Hili la shule ya CCM kutaifishwa ni kipimo cha akili zetu za kutafakari mambo

Sasa wewe mtoa mada ile shule ina ardhi kubwa sana katikati ya mji ina majengo mazuri kama humuiya ya wazazi wangwamua kuanzisha mradi mwingine hapo unadhani wangeshindwa.kwa ufupi rais ni mzalendo over.
Kwani umesikia Bk kuna shida ya ardhi. Kama suala ni ardhi ilikuwaje ccm wakashindwa kuiendesha. Ebu elezea ufanisi wa hiyo shule hapo Bk. Shule iko mjini hata haisikiki utafikiri ni shule ya kata wakati inamiaka nenda rudi. Shule limewashinda kuendesha mnadai eti kuitaifisha. Kama ni kutaifisha basi atifishe zote za ccm.

Hivi ile ya Hedalu iliishiwa wapi vile?
 
Tunaweza shangilia kumbe hayo madai ambayo amesema ccm watalipwa yakawa makubwa afadhali ya kujenga shule mpya!
Kuna shule kibao za ccm mikoani watoto wanahangaika hazitaifishi!
Ataifishe na hizo!!!
 
JMP aliposema eti ametaifisha shule ya ccm (Omwani) na kuwa ya serikali watu wakashangilia na kudai eti ni mzalendo wa kweli.

Kwa ufupi tu ni kwamba kwa wanaoifahamu shule ya omwani hawawezi kushangilia hiki kitu.

Shule hii haikuwa productive kwa ccm na ilikuwa ni mzigo kwa ccm na ilikuwa inajiendesha kwa hasara. Ni shule ambayo ilikuwa inabeba makapi ya wanafunzi na wale wazazi walikuwa hawana huwezo wa kupeleka watoto katika shule zenye sifa nzuri yankufaukisha.

Pili hili jambo lilishajadilika kwenye vikao vya ccm namna ya kutua huo mzigo. Na ndio maana unaona serikali inabeba mzigo wote hadi wa waalimu wake ili kuiokoa ccm na mzigo wa madeni. Kwa kifupi huu ni ufisadi mwingine.

Swali la kujiuliza hivi ni kweli shule hii ingekuwa inafanya vizuri katika elimu na ikawa inajiendesha kwa faida JMP angeitaifisha. Jipu ni hapana. CCM wasingekubali kuiachia. Swali lingine dogo tu, Je ccm inashule ngapi na kwanini zisitaifishwe zote!

Watanzania wenzangu tusiwe wepesi wa kushangilia kila jambo bali tujaribu kujiuliza maswali juu ya nini kiko nyuma ya uamzi uliofikiwa.

Kwa hili la shule ya umwani ni sawa na kupewa gari lililojuu ya mawe ambalo mwenye nalo limemsha mshinda. Hapa tumepigwa changa macho.

Nawatakia Heri ya Mwaka Mpya.

umbea mtupu
 
Wewe ni mpuuzi
Sijui mnalipwa humu ndani
Kwa kuikosoa serikali mitandaoni?
Kila jambo kwenu ni baya
Acheni ushabiki wa kipumbavu huo
Tumuunge mkono mh Rais anapojaribu kuinyoshs nchi
Tusiangalie maslahi yetu binafsi
Tuangalie maslahi mapana ya nchi yetu
Kwahiyo watu washindie mitandaoni kuisifia tu serikali hata kama kuna maeneo serikali inakosea? Shule hii haimo kwenye orodha ya shule zinazofanya vizuri kitaaluma na sidhani kama ina walimu cwa kutosha. Nakumbuka miaka ya nyuma ilikuwa ina matokeo duni kabisa kwa kuongoza kitaifa kwa div 0
 
Rais Magufuli siyo mara yake ya kwanza kutaifisha shule za CCM na kuzifanya kuwa shule za serekali,siku za nyuma alishawahi kufanya hivyo kwa kuitaifisha shule ya sekondari Chato iliyokuwa mali ya CCM na kuifanya kuwa shule ya serekali.

Hata hivyo siyo kwamba Magufuli ana taifisha shule za CCM,CCM ndio waliotaifisha shule za wananchi na kuzifanya kuwa mali yao kwa kuwa shule hizo zilijengwa na wananchi wote bila kujali itikadi zao na hawakujua kama shule hizo zitakuja kuhodhiwa na CCM.

Alichokifanya Magufuli ni kuwarudishia wananchi mali yao iliyopolwa na CCM,na hiyo bado haitoshi,ana takiwa arudishe shule zote na viwanja vyote mikononi mwawananchi wote,ambavyo vilijengwa na nguvu za wananchi na kupolwa na CCM.
 
Mwanzo mzuri. Tuunge mkono.
Huenda viwanja vingi na Mali nyingi zilizo chamani ambazo kimsingi ni za watz zitarudi.
Labda mnisaidie hiki kiswahili... Kutaifisha. Hii imetaifishwa au? Maana tumeambiwa watalipwa.
Watalipwa nini? Aridhi? Majengo? Madeni ya waalim na wazabuni au vyote?.
Na ubora wa students ni wa kiwango cha serikali?
Walifaulu?. Sio vilaza.
Vinginevyo thanks Mr. President. Good move.
 
Mleta mada upo sahihi kabisa.
Mpaka sasa bado hatujajua Mantiki, Sheria, Kanuni, Utaratibu, Faida au Hasara za kuitafisha shule hiyo.
Litakuwa ni jambo la ajabu sana kushangilia kitu tusichokijua.
Kwanini Shule hiyo tu?
Mantiki ya hatua hii ni kwamba fedha za serikali na wahisani wengine zilitumika kukarabati shule hii ya taasisi ya CCM. Kuiacha endelee kuwa ya CCM tafsiri yake sahihi ingekuwa serikali na wadau wametoa mtaji wa kibiashara kwa taasisi ya CCML Pia itakumbukwa wakati ina karabatiwa kulikuwa na uzi humu JF ukihoji kwa nini fedha za umma zitumike kukarabati taasisi ya CCM. Kwa hiyo ni uamuzi wa Raisi kuitaifisha kutanufaisha wanafunzi wengi wa kidato cha 1hadi 4 kwa upande wa ada ambayo haikuwa bure Kama itakayokuwa aasa
 
Mleta mada upo sahihi kabisa.
Mpaka sasa bado hatujajua Mantiki, Sheria, Kanuni, Utaratibu, Faida au Hasara za kuitafisha shule hiyo.
Litakuwa ni jambo la ajabu sana kushangilia kitu tusichokijua.
Kwanini Shule hiyo tu?
Tutakumbuka pia baada ya tetemeko kamati ya maafa ilianza kujenga upya shule hii.
Hili jambo liliwashangaza wengi na kuuliza kulikoni serikali kuisaidia shule ya Ccm. Hivyo Mh. Ameamua aidha kimtego au kinamna fulani kufikia maamuzi hayo ili kuwaziba midomo wafuatiliaji wa mambo. Hii ni Tanzania bhana
 
Hatutaki heri yako ya mwaka mpya.....najua roho zinawauma sana jinsi JPM anavyopiga kazi..na baaaado

Viva Magufuli
Mimi nina swali.
Je shule hii imeadhirika na tetemeko?
Kama jibu ni ndiyo basi kwa maoni yangu wametaifisha ili serikali ikijenga watu wasilalamike mbona wanajenga miundombinu ya shule binafsi za ccm?
 
Wewe ni mpuuzi
Sijui mnalipwa humu ndani
Kwa kuikosoa serikali mitandaoni?
Kila jambo kwenu ni baya
Acheni ushabiki wa kipumbavu huo
Tumuunge mkono mh Rais anapojaribu kuinyoshs nchi
Tusiangalie maslahi yetu binafsi
Tuangalie maslahi mapana ya nchi yetu
ni vigumu kunyosha kitu wkt we mwnyewe umepinda
 
Kwahiyo watu washindie mitandaoni kuisifia tu serikali hata kama kuna maeneo serikali inakosea? Shule hii haimo kwenye orodha ya shule zinazofanya vizuri kitaaluma na sidhani kama ina walimu cwa kutosha. Nakumbuka miaka ya nyuma ilikuwa ina matokeo duni kabisa kwa kuongoza kitaifa kwa div 0
Kama ndivyo
Si ndio maana serikali imechukua kuongeza ufanisi
 
Back
Top Bottom