Hili linanitatiza

Ushauri mzuri pia. Unajua mara nyingi binadamu tunapotoa ushauri huwa tunatengeneza bias na kukupa ushauri kuonyesha kuwa tatizo liko kwa wengine na mara chache sana watu wanafikiria kukupa ushauri kuonyesha kuwa labda wewe ndio tatizo.

Sisi wanasheria tumeligundua hili mara nying sana tunapowashauri wateja wetu. Mara nyingi mteja anakuja akidai kuwa kaonewa na mwenzi wake lakini ukichunguza sana unakuja kugundua kuwa mteja wako ndiye tatizo na unaanza kazi ya damage litigation.
Wengi wamesaidia kukupa mchango mzuri wa mawazo nakuomba kwa yale mema basi yafanyie kazi.

Unajua hakuna kitu kinachouma kama unampenda mtu na ukaona mhusika haguswi hata kidogo kuthamini upendo unao-mpa hadi inafikia hatua unakuwa-bitter as you said.

Ushauri ni huu: Wala usipoteze muda, fanya uchunguzi wa kina utabaini ukweli. Umesema upo mkoa wa jirani na Dar, sasa kama una-moyo wa ujasiri sema hivi: panga safari ya kustukiza nenda kwa mume wako-dar lakini endapo nitamkuta na mwanamke mwingine zaidi yako usiwe na hasira yeyote ile-na umuombe mungu akuongoze vema- muda wa kufika home iwe ni usiku atleast saa 4 hivi piga hodi home au kama una-funguo spare we fungua mlango choma ndani.

Kama ukimkuta yupo alone take easy tu, akiuliza mwambie gari iliharibika ndio maana nimekuja muda huu, ukimkuta na mwanamke mwingine wewe wala usijali-take simple na uone je huyo mwanamke atalala humo ndani au itakuaje na yeye je atasema nini? Wewe lala asubuhi amka kama usafi fanya kisha muandalie chai anywe! Sasa mwambie tena kwa mahaba dah mume wangu nakupenda sana na muonyeshee kweli unampenda. Sasa utaona jinsi atakavyokuwa anajikanyaga kutaka kusawazisha mambo yake wakati wewe hujamuuliza. Hapo jibu utakuwa umelipata na yeye hatarudia huo mchezo kama anao. Still bado nadhani kwa uhakika kutakuwa ma mwanamke ambaye wewe anakufahamu fika na anajua upo mkoani hivyo yeye anaona ni bora au muda muafaka kufanya apendavyo na mumeo.

Nimeongea hilo kwa sababu ya uzeefu niliokuwa nao wa kubaini matatizo madogo madogo kama ya mapenzi ambayo wengi huwa wanatatizwa nayo.

NB: If you will do that, plse usiwe na hasira hata chembe na umuombe mungu wako akuongoze ili hatimaye ujue u-kweli na hata ukijua bado mume wako utampenda zaidi ili yeye ajione mjinga na kisha ajirudi
 
Dada Rain,
Tatizo lako kwa kweli tunalo wengi tulioolewa. Mimi pia nina tatizo kama lako maana niko mkoani na mume wangu yuko Dar. Ni mtu mwema sana na aliyetokea kunipenda sana zamani lakini amepunguza sana upendo. Mwanzoni nilianza kufikiria kuwa kuna watu wananisaidia (kama wengi wanajf wanavyokwambia) na nikafanya safari nyingi tu za ghafla za usiku wa manane na za asubuhi lakini wap sikuwahi kumfumania. Actually niligundua kuwa mume wangu hakubadilisha patern yake ya maisha baada ya mimi kuondoka. Nilipochunguza sana niligundua kuwa alibaki na tabia zilezile alizokuwa nazo na actually alikuwa mpweke zaidi.(Sasa sijui kama alikuwa anaigiza lakini niligundua kitu amabcho sikuwahi kukijua kuwa mume wako is a loner n relies so much on me kama mtu wa kumpa sapoti -kitu ambaocho i must admit nilikuwa sikifanyi).

Rain dada yangu,
Wanaume ni kama Tembo. Miaka nenda miaka rudi watapita njia ileile waliyopita wakiwa watoto wadogo wakiongozana na wazazi wao. Hawabadiliki hata chembe na hata ufanye nini hutawabadilisha. Nakushauri uangalie namna alivyolelewa na jinsi wazazi wake walivyoishi. Kama ukiona anafuata patern ileile ya maisha ya wazazi wake na kuna ya mmoja wao anaifuata zaidi basi wewe fuata ile iliyo opposite na ya yule mzazi mwingine. Kwa mfano: Kama mumeo najiidentify na baba basi wewe jitahidi uwe opposite na tabia za mama mkwe (This is a golden rule).

Nitakupa mfano wa namna nilivyoweza kutatua tatizo la mimi na mume wangu.

Mume wangu alikuwa na kazi nzuri tu na mimi pia kazi yangu ilikuwa ya kawaida sana. Tilipoanza mapenzi tulikuwa na ndoto nyingi pamoja lakini kwa kuwa kuna tofauti kubwa ya kipato nilijenga dhana kuwa sitashiriki sana kwenye shughuli za familia yangu maana mimi nina kipato kidogo na yeye anacho kikubwa na anaweza kumudu gharama za kunihudumia mimi na mwanangu. Wakati huo nilikuwa naye mmoja. Kwa kuwa mimi natokea kwenye familia ya wakulima niliona sasa ni wajibu wangu baada ya kusoma kuhudumia familia yangu iliyonisomesha na kunitunza mpaka nikaolewa. Japo mimi ni mtoto wa kike na nina kaka nilidhani ni jukumu langu kuweka mkazo wa familia yangu ili nayo inyanyuke na kuwa familia ya mfano kijijini kwetu ili watu wajue kuwa wazazi wana watoto wamesoma.

Bila kujijua nikajikuta naweka concentration kwenye familia yangu na kusahau kuwa familia yangu mpya hasa mume wangu anateseka maana sasa nilikuwa wakati wote sina hela na nikaanza vituko vya kulazimisha matunzo yangu na mtoto. Nilifika wakati (usishangae) nilikuwa narudi kwa mume wangu lakini sitaki nitumie hata shilingi yangu kununua vitunguu. Kwa kuwa mume wangu hakuwa mlalamishi na labda kwa woga wa kuonekana weak akawa na yeye anaanzisha ubishi wa kutotoa matumizi hata yale ya msingi. Sote tukawa vipofu. Mimi niko busy na familia yangu na yeye yuko bize na kazi yake. Tukiwa kwenye mood tunaongea vizuri mambo mengine inagawa katu hatuongelei anything about our future together. Tukianza ugomvi tunakaa kimya hata siku tatu bila kuongea na mwisho naona ujinga naamua kurudi zangu mkoani. Tukiwa katika hali hii ya kutokuongea nilikuwa namjaribu mume wangu anipe nauli na matunzo yangu, ya mtoto na ndugu zangu ninaoishi nao mkoani lakini wapi akawa anagoma. Sikuwa najali sana maana ningeonekana dhaifu na mimi nimelelewa kujitambua kuwa ni mwanamke wa shoka asiyeshindwa kitu.

Mpaka hapo najua umeanza kuona tatizo liko wapi. Nitakuja baadaye kukueleza nini nilifanya.

malizia hii story maana naona ni nzuri sana,
 
pole sana Rain, God will make a way for you.
Jaribu kukaa naye na kumweleza zaidi kuhusu hoja zako,ikiwezekana ni bora sana kuhamia dar kikazi maana mampenzi ya mbali si mazuri
 
Back
Top Bottom