hiki ni kigezo cha maendeleo???

Mwadui

Senior Member
Dec 17, 2010
102
2
mbunge wa lushoto Henry Shekifu wakati anachangia mada leo bungeni emesema Uchumi wa Nchi umekuwa kwani ndege(eroplane) zinapishana uwanja wa ndege, anammanisha kuwa uwingi wa safari za ndege ndani na nje ya nchi ni mOja wapo ya vigezo vya kukua kwa uchumi, wa Tanzania, nawauliza wana JF je hiki ni kigezo cha uchumi kukua????
 
Unajua viongozi wetu akili zao ni kama watoto kabisa. Umewahi kuona watoto wakicheza juu ya miti na kunguruma kama magari? Ni sawa na usemi huu. Hivi hawa watu huwa hawapewi hata semina kuhusu mambo ya uchumi? Hata kama serikali haitoi mafunzo kuhusu mambo muhimu je hawana mda wa kujisomea ili kuongeza elimu zao? Nashangaa sana mimi, viongozi gani hawa?
 
Kama kweli kasema hivyo basi namwingiza kwenye orodha ya wale waleeeeeee. Uchumi wa Tanzania unapaaaaaa! uwingi wa magari Dar es salaam! na leo uwingi wa safari za ndege! Kwao nitafsiri ya kukua kwa uchumi (Indicators).Inauma sana hawa viongozi wanamna hii tumewatoa wapi, wamechaguliwa kwa vigezo gani na akina nani wamewachagua?
 
Back
Top Bottom