Hili la Loliondo tulifikiria au tulikurupuka!

kibajaj

Senior Member
Apr 12, 2011
106
26
Ni miezi kadhaa sasa tangu jina la Loliondo lilipojipatia umaarufu mkubwa Afrika ya mashariki.Kwa kadiri ninavyoelewa mimi,uganga wa kienyeji ni kitu cha kurithi katika ukoo. Japo babu,baba na wewe hamkuwa waganga lakini kama kuna uganga kwenye ukoo unaweza ukawaruka wote hao ukaja tokea kwa mjukuu wako bila kujali nafasi yake katika dini,elimu na jamii kwa ujumla.
Endapo mizimu hii ya uganga itamtaka awe mganga wakati yeye tayari ni padre,mchungaji shehe ua imamu na akaanza kutenda miujiza nani anaweza kuwashawishi watu kuwa miujiza ile haitoki kwa mungu wakati muhusika yuko katika nafasi fulani ya dini? au kuanza kufuatilia background ya mtu huyu kwa kinaga ubaga?Au watu wanakurupuka tu na kufanya mambo kwa ushabiki bila kujua mafanikio au madhara ya kufanya hivyo?
Kwa wale wenzangu na mimi niwaulize chloroquine iliyokuwa dawa maarufu ya malaria ilitumika kwa miaka mingapi na baadaye kuja kugundulika kuwa ina madhara kwenye mwili wa binadamu? Kwa nini serikali ikurupuke na kuanza kusema dawa imepimwa na TFDA haina tatizo hivi badae ikagundulika ina tatizo serikali itaficha wapi uso wake?
Sawa ni suala la imani lakini tusikurupuke.
 
Sijajua kama kuna nini ambacho unataka kuilaumu serikali. hebu fanya utafiti ili uongee vitu ambavyo ukuleata tutakuelewa, unajua ugonjwa wa sukari umeuwa watu wangapi hadi sasa kwa kupitia dawa za kitaalam? je UKIMWI? je kansa? na mengine mengi, unajua madhara ya dawa za kitaalamu? au we unakunywa na kulala tu, unataka nani aje atuthibitishie usalama wa dawa ya Babu kama soyo wataalamu tulionao? huu ni ushamba; acheni babu aponye magonjwa sugu, kama una hospitali au mladi uliyotegemea kuwavuna wa tz masikini kwa dawa zisizoponyesha shauri yako hapo imekula kwako. Krolokwini unayosema iligundulika eti inasumu, we ni muongo mkubwa, utafiti unasema iligundulika kuishiwa nguvu za kuua wadudu wa maralia. Nadhani kunahaja ukanywe dawa LOLIONDO itasaidia uwena maamuzi sahihi.
 
Kwani wakati wamegundua Krolokwini inamadhara selikali ilificha wapi uso wake????
Mbona na wewe naona unakurupuka the same way ...
 
Dawa za kutibu malaria za siku hizi ni miradi ya watu fulani waliopo juu. Kupiga stop Chloroquine ilikuwa ni njama ili waweze kuingiza dawa zao. Cha kushangaza ni kuwa kuna watu (Kenya) walikuwa wanaendelea kutumia chloroquine wakati TZ tumeipiga marufuku, swali la kujiuliza ni "Je, Malaria ya Kenya inatofautiana na ya Tanzania?".

Kuhusiana na babu kuwa na uhusiano na mambo ya waganga wa kienyeji, jaribu kufikiri na kufuata watu wanaotoa ushuhuda juu ya tiba hiyo. Gonga hapa ili upate kujijuza zaidi.
 
Tulikurupuka. Na mchezo huu wa kukurupuka iko siku nji hii itaripuka!

Angalia kama wa mwanzo walikurupuka usije ukakurupuka na wewe. Angalia jinsi dawa za kisayansi zilizoaminiwa zilivyokuja kuthibitishwa baadae kwamba hazifanyi kazi na baadae au baadhi ya nchi wakasema zinafanya kazi na wanaendelea kuzitumia...... Chroroqune,DDT....nk. Time will tell...
 
kwa kweli hili suala lina utata wake...hasa ukisikia kuwa kuna watu ambao wameshapata madhara....lakini tuache imani iitwe imani:lol:
 
Angalia kama wa mwanzo walikurupuka usije ukakurupuka na wewe. Angalia jinsi dawa za kisayansi zilizoaminiwa zilivyokuja kuthibitishwa baadae kwamba hazifanyi kazi na baadae au baadhi ya nchi wakasema zinafanya kazi na wanaendelea kuzitumia...... Chroroqune,DDT....nk. Time will tell...
Time will tell for sure. Kama hujasoma kitabu cha "Things Fall Apart" (Chinua Achebe), nakuomba ufanye hivyo kabla hayajakukuta yaliyomkuta Obi Okonkwo wa Umuahia!
 
Kuna mwanasayansi mmoja mkubwa alisema maneno haya:
"Science without religion is lame, religion without science is blind."
 
Mambo ya babu yaacheni hivi hivi, kila mtu ana imani yake. Mimi simwamini hata kwa mtutu wa bunduki, I will choose death. Ila wengine wenye imani yao ebu tuwape nafasi wewe usiyeamini kimyaaaaaaaa!! watu wakali kweli ukianza kumcrush babu.

Blessing to you all! have a wonderfu saturday
 
Hapa tulikurupuka!
Sisemi eti sizipendi dawa asili la hasha!. Isipokuwa tumejikuta hata serikali nayo ikipoteza uelekeo baada ya kufanya utafiti tukajikuta nao wanamfanyia matangazo ya biashara babu. Mimi napatwa na butwaa kuamini magonjwa ambayo babu anatibu and "if it cannot be proved scientifically, then leave it". Nani mwenye magonjwa sugu kapona kwa imani, watu wetu wanaibiwa pesa, hili la babu angekuwa ni sheikh Yahya, tungeambiwa moja kwa moja kuwa ni nguvu za giza. Watanzania tumepoteza mwelekeo, si amini hata kidogo kuwa ugunduzi wa dawa dhidi ya magonjwa 5 hayo sugu utapatikana africa, sina hakika hata kidogo. Lakini, tuzipe nafasi dawa zetu za asili kwa kuwa hii ndiyo asili yetu waafrica na ni utamaduni wetu.
 
Ni miezi kadhaa sasa tangu jina la Loliondo lilipojipatia umaarufu mkubwa Afrika ya mashariki.Kwa kadiri ninavyoelewa mimi,uganga wa kienyeji ni kitu cha kurithi katika ukoo. Japo babu,baba na wewe hamkuwa waganga lakini kama kuna uganga kwenye ukoo unaweza ukawaruka wote hao ukaja tokea kwa mjukuu wako bila kujali nafasi yake katika dini,elimu na jamii kwa ujumla.
Endapo mizimu hii ya uganga itamtaka awe mganga wakati yeye tayari ni padre,mchungaji shehe ua imamu na akaanza kutenda miujiza nani anaweza kuwashawishi watu kuwa miujiza ile haitoki kwa mungu wakati muhusika yuko katika nafasi fulani ya dini? au kuanza kufuatilia background ya mtu huyu kwa kinaga ubaga?Au watu wanakurupuka tu na kufanya mambo kwa ushabiki bila kujua mafanikio au madhara ya kufanya hivyo?
Kwa wale wenzangu na mimi niwaulize chloroquine iliyokuwa dawa maarufu ya malaria ilitumika kwa miaka mingapi na baadaye kuja kugundulika kuwa ina madhara kwenye mwili wa binadamu? Kwa nini serikali ikurupuke na kuanza kusema dawa imepimwa na TFDA haina tatizo hivi badae ikagundulika ina tatizo serikali itaficha wapi uso wake?
Sawa ni suala la imani lakini tusikurupuke.

Ni kweli k,hata leo PM ameligusia hilo tena Kawaasa kwelikweli kwa nguvu zake zote wale wote wanao kurupukia aina hiyo ya TIBA
 
Ni kweli k,hata leo PM ameligusia hilo tena Kawaasa kwelikweli kwa nguvu zake zote wale wote wanao kurupukia aina hiyo ya TIBA

Hivi maposema kukurupukia hiyo tiba mna maana gani hasa? Mna maana mpaka taarifa ipelekwe WHO na tuelezwe kuwa tuanze matibabu au?

Au ina maana hamfahamu kuwa miti shamba nazo ni dawa? Hivi mtu akikuambia twanga tangawizi ,kamua maji yake kisha changanya na kijiko kimoja cha asali mbichi halafu kunywa utapona kikohozi , huyu naye ni mgamga wa kienyeji? Mganga wa kienyeji ni yupi hasa, maana hata Hospitali tunashauriwa kula mchicha ili kuongeza damu.

Katika Biblia Yesu alikoroga tope akampaka kipofu na akapata kuona. Hii nayo ni tiba ipi?
 
Dawa za kutibu malaria za siku hizi ni miradi ya watu fulani waliopo juu. Kupiga stop Chloroquine ilikuwa ni njama ili waweze kuingiza dawa zao. Cha kushangaza ni kuwa kuna watu (Kenya) walikuwa wanaendelea kutumia chloroquine wakati TZ tumeipiga marufuku, swali la kujiuliza ni "Je, Malaria ya Kenya inatofautiana na ya Tanzania?".

Kuhusiana na babu kuwa na uhusiano na mambo ya waganga wa kienyeji, jaribu kufikiri na kufuata watu wanaotoa ushuhuda juu ya tiba hiyo. Gonga hapa ili upate kujijuza zaidi.

By the way Uganda bado kuna baadhi ya watu wanatumia Kloroquini......
 
Back
Top Bottom