Hili hapana, Hayati Magufuli anasingiziwa

Hili hapana, Hayati Magufuli anasingiziwa

thetallest

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2017
Posts
8,271
Reaction score
9,116
Baada ya hayati Magufuli kufariki maadui zake kazi ikabaki moja tu kuwekeza kwenye propaganda chafu dhidi yake, ili kumuondoa Magufuli mioyoni mwa watanzania wengi walioumuelewa na kuipenda kazi yake.

Waliwekeza mitandaoni kwa kuajiri vijana wa kumponda, threads nyingi ziliandikwa kwa pupa bila umakini.

Walichokosea ni kutoajiri watu makini wa kuchambua hoja zilizoshiba kutofautiana na mtazamo wa Rais Magufuli ili mbivu na mbichi zijitenge.

Matokeo yake wakaajiri wahuni ,wakiwemo na wahanga wa vyeti fake, kazi yao ikawa ni matusi kutwa kucha, matokeo yake wamepuuzwa vibaya sana na pumzi zimekata ghafla

Ukweli ni kwamba, mpaka sasa Magufuli anashaini mioyoni mwa watanzania wengi na anaendelea kuwa prove wrong watesi wake.

Leo mama Samia imebidi ataje jina la Magufuli alipokuwa akiifungua barabara ya Mbezi Louis, anajua bila Magufuli ushawishi unazidi kupungua.

Mungu mjalie Rais Samia angalau afikie hata nusu ya speed ya hayati Magufuli mambo yatakwenda
 
Baada ya hayati Magufuli kufariki maadui zake kazi ikabaki moja tu kuwekeza kwenye propaganda chafu dhidi yake, ili kumuondoa Magufuli mioyoni mwa watanzania wengi walioumuelewa na kuipenda kazi yake...
Samia, kiutendaji amemwacha mbali sana Magufuli. Magufuli alikuwa na speed kubwa katika propaganda, na siyo katila utendaji. Mimi siyo shabiki wa Samia, lakini ukimlinganisha Samia na Magufuli, Samia pamoja na mapungufu yake, atakuwa malaika

Kitu gani Magufuli ilisema kitakamilika wakati fulani halafu kikamilika wakati uliotajwa?

Speed kubwa ya Magufuli ilikuwa katika kudidimiza uhuru wa watu, demokrasia, haki za watu, kukanyaga sheria na katiba, na kudidimiza uchumi.

Wakati wa Kikwete uchumi ulikuwa unakua kwa 7%, Magufuli aliuporomosha mpaka 1.9% (taarifa ya WB), uwekezaji mwaka 2015 ulikuwa unakua kwa 28%, Magufuli aliuangusha mpaka 4%. Utalii mwaka 2015 ulikuwa unakua kwa 15%, mpaka 2019, Magufuli alikuwa ameuangusha mpaka 3.6%. Kwa takwimu hizi, Magufuli alikuwa anaenda spidi kali katika kuangamiza Taifa.

Kitu pekee alichofanikiwa Magufuli kuliko watangulizi waje ni siasa za ulaghai. Na wajinga aliwapata sana, hata wengine kufikiria kuwa alikuwa anafanya mambo makubwa sana kuliko watangulizi wake. Kwa kweli wajinga aliwaokota hasa, lakini wenye akili wanajua kuwa Magufuli alikuwa janga kwa Taifa. Hakuistahili ile nafasi.

Jbo jingine, ni kwamba marehemu Magufuli anasemwa sana sasa kwa sababu moja kubwa, alikuwa dikteta aliyewanyima watu haki ya kusema. Nani angemkosoa Magufuli wakati akiwa hai, halafu angebaki salama? Tazama alichofanyiwa Lisu. Yuko wapi Ben Saalnane aliekosoa PhD ya Magufuli?

Usizungumze kama vile umeshuka leo toka ahera. Ka ulikuwepo nchini wajati wa Magufuli, huwezi kushangaa kwa nini watu wanasema leo, na siyo wajati wa uhai wake.
 
Samia, kiutendaji amemwacha mbali sana Magufuli. Magufuli alikuwa na speed kubwa katika propaganda, na siyo katila utendaji. Mimi siyo shabiki wa Samia, lakini ukimlinganisha Samia na Magufuli, Samia pamoja na mapungufu yake, atakuwa malaika...
Ni kichaa pekee nchi hii atakuelewa kwa huu ujinga wa kupika, mega projects ndio zinathibitisha umwamba wake, haijawahi tokea.

Unaleta za wazungu wakikupiga wanakutengenezea figure ya kuwa una perform, huijui dunia wewe, kariri tu makaratasi
 
Samia, kiutendaji amemwacha mbali sana Magufuli. Magufuli alikuwa na speed kubwa katika propaganda, na siyo katila utendaji. Mimi siyo shabiki wa Samia, lakini ukimlinganisha Samia na Magufuli, Samia pamoja na mapungufu yake, atakuwa malaika...
Halafu nyie masijala wenye vyeti feki mmekazana kutetea ujinga tu hamujistukii! Hamna ajira kwa msio na vyeti
 
Kosa kubwa kabisa walilotupiga na kitu kizito kuliko mambo yote ni uchaguzi uliopita, nafikiri hii ilisababisha Mungu athihirishe kwamba atakalo yeye, ndio linakua na si kama atakavyo mwanadamu.

Ule uchaguzi ulileta simanzi na ganzi mioyoni mwa wengi. Umetuachia majeraha na ari ya kupiga kura kwa wengi imepotea kabisa.
 
Baada ya hayati Magufuli kufariki maadui zake kazi ikabaki moja tu kuwekeza kwenye propaganda chafu dhidi yake, ili kumuondoa Magufuli mioyoni mwa watanzania wengi walioumuelewa na kuipenda kazi yake...
Umeelekweka vyema ndugu , ni kweli wala rushwa wapiga deal na walioondolewa kwa vyeti fyeki ndo kila leo wanafungua thread kila saa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Samia, kiutendaji amemwacha mbali sana Magufuli. Magufuli alikuwa na speed kubwa katika propaganda, na siyo katila utendaji. Mimi siyo shabiki wa Samia, lakini ukimlinganisha Samia na Magufuli, Samia pamoja na mapungufu yake, atakuwa malaika

Kitu gani Magufuli ilisema kitakamilika wakati fulani halafu kikamilika wakati uliotajwa?

Speed kubwa ya Magufuli ilikuwa katika kudidimiza uhuru wa watu, demokrasia, haki za watu, kukanyaga sheria na katiba, na kudidimiza uchumi.

Wakati wa Kikwete uchumi ulikuwa unakua kwa 7%, Magufuli aliuporomosha mpaka 1.9% (taarifa ya WB), uwekezaji mwaka 2015 ulikuwa unakua kwa 28%, Magufuli aliuangusha mpaka 4%. Utalii mwaka 2015 ulikuwa unakua kwa 15%, mpaka 2019, Magufuli alikuwa ameuangusha mpaka 3.6%. Kwa takwimu hizi, Magufuli alikuwa anaenda spidi kali katika kuangamiza Taifa.

Kitu pekee alichofanikiwa Magufuli kuliko watangulizi waje ni siasa za ulaghai. Na wajinga aliwapata sana, hata wengine kufikiria kuwa alikuwa anafanya mambo makubwa sana kuliko watangulizi wake. Kwa kweli wajinga aliwaokota hasa, lakini wenye akili wanajua kuwa Magufuli alikuwa janga kwa Taifa. Hakuistahili ile nafasi.

Jbo jingine, ni kwamba marehemu Magufuli anasemwa sana sasa kwa sababu moja kubwa, alikuwa dikteta aliyewanyima watu haki ya kusema. Nani angemkosoa Magufuli wakati akiwa hai, halafu angebaki salama? Tazama alichofanyiwa Lisu. Yuko wapi Ben Saalnane aliekosoa PhD ya Magufuli?

Usizungumze kama vile umeshuka leo toka ahera. Ka ulikuwepo nchini wajati wa Magufuli, huwezi kushangaa kwa nini watu wanasema leo, na siyo wajati wa uhai wake.
Mkuu nakupongeza kwa uandishi mzuri ila kichwani huna kitu sababu uchumi wa dunia uliporomoka sababu ya corona, ss ulitwgemea tanzania iwe na uchumi mkubwa kwani ni kisiwa. Pia magufuli anasifika kote duniani kwa maamuzi yake ambayo mengi ni very positive na ni mtendaji asiyeteterwka na husimamia kila anachokiqmini ni sahihi
 
Ni kichaa pekee nchi hii atakuelewa kwa huu ujinga wa kupika,mega projects ndio zinathibitisha umwamba wake ,haijawahi tokea.

Unaleta za wazungu wakikupiga wanakutengenezea figure ya kuwa Una perform,huijui dunia wewe,kariri tu makaratasi
Linganisha hizo gharama za mega projects na pesa alozokopa. Ukisha calculate njoo na jibu sahihi
 
Baada ya hayati Magufuli kufariki maadui zake kazi ikabaki moja tu kuwekeza kwenye propaganda chafu dhidi yake, ili kumuondoa Magufuli mioyoni mwa watanzania wengi walioumuelewa na kuipenda kazi yake.

Waliwekeza mitandaoni kwa kuajiri vijana wa kumponda,threads nyingi ziliandikwa kwa pupa bila umakini.

Walichokosea ni kutoajiri watu makini wa kuchambua hoja zilizoshiba kutofautiana na mtazamo wa Rais Magufuli ili mbivu na mbichi zijitenge.

Matokeo yake wakaajiri wahuni ,wakiwemo na wahanga wa vyeti fake, kazi yao ikawa ni matusi kutwa kucha, matokeo yake wamepuuzwa vibaya sana na pumzi zimekata ghafla

Ukweli ni kwamba , mpaka sasa Magufuli anashaini mioyoni mwa watanzania wengi na anaendelea kuwa prove wrong watesi wake.

Leo mama Samia imebidi ataje jina la Magufuli alipokuwa akiifungua barabara ya mbezi louis,anajua bila Magufuli ushawishi unazidi kupungua.

Mungu mjalie Rais Samia angalau afikie hata nusu ya speed ya hayati Magufuli mambo yatakwenda
Pple sana. Inaonekana bado una majonzi mazito na hauamini kilichotokea March 17, 2021
 
Back
Top Bottom