Hili tangazo ITV sio zuri

Hili tangazo ITV sio zuri

Duh nlikuwa sijui kama kutusua ndo lina maana hyo.....sasa watt wanaelewa maana unayoijua ww?? Au na ww unashiriki katika kulisambaza na kulipa maana mbaya?? Fikiri kabla ya kuropoka bhana.
 
Kutusua enzi zetu maana yake ni kunyofoa nyama toka kwa mfupa ama nyama kubwa kwa kutumia meno ili ule vipande vidogo vidogo. Kama washika nyama kwa mkono unatusua kwa meno ya mbele kwa kuila mpaka inaisha.

Jamaa kwenye ile paper si katusua!
 
kutusua ni kutoboa ,sasa itategemea unatoboa nini.
Ni kutoka,''breakthrough'' kupata upenyo.
 
Kila neno ukitafsiri utapata maana tofauti kutokana na jamii, rika au kundi flani wanavolitumia....mbona huku JF maneno ya kawaida yamepewa maana tofauti na ufaham wangu..mfano neno tiGo, kibamia, mhogo, n.k yanatumika tofauti
Hivyo kutusua pia inaweza eleweka tofauti kutokana na aina ya jamii inayowasiliana kwa kuzingatia muktadha, umri wa hao watu, eneo, na categories nyinginezo
 
Kuna Tangazo linatoka ITV la TMT linalosema mpaka utusue, mpaka kieleweke, mpaka ukome. Sasa hili neno 'mpaka utusue' maana yake nini? Kwa sisi wa miaka hiyo, hili neno lina maana mbaya, na ubaya tangazo hili mpaka watoto wanaangalia.

Kutusua ina maana mbaya ipi??
 
Hilo neno "tusua" au "kutusua" halipo kwenye kamusi ya kiswahili sanifu labda ni neno la msimu la mtaani la enzi hizo sasa limerudi tena.
 
Duh nlikuwa sijui kama kutusua ndo lina maana hyo.....sasa watt wanaelewa maana unayoijua ww?? Au na ww unashiriki katika kulisambaza na kulipa maana mbaya?? Fikiri kabla ya kuropoka bhana.

Walewale wa kugegeda.
Kikwetu kugegeda ni kutafuna, sasa kutafuna sijui ni tusi.
 
Walewale wa kugegeda.
Kikwetu kugegeda ni kutafuna, sasa kutafuna sijui ni tusi.

Kutafuna nn?? Maana siku hizi kila neno linaelekezwa kwanza kwny maana yake mbaya kisha wanakutaka ufafanue kama ndiyo uliyomaanisha.
 
Meneno yanabadilika maana na matumizi kuendana na wakati na hata mahali.

Neno 'mshikaji' pia lilikuwa na hali ya utusi lakini sasa hivi linatumika tu tena baina ya jinsia ya kiume (mwanaume kwa mwanaume wanaitana mshikaji!).

Shoga, pia linabadilika maana na mpaka sasa kuna baadhi ya maeneno wanalitumia confortably wakimaanisha 'rafiki' (mfano unaweza kuulizwa "wale shoga zako umemwacha wapi"?). Wanawake wao wanalitumia katika kuitana wao kwa wao.

Hata salamu hii "mambo!" wakati inaaza haikukubalika sana (ilikuwa na "ukakasi" hivi) hasa baina ya watu waliopishana rika, lakini sasa naona inakubalika tu (ingawa bado sio katika matumizi rasmi).
 
Mimi nipo hapa Bongo kitambo sana, sasa nina miaka 50 hivi. Hili neno KUTUSUA lilitumika sana miaka ile ya 1980.Manayake kiukweli wakati ule ni KUGEGEDA mwanamke.Kwa kuhitimisha ni kuwa KUTUSUA (1980) = KUGEGEDA (2015)
 
Kutusua ni lugha tuliyokuwa tunaitumia miaka hiyo ukipata demu ukalala naye ( kufanya naye mapenzi) ndio unasema umemtusua lilikuwa neno la kawaida sana kwa vijana wakati huo...... Maana yake ndio hiyo hata kama hutaki ITV wasitishe hili tangazo sio zuri linafaa kule kwa wakubwa
 
Kutafuna nn?? Maana siku hizi kila neno linaelekezwa kwanza kwny maana yake mbaya kisha wanakutaka ufafanue kama ndiyo uliyomaanisha.

Kutafuna huelewi?
Ukila hutafuni? Baadae hadi kula litakua tusi.
 
Back
Top Bottom