Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,709
Huyu dada alikutana na huyu mtu kwenye pati ya harusi,wote walikua waalikwa.Jamaa akamwomba huyu dada contact dada akakataa,jamaa akawa anamsumbua dada wa watu mpaka akaiona pati chungu,lakini dada akashikilia msimamo wake. . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . Sherehe ilipoisha hili lijamaa likamfuatilia yule dada mpaka nyumbani.Baada ya kupajua jamaa likawa linamsumbua dada wa watu nyumbani kwake dada akawa bado mgumu. . . . . . . . . . . . . . . . . . Juzi lilimemvizia wakati anatoka kazini,alivyofungua mlango jamaa akaingia ndani kisha likamwambia halitoki mpaka lipate jibu kwani limechoka kuteseka na penzi.Dada wa watu akaliambia kistaarabu hamhitaji kwani ana mchumba,lijamaa likaanza kufoka,likadai kwani huyo mchumba wake ana nini.Yule dada akaamua kutaka kutoka nje,likamvuta,purukushani ikatokea. . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . Dada katika ile purukushani akaona anazidiwa nguvu,akalipiga teke la ikulu,lijamaa likampiga ngumi yule dada likamng'oa jino moja.Bahati majirani tukawa tumefika baada ya kelele za kuomba msaada kutoka kwa yule dada,tulipofika lijamaa likatoka nduki,dada ameshachukua RB.Jamani wadada kuweni makini sana!