Hii ya Makonda kupiga salute imekaaje?!

Hii ya Makonda kupiga salute imekaaje?!

Ungesema kujishau manake mabasha siku hizi wanapita nao kimya kimya hawa wanaojichetua
Ni kweli! Nlimuona MANARA ile siku ya SIMBA DAY...alivokuwa anajichetua akiwa na Mo kule chini!
 
Sometimes i find this person funny... kiukweli nashindwaga kumchukia mtu huyu.
 
Wewe ndo zuzu. Mana tunajua kuwa Watu wote hunyenyekea wakubwa. Au hata wadada warembo Pale unapotaka mhhh. Shida hatuwajui Basi kila neno mnaweza Sema. Ila wasema sema watu wengi ni dhaifu sana. Tena wanasuffer hizo Hali wanazopenda kuwatangazia wenzao nyuma ya Tecno.
Mkuu katika comments zote kwenye uzi huu, wewe umenyoosha maneno, ingawa umetumia lugha ngumu kidogo. Ninakupa big up.

Hao wote humu wanaojifaragua kwa lugha za kikakamavu, dharau, matusi nk nk, wallah wakiitwa na Jpm hadharani: '....wewe njoo hapa, hapana, ee yule pale...eee! Wewe, njoo.....'.

Hakuna atakayeenda kushikana mikono na mheshimiwa akiwa kakunja uso.

Atavamiwa na tabasamu la kijinga bila hata ya yeye anayetabasamu, kupanga ama kutarajia.

Linakuja tu kama kichefuchefu kinavyokuvamia baada ya kula kitu kibaya.

Hiyo ni kwa mtu yeyote, hata viongozi wa upinzani mnaowaamini kwa misimamo yao hasi dhidi ya Jpm, akiitwa ni lazima ajichekeleze kijingajinga tu, hakuna ujanja.

Sembuse kwa viongozi waliopo madarakani!

Jamani acheni kudanganyana ili kufurahisha nafsi zenu.
 
Wakati Rais Magufuli anatoka baada ya kikao cha SADC alipita mbele ya viongozi pamoja na wastaafu kuwasalimu na kuwapa mkono, akina Kikwete, Mkapa, Mwinyi, Warioba, Majaliwa, nk.

Ajabu Rais alipofika kwa makonda RC Makonda akapiga salute ndo akampa mkono Rais tofauti na walivyofanya viongozi wengine, hii style ya Makonda huwa naona wanafanya akina Sirro, Mabeyo na maaskari wengine, hata yule mchungaji bosi wa TISS hafanyagi hivyo.

Sasa hii ya leo ya makonda kupiga salute ni mbwembwe tu ama ni nini?
Makonda kuwa kiongozi wa kamati ya usalama ya mkoa naye kashajiona mwanajeshi.
 
Ukiishi jirani na kambi ya Jeshi unakua mwanajeshi pia
 
Hivi nyie katika maisha yenu hamjawahi kuwa chini ya watu wengine?

Ni mbwembwe za kawaida katika kujinyenyekeza kulikopitiliza ili kumuonesha mkubwa wako kwamba yupo/amefanya vizuri.

Ni sawa na kusema, mkuu umefanya vyema sana, hotuba nzuri sana sana, na mambo mengine kama hayo.
Yes,ni sawa na kumwambia mtu aliyefanya vizuri kuwa umetisha Salute kwako.
 
Hahaaa hayo ni maneno ya kawaida tuu ya kumwagia SIFA na utukufu mkubwa/mfalme/boss/tajiri wakeee....
 
Ikitokea huna elimu au ujuz wowote na umezaliwa katika familia yenye kipato kidogo njia pekee ya wewe kufanikiwa ni KUJIPENDEKEZA either kwa bosi wako au mtu yeyote mwenye uwezo
Na Kujipendekeza huzaa Unafiki na Unafiki huzaa Dhambi na Dhambi huzaa mauti
 
Undercover Agent
Wakati Rais Magufuli anatoka baada ya kikao cha SADC alipita mbele ya viongozi pamoja na wastaafu kuwasalimu na kuwapa mkono, akina Kikwete, Mkapa, Mwinyi, Warioba, Majaliwa, nk.

Ajabu Rais alipofika kwa makonda RC Makonda akapiga salute ndo akampa mkono Rais tofauti na walivyofanya viongozi wengine, hii style ya Makonda huwa naona wanafanya akina Sirro, Mabeyo na maaskari wengine, hata yule mchungaji bosi wa TISS hafanyagi hivyo.

Sasa hii ya leo ya makonda kupiga salute ni mbwembwe tu ama ni nini?
 
Labda alikuwa anataka rais awe namba moja kusajili ndoa yake kwenye tuvuti yake ili kupunguza malalamiko ya wasichana na wanawake wanaoumizwa na wanaume maana alisema atatumia mkutano wa SADEC kujifunza kuhusu nchi za SADEC wanafanyaje kuwasaidia wasichana wanaoumizwa kimapenzi maana yeye amepokea malalamiko mengi kutoka kwa wasichana wakilalamika kutoswa na wapenzi wao.
 
Kwani hamuwezi kubishana kwa hoja hadi mtoleane matusi?

Matusi kwa viongozi pia mmezidi,kuweni na staha jamani.

Hakuna wakubwa kwenu, maadili mabaya sana hayo.

Tuwategemee kuwa viongozi wa aina gani in future?
 
Back
Top Bottom