SAYVILLE
JF-Expert Member
- Mar 25, 2010
- 5,130
- 7,901
Juzi nilipita maeneo ya karibu na Ubalozi wa Ufaransa nikaona bango moja limeandikwa "Kifo cha Imam Husain kinatukumbusha umuhimu wa Uhuru". Huwa nina kawaida nikiona mabango ya dini napendaga kufuatilia zaidi maandiko yale hasa kama kuna ujumbe ambao umenigusa wakati huo.
Ila kuna kitu zaidi kilinigusa pale. Miaka kama 2 iliyopita kuna jamaa mmoja aliyejulikana kama "Hamza" alizua taharuki maeneo yale akarushiana risasi na polisi hadi akauawa. Hili tukio huwa nalikumbuka kila nikipita maeneo yale.
Baadae nilivyotulia nikasema embu ngoja nigoogle kama nitapata maarifa yoyote kuhusu maandiko yale na nimejifunza machache ya kunipa mwanga kidogo:
"Iman Hussein alikuwa mjukuu wa Mtume Muhammad (s.a.w.w), Imam Hussain (as) aliyeuawa Karbala, Iraq , siku ya Ashura."
"Alisimama kidete dhidi ya mtawala dhalimu wa wakati ule, Yazid bin Muawiya, akatoa fundisho la kukataa kumpigia magoti mdhalimu huyo, Ndipo akajitolea maisha yake, akauawa ili kunusuru ubinaadamu na utu."
"Imam Hussein (a.s) hakujitoa Muhanga yeye na familia yake kwa ajili ya Ummah wa Kiislam tu, bali alijitoa muhanga kwa ajili ya manufaa ya Ummah wote duniani."
Sasa mimi sina shida na maandiko hayo wala ndugu zangu wenye imani tofauti na mimi. Nimewaza tu busara ya kuweka bango lile mahali pale ukizingatia kumbukumbu ya tukio lililotokea mazingira yale na hapa simaanishi kama tukio lile lina uhusiano wowote wa masuala ya imani maana sidhani kama tuliwahi kuambiwa hivyo.
Kwa kumalizia, natamani kujifunza Uislamu. Naomba mwongozo naweza kuanzia wapi.
Ila kuna kitu zaidi kilinigusa pale. Miaka kama 2 iliyopita kuna jamaa mmoja aliyejulikana kama "Hamza" alizua taharuki maeneo yale akarushiana risasi na polisi hadi akauawa. Hili tukio huwa nalikumbuka kila nikipita maeneo yale.
Baadae nilivyotulia nikasema embu ngoja nigoogle kama nitapata maarifa yoyote kuhusu maandiko yale na nimejifunza machache ya kunipa mwanga kidogo:
"Iman Hussein alikuwa mjukuu wa Mtume Muhammad (s.a.w.w), Imam Hussain (as) aliyeuawa Karbala, Iraq , siku ya Ashura."
"Alisimama kidete dhidi ya mtawala dhalimu wa wakati ule, Yazid bin Muawiya, akatoa fundisho la kukataa kumpigia magoti mdhalimu huyo, Ndipo akajitolea maisha yake, akauawa ili kunusuru ubinaadamu na utu."
"Imam Hussein (a.s) hakujitoa Muhanga yeye na familia yake kwa ajili ya Ummah wa Kiislam tu, bali alijitoa muhanga kwa ajili ya manufaa ya Ummah wote duniani."
Sasa mimi sina shida na maandiko hayo wala ndugu zangu wenye imani tofauti na mimi. Nimewaza tu busara ya kuweka bango lile mahali pale ukizingatia kumbukumbu ya tukio lililotokea mazingira yale na hapa simaanishi kama tukio lile lina uhusiano wowote wa masuala ya imani maana sidhani kama tuliwahi kuambiwa hivyo.
Kwa kumalizia, natamani kujifunza Uislamu. Naomba mwongozo naweza kuanzia wapi.