- Thread starter
- #21
Mnafiki! huwezi kumtenganisha JK na Lowassa hata kidogo, kukubali kuwa wewe ni CCM na kuwagawa hawa wasafi na hawa wachafu...hutafiki mbali
hakuna msafi CCM si wewe si bosi wako Membe na mjomba wako Kikwete!
Aibu!!!
Hizo blanket accusations zako dhidi ya JK bila kuwa na hoja ambazo mimi na watu wa aina yangu zitatubaidilisha msimamo au mtazamo wetu hazikupi heshima na kinyume chake unaonekana ni mtu ambaye anaendeshwa zaidi na chuki . Kila siku tumekuwa tuki-demand tuambiwe uchafu wa JK au hata huyo Membe lakini stori zinazokuja hapa ni kwamba wanajipanga kwa 2015. Wewe ambaye unasema Lowassa na Kikwete ni one and the same ndiye mwenye onus ya kuthibitisha hilo maana matendo ya Lowassa yanafahamika kwa ushahidi na hatujafika hatua ya kumuona hivyo kwa hisia au kwa kukurupuka.
Mimi nimekuambia kwamba sijawahi kuwa CCM wala chama chochote cha siasa and I am happy this way. Lakini siwezi kuingia kwenye fashion ya kudhani kuitukana CCM pasipostahili na kuisifia CDM pasipostahili ni uzalendo. Upumbavu uitwe hivyo unapostahili na hivyo hivyo ustaarabu. Kwa vile wewe unawiwa na allegiance ya chama chako, ndio maana kila wakati unajikuta ni mateka wa kushabikia kila linalofanywa na chama chako na hivyo hivyo kuponda kila linalofanywa na chama pinzani na chako. Grow up man!