Ni miezi kadhaa sasa tangu jina la Loliondo lilipojipatia umaarufu mkubwa Afrika ya mashariki.Kwa kadiri ninavyoelewa mimi,uganga wa kienyeji ni kitu cha kurithi katika ukoo. Japo babu,baba na wewe hamkuwa waganga lakini kama kuna uganga kwenye ukoo unaweza ukawaruka wote hao ukaja tokea kwa mjukuu wako bila kujali nafasi yake katika dini,elimu na jamii kwa ujumla.
Endapo mizimu hii ya uganga itamtaka awe mganga wakati yeye tayari ni padre,mchungaji shehe ua imamu na akaanza kutenda miujiza nani anaweza kuwashawishi watu kuwa miujiza ile haitoki kwa mungu wakati muhusika yuko katika nafasi fulani ya dini? au kuanza kufuatilia background ya mtu huyu kwa kinaga ubaga?Au watu wanakurupuka tu na kufanya mambo kwa ushabiki bila kujua mafanikio au madhara ya kufanya hivyo?
Kwa wale wenzangu na mimi niwaulize chloroquine iliyokuwa dawa maarufu ya malaria ilitumika kwa miaka mingapi na baadaye kuja kugundulika kuwa ina madhara kwenye mwili wa binadamu? Kwa nini serikali ikurupuke na kuanza kusema dawa imepimwa na TFDA haina tatizo hivi badae ikagundulika ina tatizo serikali itaficha wapi uso wake?
Sawa ni suala la imani lakini tusikurupuke.
Endapo mizimu hii ya uganga itamtaka awe mganga wakati yeye tayari ni padre,mchungaji shehe ua imamu na akaanza kutenda miujiza nani anaweza kuwashawishi watu kuwa miujiza ile haitoki kwa mungu wakati muhusika yuko katika nafasi fulani ya dini? au kuanza kufuatilia background ya mtu huyu kwa kinaga ubaga?Au watu wanakurupuka tu na kufanya mambo kwa ushabiki bila kujua mafanikio au madhara ya kufanya hivyo?
Kwa wale wenzangu na mimi niwaulize chloroquine iliyokuwa dawa maarufu ya malaria ilitumika kwa miaka mingapi na baadaye kuja kugundulika kuwa ina madhara kwenye mwili wa binadamu? Kwa nini serikali ikurupuke na kuanza kusema dawa imepimwa na TFDA haina tatizo hivi badae ikagundulika ina tatizo serikali itaficha wapi uso wake?
Sawa ni suala la imani lakini tusikurupuke.