Tulio wengi tunajua kuwa kulikuwa na uchaguzi mdogo wa madiwani katika kata 26 ambapo kata 4 za Arusha mjini uchaguzi huo ulihairishwa kufanyika kutokana na mlipuko wa bomu lililo pelekea watu wawili kufariki na wengine 70 kujeruhiwa.
Mimi katika uchaguzi huo nimeliona anguko la CCM katika maeneo yafuatayo:-
1. Chama kikongwe kinachoshika dola kimeweza kupoteza tena kata 5 ambazo kilikuwa kinazishikilia zimechukuliwa na CHADEMA huku CHADEMA wakitetea 2 za kwao walizokuwa wanazishikilia, hilo kwao ccm ni anguko, hawapandi bali wanashuka
2. Anguko la pili na baya zaidi ni lile la kuporomoka kwa maadili , sasa maadili hayapo tena ndani ya ccm, watu wanaropoka ovyo ovyo na kutukana matusi badala ya kujenga hoja kwa kueneza sera za chama chao, pia wameonekana wakitoa rushwa wazi wazi za chumvi, pesa n.k, na hiyo ikapelekea kuumbuka kwa Waziri Mary nagu kule babati walipokamatwa na yule Mbunge wa babati na vijana wa CHADEMA, hilo ccm wamelifanya maeneo mengi sana. Na watu nao katika kuripoti wakaandika Waziri Mary Nagu na Jeetuson yule Mbunge mwingine mwanaume wafumaniwa, niliposikia ghafla nikashituka na nilipofuatilia zaidi kumbe ilikuwa ni fumanizi la kutoa rushwa ya pesa na ndipo nikauzunika sana, nikajiuliza iko wapi ile miiko ya tanu maana kipengele Na. kinasema RUSHWA NI ADUI WA HAKI SITAPOKEA WALA KUTOA RUSHWA
3. Kukosekana kwa uvumilivu wa kisiasa, ni hatari kubwa hilo wasipoliangalia vizuri taifa sasa linaenda kuhangamia kuelekea uchaguzi 2015, kwa waliosoma magazeti na wengine kushuhudia ccm wamekwisha kumwaga damu nyingi za watanzania wasiokuwa na hatia kwa kuwajeruhi kila kona kuliko kuwa na uchaguzi huu mdogo, kutegemea vitisho na kumwaga damu ili ushinde bila kufanya hivyo ushindi, hilo ni anguko pia
4. CCM imeaza kupoteza mvuto katika maeneo muhimu ambayo zilikuwa ndiyo ngome zao kuu, maeneo niliyoyashuhudia ccm ikipoteza mvuto huo wa kisiasa ni pamoja na Tanga, Morogoro, Singida n.k. Tanga ccm imeshinda kata zote mbili lakini shaka ninayoipata ni ile tafauti ya kura za ushindi, kata moja wamepishana na CHADEMA kwa kura 19, na kata nyingine wamepishana tena na CHADEMA kwa kula zisizoziidi 30
Kwa haya niliojaribu kuainisha kwa anayeweza kuyaangalia kwa kina bila kujali ushabiki wa kisiasa yanaashiria dalili mbaya mno kwa ccm kuelekea uchaguzi 2015.
Watanzania naomba tukumbushane kitu kimoja , Kitakwimu ccm maeneo ya mijini na majiji kwa sasa haishindi kirahisi, mfano halisi ni katika matokeo haya ya chaguzi hizi ndogo. Hebu jaribu kuangalia kata walizoshinda ccm ni za vijini karibu zote. Kitawimu nimejaribu kuaangalia matokeo ya sensa ya mwaka huu karibu wilaya zoze angalau zaidi ya nusu ya wakazi katika Wilaya yoyote ile. utakawakuta wanaishi aidha katika makao makuu ya wilaya na wengine katika miji midogo iliyopo ndania ya Wilaya.
Ukitaka kuthibitisha hili jaribu kufuatilia kwa nini majimbo mengi ambayo CHADEMA na NCCR Mageuzi walishinda walishindwa kuwa na madiwani wengi na kuunda uongozi kuendesha halmashauri hizo. jibu ni kwamba ushindi wao kwa kiasi kikubwa ulibebwa na kata zile chache zenye watu wengi wanaoishi maeneo hayo niliyoyataja
Kwa kuhitimisha CCM hamko salama kabisa kuelekea 2015, mtakuja kushangazwa na msiamini kitakachokuja kutokea, maana nyinyi mmezoea siasa za majitaka pasipokufanya utafiti wa kina
Mimi katika uchaguzi huo nimeliona anguko la CCM katika maeneo yafuatayo:-
1. Chama kikongwe kinachoshika dola kimeweza kupoteza tena kata 5 ambazo kilikuwa kinazishikilia zimechukuliwa na CHADEMA huku CHADEMA wakitetea 2 za kwao walizokuwa wanazishikilia, hilo kwao ccm ni anguko, hawapandi bali wanashuka
2. Anguko la pili na baya zaidi ni lile la kuporomoka kwa maadili , sasa maadili hayapo tena ndani ya ccm, watu wanaropoka ovyo ovyo na kutukana matusi badala ya kujenga hoja kwa kueneza sera za chama chao, pia wameonekana wakitoa rushwa wazi wazi za chumvi, pesa n.k, na hiyo ikapelekea kuumbuka kwa Waziri Mary nagu kule babati walipokamatwa na yule Mbunge wa babati na vijana wa CHADEMA, hilo ccm wamelifanya maeneo mengi sana. Na watu nao katika kuripoti wakaandika Waziri Mary Nagu na Jeetuson yule Mbunge mwingine mwanaume wafumaniwa, niliposikia ghafla nikashituka na nilipofuatilia zaidi kumbe ilikuwa ni fumanizi la kutoa rushwa ya pesa na ndipo nikauzunika sana, nikajiuliza iko wapi ile miiko ya tanu maana kipengele Na. kinasema RUSHWA NI ADUI WA HAKI SITAPOKEA WALA KUTOA RUSHWA
3. Kukosekana kwa uvumilivu wa kisiasa, ni hatari kubwa hilo wasipoliangalia vizuri taifa sasa linaenda kuhangamia kuelekea uchaguzi 2015, kwa waliosoma magazeti na wengine kushuhudia ccm wamekwisha kumwaga damu nyingi za watanzania wasiokuwa na hatia kwa kuwajeruhi kila kona kuliko kuwa na uchaguzi huu mdogo, kutegemea vitisho na kumwaga damu ili ushinde bila kufanya hivyo ushindi, hilo ni anguko pia
4. CCM imeaza kupoteza mvuto katika maeneo muhimu ambayo zilikuwa ndiyo ngome zao kuu, maeneo niliyoyashuhudia ccm ikipoteza mvuto huo wa kisiasa ni pamoja na Tanga, Morogoro, Singida n.k. Tanga ccm imeshinda kata zote mbili lakini shaka ninayoipata ni ile tafauti ya kura za ushindi, kata moja wamepishana na CHADEMA kwa kura 19, na kata nyingine wamepishana tena na CHADEMA kwa kula zisizoziidi 30
Kwa haya niliojaribu kuainisha kwa anayeweza kuyaangalia kwa kina bila kujali ushabiki wa kisiasa yanaashiria dalili mbaya mno kwa ccm kuelekea uchaguzi 2015.
Watanzania naomba tukumbushane kitu kimoja , Kitakwimu ccm maeneo ya mijini na majiji kwa sasa haishindi kirahisi, mfano halisi ni katika matokeo haya ya chaguzi hizi ndogo. Hebu jaribu kuangalia kata walizoshinda ccm ni za vijini karibu zote. Kitawimu nimejaribu kuaangalia matokeo ya sensa ya mwaka huu karibu wilaya zoze angalau zaidi ya nusu ya wakazi katika Wilaya yoyote ile. utakawakuta wanaishi aidha katika makao makuu ya wilaya na wengine katika miji midogo iliyopo ndania ya Wilaya.
Ukitaka kuthibitisha hili jaribu kufuatilia kwa nini majimbo mengi ambayo CHADEMA na NCCR Mageuzi walishinda walishindwa kuwa na madiwani wengi na kuunda uongozi kuendesha halmashauri hizo. jibu ni kwamba ushindi wao kwa kiasi kikubwa ulibebwa na kata zile chache zenye watu wengi wanaoishi maeneo hayo niliyoyataja
Kwa kuhitimisha CCM hamko salama kabisa kuelekea 2015, mtakuja kushangazwa na msiamini kitakachokuja kutokea, maana nyinyi mmezoea siasa za majitaka pasipokufanya utafiti wa kina