Hili daraja la Dumila hili!

Hili daraja la Dumila hili!

Munkari

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2013
Posts
8,084
Reaction score
4,363
Inabidi serikali iangalie hii sehemu ya muhimu kwa jicho pana zaidi,hii ni pamoja na kuboresha hili daraja mana nimepita hapo muda si mrefu mto umejaa balaa maji yameanza kupanda hadi darajani,na mvua bado zinaendelea kunyesha.ikiendelea hivi kwa siku mfululizo laweza kusombwa kwa mara nyingine.So nadhani serikali ingejipanga kwa hili.
 
Inabidi serikali iangalie hii sehemu ya muhimu kwa jicho pana zaidi,hii ni pamoja na kuboresha hili daraja mana nimepita hapo muda si mrefu mto umejaa balaa maji yameanza kupanda hadi darajani,na mvua bado zinaendelea kunyesha.ikiendelea hivi kwa siku mfululizo laweza kusombwa kwa mara nyingine.so nadhani serikali ingejipanga kwa hili.



Hakika ndugu me mwenyewe nimepita si muda mrefu hapo yaan hatar tupu...!
 
dah!
hii nchi, mvua shida, jua shida.
Tatizo sio hali ya hewa mkuu, kwani ni Tanzania pekee pananyesha mvua? Hii ni kutokua ni miundombinu bora, kila kitu kinalipuliwa lipuliwa tu..Kila mtu anaiba, unadhani ubora utatoka wapi? Kwa kweli hii inauma sana kwani sisi watoa kodi ndio tunanyonywa.
 
mradi wa watu wanasubiri wajipigie hela kwa kujenga lingine
 
Tatizo sio hali ya hewa mkuu, kwani ni Tanzania pekee pananyesha mvua? Hii ni kutokua ni miundombinu bora, kila kitu kinalipuliwa lipuliwa tu..Kila mtu anaiba, unadhani ubora utatoka wapi? Kwa kweli hii inauma sana kwani sisi watoa kodi ndio tunanyonywa.

hapo sasa! Alafu najiuliza kama lile daraja la mwanzo ambalo ni la muda mrefu japo sijui lilijengwa kwa muda gani na likabebwa sembuse hili ambalo limejengwa kwa muda mfupi? Ama?
 
hapo sasa! Alafu najiuliza kama lile daraja la mwanzo ambalo ni la muda mrefu japo sijui lilijengwa kwa muda gani na likabebwa sembuse hili ambalo limejengwa kwa muda mfupi? Ama?
Budget kubwa zinapitishwa lakini haifikishwi yote kwenye lengo kuu. Tusubiri tu, tuone mwisho utakua nini?
 
Tatizo sio hali ya hewa mkuu, kwani ni Tanzania pekee pananyesha mvua? Hii ni kutokua ni miundombinu bora, kila kitu kinalipuliwa lipuliwa tu..Kila mtu anaiba, unadhani ubora utatoka wapi? Kwa kweli hii inauma sana kwani sisi watoa kodi ndio tunanyonywa.

Wewe unanyonywa nini? unajuwa maana ya mafuriko wewe?
 
Wewe unanyonywa nini? unajuwa maana ya mafuriko wewe?
Mkuu, najua hujua system inavvyofanya kazi, au labda unajua lakini unanufaika nayo..We unaona majumba ya kisasa yanajengwa na magari ya kifahari huko barabarani unadhani hii ni salary pekee? Usijaribu kufunika kombe mwanaharamu apite kwenye uchakachuaji kila kitu kinaonekana. Hayo sio mafuriko, huo ni mfumo mbaya ya miundombinu. naweza sema low cost infrastructure...
 
Huku Daraja la Doma baada ya kutokaMbuga ya Mikumi limejaa na magari yote toka Dar na Nyanda. Za juu kusini yamekwama. Inawezekana ni kwa sababu ya mvua maeneo ya Kilosa
 
Kuna melele napo hali si shwari maji yanapita juu ya daraja na yamesambaa kama robo ya barabara magari mengine yamekwama,ingawa sisi tumeyawahi kidogo kabla ya kujaa zaidi
 
Lakini huu ndio msimu wa masika lazima mvua zinyeshe tu
 
Mkuu, najua hujua system inavvyofanya kazi, au labda unajua lakini unanufaika nayo..We unaona majumba ya kisasa yanajengwa na magari ya kifahari huko barabarani unadhani hii ni salary pekee? Usijaribu kufunika kombe mwanaharamu apite kwenye uchakachuaji kila kitu kinaonekana. Hayo sio mafuriko, huo ni mfumo mbaya ya miundombinu. naweza sema low cost infrastructure...

Kama wewe huzioni fursa zilizopo, kaa ulale.

Eti magari, ulikatazwa kutumia frsa nawe ukanunuwa la kwako? hata hausigeli wangu ana gari.
 
Back
Top Bottom