Hili la Loliondo tulifikiria au tulikurupuka!

Nina mwezi sasa toka nimesimama kunywa dawa za kisukari sukari yangu iko chini,utanidanganya nini.hebu soma madhara ya dawa za kurefusha maisha wanzo kunywa watu walioathilika na UKIMWI hasa kwenye ini.
 
mkuu naona umepotoka
maana siamini kama watu wote waliokunywa kikombe kwa babu wamepona
nataka mtu atakaye thibitisha baada ya kupimwa kabisa

kuhakiki ni lazima

so selikali ya tanzania naona imekurupuka.




sijajua kama kuna nini ambacho unataka kuilaumu serikali. Hebu fanya utafiti ili uongee vitu ambavyo ukuleata tutakuelewa, unajua ugonjwa wa sukari umeuwa watu wangapi hadi sasa kwa kupitia dawa za kitaalam? Je ukimwi? Je kansa? Na mengine mengi, unajua madhara ya dawa za kitaalamu? Au we unakunywa na kulala tu, unataka nani aje atuthibitishie usalama wa dawa ya babu kama soyo wataalamu tulionao? Huu ni ushamba; acheni babu aponye magonjwa sugu, kama una hospitali au mladi uliyotegemea kuwavuna wa tz masikini kwa dawa zisizoponyesha shauri yako hapo imekula kwako. Krolokwini unayosema iligundulika eti inasumu, we ni muongo mkubwa, utafiti unasema iligundulika kuishiwa nguvu za kuua wadudu wa maralia. Nadhani kunahaja ukanywe dawa loliondo itasaidia uwena maamuzi sahihi.
 
Ni miezi kadhaa sasa tangu jina la Loliondo lilipojipatia umaarufu mkubwa Afrika ya mashariki.Kwa kadiri ninavyoelewa mimi,uganga wa kienyeji ni kitu cha kurithi katika ukoo. Japo babu,baba na wewe hamkuwa waganga lakini kama kuna uganga kwenye ukoo unaweza ukawaruka wote hao ukaja tokea kwa mjukuu wako bila kujali nafasi yake katika dini,elimu na jamii kwa ujumla.
Endapo mizimu hii ya uganga itamtaka awe mganga wakati yeye tayari ni padre,mchungaji shehe ua imamu na akaanza kutenda miujiza nani anaweza kuwashawishi watu kuwa miujiza ile haitoki kwa mungu wakati muhusika yuko katika nafasi fulani ya dini? au kuanza kufuatilia background ya mtu huyu kwa kinaga ubaga?Au watu wanakurupuka tu na kufanya mambo kwa ushabiki bila kujua mafanikio au madhara ya kufanya hivyo?
Kwa wale wenzangu na mimi niwaulize chloroquine iliyokuwa dawa maarufu ya malaria ilitumika kwa miaka mingapi na baadaye kuja kugundulika kuwa ina madhara kwenye mwili wa binadamu? Kwa nini serikali ikurupuke na kuanza kusema dawa imepimwa na TFDA haina tatizo hivi badae ikagundulika ina tatizo serikali itaficha wapi uso wake?
Sawa ni suala la imani lakini tusikurupuke.

Napenda kukusahihisha kuwa chloroquine haikuwa na madhara ila ilipigwa marufuku 1. Ilikuwa imezoeleka sana mwilini hivyo watu wengi walianza kutopona kwa kutumia dawa hiyo. 2. Kina dada walikuwa wanaitumia vibaya, ndiyo ilikuwa inatumika sana kutoa mimba
 
Mambo ya babu yaacheni hivi hivi, kila mtu ana imani yake. Mimi simwamini hata kwa mtutu wa bunduki, I will choose death. Ila wengine wenye imani yao ebu tuwape nafasi wewe usiyeamini kimyaaaaaaaa!! watu wakali kweli ukianza kumcrush babu.

Blessing to you all! have a wonderfu saturday

Ahsante sana CD. Hii Serikali ya kisanii inasikitisha sana kusema kweli. Na kama ulivyosema kuna watu wanakuwa wakali mno! pale unapoanza kuhoji kikombe cha Babu. Mpaka sasa hivi hakuna uthibitisho wowote wa kitaalamu unaoonyesha kwamba watu wamepona ukimwi, kisukari, saratani n.k.
 
kamimbi acha kutetea ushirikina, babu ni Mganga kama walivyo wagnaga wengine na toa hoja acha kuongea upupu kwa ushabiki
 
Hi waganga wa kienyeji wale wanaojiita maprofesa na madokta hasa kule jangwani (dar) wana leseni ya kufanya hizo shughuli? Ni lini serikali ilithibitisha wanauwezo wakutibu magonjwa sugu kama inavyoonekana kwenye matangazo yao?

Wakuu, uiko hivi, mnaompiga vita babu:
1. Hamuugui kisukari, cancer, ukimwi wala hamna ndugu wanaosumbuliwa na magonjwa hayo au,
2. Mko kwenye ileeee miradi ya ukimwi ... watu wakipata tiba si miradi itakufa? au,
3. Mnamiliki makanisha kama yale ya kina nabii ambayo ustawi wake unategemea sana waumini wenye matatizo.

Ushauri wangu, kabla hamjaanza vita dhidi ya babu, anzisheni ya wangango wa kienyeji wale wapiga ramli kwanza.
 
Ukweli ni kwamba serikali ilikurupuka, wala haiwezi kukwepa lawama kwa hili. Serikali inapaswa kufanya mambo yote kwa umakini na kuwa na uhakika ya kile inachokifanya. Hakuna utafiti wowote wa kitaalamu uliofanywa kuthibitishwa huo unaoitwa uponyaji, halafu serikali inakimbilia kujenga miundo mbinu ikitumia kodi za watu. Serikali gani hii inafanya maamuzi kwa maneno ya kusikia yasiyo na uthibitisho?
 
Hivi maposema kukurupukia hiyo tiba mna maana gani hasa? Mna maana mpaka taarifa ipelekwe WHO na tuelezwe kuwa tuanze matibabu au?

Au ina maana hamfahamu kuwa miti shamba nazo ni dawa? Hivi mtu akikuambia twanga tangawizi ,kamua maji yake kisha changanya na kijiko kimoja cha asali mbichi halafu kunywa utapona kikohozi , huyu naye ni mgamga wa kienyeji? Mganga wa kienyeji ni yupi hasa, maana hata Hospitali tunashauriwa kula mchicha ili kuongeza damu.Katika Biblia Yesu alikoroga tope akampaka kipofu na akapata kuona. Hii nayo ni tiba ipi?


Mkuu well said,
Unajua waafrika ni wajinga sana. Tiba hii ingetolewa na Sheikh wa Kiarabu, au Mzungu wa Roma wangeiita inatoka kwa Mungu. Lakini kwa kuwa ni ya mtu mweusi watamponda hadi basi. Ndo laana hiyo, tumekuwa watumwa wa Ukristo na Uislamu, vyote ambavyo ni tamaduni tu za wenzetu na hakuna u Mungu wowote kwenye hizo dini. Ila kwa kuwa ni za watu weupe, ah ! Tunajidharau halafu tunalaumu wazungu kwamba wanatudharau. Aibu sana!
 
Mkuu well said,
Unajua waafrika ni wajinga sana. Tiba hii ingetolewa na Sheikh wa Kiarabu, au Mzungu wa Roma wangeiita inatoka kwa Mungu. Lakini kwa kuwa ni ya mtu mweusi watamponda hadi basi. Ndo laana hiyo, tumekuwa watumwa wa Ukristo na Uislamu, vyote ambavyo ni tamaduni tu za wenzetu na hakuna u Mungu wowote kwenye hizo dini. Ila kwa kuwa ni za watu weupe, ah ! Tunajidharau halafu tunalaumu wazungu kwamba wanatudharau. Aibu sana!

Hapa sio suala la kujidharau. Wapo watumishi wa Mungu wengi tu watanzania wanaotumiwa na Mungu na tunawaheshimu sana. Tatizo hapa ni serikali kujiingiza kwenye jambo ambalo halina uthibitisho wowote. Kama kweli watu wanapona serikali ilipaswa kwanza ithibitishe hivyo kitaalamu. Watu wanasema wamepona, halafu baada ya siku kadhaa hali yao inakuwa mbaya kuliko ile ya mwanzo, uponyaji gani huo?
 
Unajua waafrika ni wajinga sana...
Huyu naye anaitwa Nyumbu

blue-wildebeest-07.jpg
Wildebeest (Connochaetes taurinus) Swahili: Nyumbu

Wildebeest or Gnu are to the African Savannah what the bison once were to the North American prairies. Numbering in their millions in certain areas,particularly Masai Mara and over the border in Serengeti, they are unmistakable for their prehistoric appearance.

Wildebeest are also known as blue wildebeest or brindled Gnu.They are well known for their excentric behaviour which includes loud snorting, tossing and shaking of the head, bucking, running around in circles and rolling in the dust, thought to be a reaction to the activity of the botfly larva which manage to find their way up into their nostrils.
 
Mwenye shida haralamiki ni kujaribu
Wewe hujapata shida na ndio unaandika yote haya

Omba Mubgu yasikukute

Uko Sahihi Mkuu, huyu ndugu hayajamkuta yeye au jamaa yake wa karibu. Ikiwa kuna mtu wa karibu yako ana tatizo ambalo mnasumbuka kutafuta suluhu yake, unaweza kujaribu kila kitu. Kwa hiyo si vyema kuwalaumu waliyochukua uwamuzi wa kwenda kwa Babu.
 
Kama unaumwa kopo nauli popote kimbia sana nenda kwa babu, kama u mzima mshukuru Mungu ila usifurahie msiba wa mwenzio bali liya na wanaolia pia furahi na wanaofurahi.
 
Acha waliokunywa watupe ushuhuda.
Umuhimu ni kwamba kama mtu alikuwa na maumivu makali na amepungua basi dawa imesaidia.
Dawa hii si ya kurefusha maisha bali ni ya kutibu lakini haiwezi kumwongezea mtu hata siku moja ya kuishi.
Adamu na Eva walitupwa nje ya bustani ya edeni na malaika mwenye upanga akapewa kazi ya kulinda wasirudi tena. Maana walikula matunda ya mti wa kutambua mema na mabaya sasa ilikuwa imebakia wale matunda ya mti wa uzima, ambayo ingewafanya wasione mauti!!!!
Mchungaji yeye anotoa dawa kwa wagonjwa wanomwa na sio kwa wanao tafuta kinga. Mtu anapokuwa anaumwa anahangaika huku na kule kutafuta sehemu ambapo atapata nafuu. Ndiyo maana mtu anakwenda Muhimbili, anatoka hapo anakwenda Regency/Aga Khan, Tumaini, Mikocheni, etc. ili mradi tu apate dawa ya kumpunguzia maumivu au kupona kabisa.
 
Nawashangaa sana. Serikali ingekurupuka bila kuwa na ushahidi? Wamepona wao wenyewe ndio maana wameshabikia, maana walikuwa wa kwanza kwenda. Kabla hayajakupata huwezi kuelewa dunia ya kuwa mgonjwa ikoje. Nyie wazima kaeni kimya mumshukuru Mungu amewajaalia uzima hata kama babu ni sangoma, wangapi wanakwenda kwa waganga kuna vibao kila pahali na hampigi kelele? Shida ni kuwa anajaza umati wa watu? Dawa za waganga wengine na waaguzi zimepimwa na nani??? Babu zenu walitumia dawa gani kabla mzungu hajaja kuwaambia mziache ni ushenzi??? Nawashangaa sana.
 
Watanzania wengi tu vipofu, mpaka tufunguke macho sumu itakuwa tayari inafanya kazi vizuri mwilini. Zinduka we mtanzania.
 
Hi waganga wa kienyeji wale wanaojiita maprofesa na madokta hasa kule jangwani (dar) wana leseni ya kufanya hizo shughuli? Ni lini serikali ilithibitisha wanauwezo wakutibu magonjwa sugu kama inavyoonekana kwenye matangazo yao?

Wakuu, uiko hivi, mnaompiga vita babu:
1. Hamuugui kisukari, cancer, ukimwi wala hamna ndugu wanaosumbuliwa na magonjwa hayo au,
2. Mko kwenye ileeee miradi ya ukimwi ... watu wakipata tiba si miradi itakufa? au,
3. Mnamiliki makanisha kama yale ya kina nabii ambayo ustawi wake unategemea sana waumini wenye matatizo.

Ushauri wangu, kabla hamjaanza vita dhidi ya babu, anzisheni ya wangango wa kienyeji wale wapiga ramli kwanza.

Hapo kwenye RED, iradi sasa ndio itapambana moto, maana tunajipanga kufanya community sensitization, impact evaluation na kedevelop mitigation plans!!! so ni ulaji kwa kwenda mbele teh teh teh LOL.......BUT ON A SERIOUS NOTE,
hiyo namba moja ndio chanzo cha hii hullabaloo ya kukimbilia kwa Babu, magonjwa sugu huambatana na depression na kukata tamaa,matokeo yake ni kukumbatia chochote utakachoelezwa kuwa kitakurejeshea afya njema. Bahati mabaya sana, tuna wataalamu wachache sana wa afya ya akili na mara nyingi magonjwa ya akili yanayoambata na magonjwa mengine kama UKIMWI, Cancer nk yashindwa kupewa attention inyostahili. Tukumbuke kwamba, the fact kwamba BABU ameattach KIKOMBE chake cha maji ya mugariga (sitaki tuiite dawa kwani haiqualify kuitwa hivyo) na nguvu za kimiujiza , yaani supernatural powers hii peke yake ina impact kubwa sana kwenye saikolojia ya mgonjwa. Tayari Mgonjwa nakuwa ametua mzigo mmoja DEPRESSION na anaijaza nafsi yake na matumaini ya kupona, na ndio wengi tunaowasikia wakirudi na kusema wanajisikia vizuri. ...sitaki kuelezea kuhusu kupona na kutokupona. Wengi wanaumia sana kwasababu ni kuwanvunja matumaini mapya waliyorudi nayo kutoka kwa babu, fikiria umeenda hospitali daktari akakwambia kuwa ''mama tatizo lako la kutokupata ujauzito kwa miaka sita sasa limepona'' halafu unakutana na shoga yako unamwambia hayo maneno anaangua kicheko kikubwa na kukwambia, ''utamaliza waganga wote mtoto utamsikia kwenye bomba''.......tafakari.
 
Back
Top Bottom