za mida hii wakuu..!!
Natanguliza pole kwa mihangaiko ya siku nzima ili mradi tu mkono uende kinywani..!!
Ilikuwa mwaka 1999 nikiwa shule ya msingi likizo ilinibidi nikamtembelee bibi na babu kizaa mama angu huko kijiji cha Nyakagomba Butundwe wilayani Geita, katika kijiji hiki watu waliishi maisha ya ujamaa sana.
Wiki ya kama ya pili hivi nikiwa kwa bibi yangu nakumbukuka ilikuwa siku ya Jumapili jioni kama saa kumi na mbili hivi alikuja mgeni ambaye alikuwa ni rafiki ake babu wa muda mrefu walikaa na kuzungumza mambo yao kama mnavyojua watoto hatukuruhusiwa kusogea karibu watu wakubwa wakiwa wanazungumza.
Walizungumza stori zao mpaka mida ya kama saa moja hivi ki giza kilianza kuingia, yule mgeni aliiga na kuondoka kama ilivyo desturi babu alimsindikiza mgeni wake lakini kitu cha ajabu babu hakurudi, ilipofika mida ya kama saa nne hivi wasiwasi ukatawala pale nyumbani.
Wajomba zangu walimtafuta sana mpaka kwa yule rafiki ake lakini rafiki ake alidai kwamba waliagana na alirudi nyumbani, juhudi za kumtafuta ziliendelea kwa kushirikiana na wanakijiji wengine lakini hakuna lililofanikiwa.
Siku ya pili baada ya babu kutoweka ilibidi tu tuweke msiba na kuamini amefariki kama ilivyokawaida huko kijijini walitengeneza kaburi kama ishara ya kuwa alifariki.
Baada ya siku kama sita hivi tangu ametoweka ilikuwa ni usiku mida ya kama saa mbili hivi tukiwa tunakula tulisikia hodi alitoka mjomba wangu na alipofungua alikuta ni babu, mjomba yule alikimbia kwani wote tulimuogopa lakini babu alitusihi tusimuogope aliomba maji ya kunywa kisha akaomba akapumzike.
Siku ilifuata asubuhi alituita wote na kuanza kutusimulia ilivyokuwa. Anasema alipokuwa anatoka kumsindika huyo rafiki ake alijikuta anatokea katika njia ambayo hakuielewa japo alidai ilifanana na njia aliyopita akimsindikiza mgeni wake lakini kitu cha ajabu alijikuta ametokea sehemu ambayo haikuielewa kabisa japo kulikuwa na watu waliokuwa wanamshangaa sana kwa jinsi alivyokuwa pia alidai walikuwa wanazungumza lugha ambayo hakuielewa kabisa hawakuwa tofauti na binadamu wa kawaida ila kwa jinsi alivyodai ilionesha kama walikuwa hawaamini kama kuna binadamu kama wao.
Mwisho alidai hakukumbuka ilikuaje mpaka akajikuta yupo kijijini kwake tena. Baada ya kutusimulia alifariki siku iliyofuata.
Mpaka leo nikiwa mtu mzima sielewi kabsa tukio hili. !!
Natanguliza pole kwa mihangaiko ya siku nzima ili mradi tu mkono uende kinywani..!!
Ilikuwa mwaka 1999 nikiwa shule ya msingi likizo ilinibidi nikamtembelee bibi na babu kizaa mama angu huko kijiji cha Nyakagomba Butundwe wilayani Geita, katika kijiji hiki watu waliishi maisha ya ujamaa sana.
Wiki ya kama ya pili hivi nikiwa kwa bibi yangu nakumbukuka ilikuwa siku ya Jumapili jioni kama saa kumi na mbili hivi alikuja mgeni ambaye alikuwa ni rafiki ake babu wa muda mrefu walikaa na kuzungumza mambo yao kama mnavyojua watoto hatukuruhusiwa kusogea karibu watu wakubwa wakiwa wanazungumza.
Walizungumza stori zao mpaka mida ya kama saa moja hivi ki giza kilianza kuingia, yule mgeni aliiga na kuondoka kama ilivyo desturi babu alimsindikiza mgeni wake lakini kitu cha ajabu babu hakurudi, ilipofika mida ya kama saa nne hivi wasiwasi ukatawala pale nyumbani.
Wajomba zangu walimtafuta sana mpaka kwa yule rafiki ake lakini rafiki ake alidai kwamba waliagana na alirudi nyumbani, juhudi za kumtafuta ziliendelea kwa kushirikiana na wanakijiji wengine lakini hakuna lililofanikiwa.
Siku ya pili baada ya babu kutoweka ilibidi tu tuweke msiba na kuamini amefariki kama ilivyokawaida huko kijijini walitengeneza kaburi kama ishara ya kuwa alifariki.
Baada ya siku kama sita hivi tangu ametoweka ilikuwa ni usiku mida ya kama saa mbili hivi tukiwa tunakula tulisikia hodi alitoka mjomba wangu na alipofungua alikuta ni babu, mjomba yule alikimbia kwani wote tulimuogopa lakini babu alitusihi tusimuogope aliomba maji ya kunywa kisha akaomba akapumzike.
Siku ilifuata asubuhi alituita wote na kuanza kutusimulia ilivyokuwa. Anasema alipokuwa anatoka kumsindika huyo rafiki ake alijikuta anatokea katika njia ambayo hakuielewa japo alidai ilifanana na njia aliyopita akimsindikiza mgeni wake lakini kitu cha ajabu alijikuta ametokea sehemu ambayo haikuielewa kabisa japo kulikuwa na watu waliokuwa wanamshangaa sana kwa jinsi alivyokuwa pia alidai walikuwa wanazungumza lugha ambayo hakuielewa kabisa hawakuwa tofauti na binadamu wa kawaida ila kwa jinsi alivyodai ilionesha kama walikuwa hawaamini kama kuna binadamu kama wao.
Mwisho alidai hakukumbuka ilikuaje mpaka akajikuta yupo kijijini kwake tena. Baada ya kutusimulia alifariki siku iliyofuata.
Mpaka leo nikiwa mtu mzima sielewi kabsa tukio hili. !!