Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 17,026
- 20,511
Ikulu ni taasisi pana, yenye bendera na miiko yake, inakiongozi wake na watendakazi wake pia.
Mnadhimu mkuu wa Ikulu ambaye hutambuliwa kwa lugha ya mafumbo (shafron) kama AT2 ndiye kiongozi wa ikulu, Itifaki ya kirais ipo chini ya AT2 hata rais yupo chini yake. (kinadharia)
Katibu mkuu kiongozi ni sehemu ya wanaounda taasisi ya urais ndani ya Ikuli ambapo kwa sasa ni Bwana Sefue,
Pia yupo mkuu wa walinzi wote wa rais ambae kwasasa yupo kamanda Ben Mashaba,
Na pia yupo katibu muhitasi wa rais ama twaita mnikulu, ambapo kwa sasa yupo Bwana Gurumo.
Sasa kwa siku za karibuni kumeibuka kuvuja siri mhimu za rais (ikulu), jambo linalotia shaka sana ustahimilivu wa watumishi wetu hawa,
Kwanza ilianza kuvuja kwa "siri" za vikao vya siri vya Mheshiwa rais na wakala Zitto Kabwe,
Hili kwangu lilinipa hofu kubwa, kwamba kumbe unaweza kupeleka siri za nchi kwa rais na zikavuja kienyeji hivi??? Sasa sie wambeya tutapeleka wapi ili tuwe salama???
Lakini hilo likiwa halijapoa, wiki jana magazeti yameripoti mtumishi wa Hospitali ya KCMC amefukuzwa kazi kwakumpenyezea Rais taarifa nyeti zinazojiri hospitalini hapo,
Hakiki nimefadhaika sana sana, taasisi ya urais inawezaje kuvujisha taarifa za mawakala mhimu wa nchi ambao wanaripoti mojakwamoja kwa rais?? Je amevujisha rais mwenyewe au ni hawa watunza siri za urais?
Najihisi ni mkiwa ndani ya nchi yangu yenye mamlaka ya urais inayohatarisha maisha ya mawakala wake.
Vetting inazingatiwa vema kuwapata hawa watumishi wa rais?
Hali hii inanitisha na sitaki kuamini kabisa!!
Mnadhimu mkuu wa Ikulu ambaye hutambuliwa kwa lugha ya mafumbo (shafron) kama AT2 ndiye kiongozi wa ikulu, Itifaki ya kirais ipo chini ya AT2 hata rais yupo chini yake. (kinadharia)
Katibu mkuu kiongozi ni sehemu ya wanaounda taasisi ya urais ndani ya Ikuli ambapo kwa sasa ni Bwana Sefue,
Pia yupo mkuu wa walinzi wote wa rais ambae kwasasa yupo kamanda Ben Mashaba,
Na pia yupo katibu muhitasi wa rais ama twaita mnikulu, ambapo kwa sasa yupo Bwana Gurumo.
Sasa kwa siku za karibuni kumeibuka kuvuja siri mhimu za rais (ikulu), jambo linalotia shaka sana ustahimilivu wa watumishi wetu hawa,
Kwanza ilianza kuvuja kwa "siri" za vikao vya siri vya Mheshiwa rais na wakala Zitto Kabwe,
Hili kwangu lilinipa hofu kubwa, kwamba kumbe unaweza kupeleka siri za nchi kwa rais na zikavuja kienyeji hivi??? Sasa sie wambeya tutapeleka wapi ili tuwe salama???
Lakini hilo likiwa halijapoa, wiki jana magazeti yameripoti mtumishi wa Hospitali ya KCMC amefukuzwa kazi kwakumpenyezea Rais taarifa nyeti zinazojiri hospitalini hapo,
Hakiki nimefadhaika sana sana, taasisi ya urais inawezaje kuvujisha taarifa za mawakala mhimu wa nchi ambao wanaripoti mojakwamoja kwa rais?? Je amevujisha rais mwenyewe au ni hawa watunza siri za urais?
Najihisi ni mkiwa ndani ya nchi yangu yenye mamlaka ya urais inayohatarisha maisha ya mawakala wake.
Vetting inazingatiwa vema kuwapata hawa watumishi wa rais?
Hali hii inanitisha na sitaki kuamini kabisa!!