Hii tabia ya Polisi Tanzania imenishtua

Hii tabia ya Polisi Tanzania imenishtua

Dogo wewe kumbe hujatembea,,, ingekua Kenya wangekuomba LIVE ukileta za kuleta wanakubambikia mwende kituoni, huko ile subiri kidogo gari ingekaa siku tatu. Hawa wangekuzushia urongo sasa hivi ungesema.. SI WANGEOMBA TU.

Kwingine ni South Africa. Raia wa kigeni yeyote huwa wanamuita Mobile ATM!
 
Mbugani pale kuna askari!
Basi wana moyo mkavu.
 
Tarehe 16 may nilikua nafanya safar ya kutoka Dar nikiwa naelekea Tunduma Mbeya. Nilikua naendesha gar ya rafiki yangu ambae ni raia wa zambia na tulikubaliana nilisogeze mpaka mpakani yeye atalichukua kwanzia Tunduma. Katika hali isiyokua ya kawaida kwangu nimesimamishwa na askari wa barabarani mara 4 kama ifuatavyo.

Wa kwanza : checkpoint kabla ya misugusugu; aliomba lesseni nikampa akakagua gar na baadae akanambia anaomba hela anunue maji. sikumpatia nikatimka baada ya kuchukua leseni yangu.

Wa pili: Hii ilikua Maseyu Moro. Yeye akanichana live akasema naomba hela njaaa inauma sana. Huyu wa kiume. Nikasema sina na gari inanisumbua nikasepa.

Wa tatu : Doma Morogoro tena huyu alikua mmama anatochi akakuta nina nyama ya mbuzi ndani huwezi kuamini kaiomba mpaka nikamkatia kipande. Akataka na hela nikaruka kama swala.

Mikumi ndani mbugani nikakutana na wengine hawa hawakua na madhara sana nikiwapiga sound wakaniacha. Sikua na kosa kwani gar yangu ilikua na king'amuzi.

Wa mwisho alieniua ni huyu wa nne: huyu nimekutana nae hapa chekpoint ya kuingia Mbeya kanisimamisha akasema "naomba japo buku mbili si unaona baridi hili?" nikamtosa nikimwambia sina hata kumi. Akasema poa nikasepa.


Hii haina maana hakuna wengine walionizingua kama pale check point Iringa ila hawa wa kuomba live live ndo noma.

Nikajiuliza: hawa jamaa wanashida gani?

Wamekula maharage gani?.

Hawaoni aibu?

Dah. Nilitaman kuwarekodi ila nilishindwa.

Ngoja nimalize safari.

Asanteni.

Hesabu zinakupiga chenga kidogo eee, hiyo checkpoint ni ya mpaka wa Njoluma na Mbeya au ni ile pale Chimala?
 
Nchi yenyewe ni ombaomba,Hiyo buku 2 utaona ndogo na kumdharau Lakin akipokea kwa watu 100 kwa siku ni Laki 2,piga kwa mwezi,wana hakiri sana hao sio njaa ni wajasiriamali
 
Tanzania tunatengeneza rushwa nchi zingine traffic hasimamishi gari mpaka aone kosa moja kwa moja lkn hapa TZ anakupiga mkono halafu anaanza kutafuta kosa!
 
Posho ya maaskari wetu ni 50,000 kwa mwezi wakati kuna wateule hata laki 2 kwa siku wanalalamika haitoshi. Wakiomba ni kielelezo cha hali ngumu walizonazo na wapewe tu wakiomba, siyo rushwa hiyo ni nchi tu imewavuruga
 
Nchi yenyewe ni ombaomba,Hiyo buku 2 utaona ndogo na kumdharau Lakin akipokea kwa watu 100 kwa siku ni Laki 2,piga kwa mwezi,wana hakiri sana hao sio njaa ni wajasiriamali

Muache aendelee kuona aibu yeye.watu wanaishia hivyo.
 
Kuna siku, mmoja maeneo ya bomang'ombe mkoani Kilimanjaro alinipigia magoti. Tena askari wa kiume, dah ilibidi nimtoe elfu mbili.

Hawa watu wana njaa sana.
 
Tarehe 16 may nilikua nafanya safar ya kutoka Dar nikiwa naelekea Tunduma Mbeya. Nilikua naendesha gar ya rafiki yangu ambae ni raia wa zambia na tulikubaliana nilisogeze mpaka mpakani yeye atalichukua kwanzia Tunduma. Katika hali isiyokua ya kawaida kwangu nimesimamishwa na askari wa barabarani mara 4 kama ifuatavyo.

Wa kwanza : checkpoint kabla ya misugusugu; aliomba lesseni nikampa akakagua gar na baadae akanambia anaomba hela anunue maji. sikumpatia nikatimka baada ya kuchukua leseni yangu.

Wa pili: Hii ilikua Maseyu Moro. Yeye akanichana live akasema naomba hela njaaa inauma sana. Huyu wa kiume. Nikasema sina na gari inanisumbua nikasepa.

Wa tatu : Doma Morogoro tena huyu alikua mmama anatochi akakuta nina nyama ya mbuzi ndani huwezi kuamini kaiomba mpaka nikamkatia kipande. Akataka na hela nikaruka kama swala.

Mikumi ndani mbugani nikakutana na wengine hawa hawakua na madhara sana nikiwapiga sound wakaniacha. Sikua na kosa kwani gar yangu ilikua na king'amuzi.

Wa mwisho alieniua ni huyu wa nne: huyu nimekutana nae hapa chekpoint ya kuingia Mbeya kanisimamisha akasema "naomba japo buku mbili si unaona baridi hili?" nikamtosa nikimwambia sina hata kumi. Akasema poa nikasepa.


Hii haina maana hakuna wengine walionizingua kama pale check point Iringa ila hawa wa kuomba live live ndo noma.

Nikajiuliza: hawa jamaa wanashida gani?

Wamekula maharage gani?.

Hawaoni aibu?

Dah. Nilitaman kuwarekodi ila nilishindwa.

Ngoja nimalize safari.

Asanteni.
Mkuu kuomba si dhambi na inavyoonesha wote walikuwa wanakuomba tu,
njaa kali!
 
Arusha wanakuomba mpaka hela ya petrol ya magari yao waliyokuja nayo checkpoint
 
Hilo ni tatizo la kisaikolojia nadhani japo so mtaalam maana mtu akiingia upolisi tu hata kama ni ndugu yako anakuwa mtu wa kupenda dezo dezo hata kwenye mambo ya msingi ya ndani ya familia. Issue sio mshahara wala nini bali ni ile position yao ya kumkamata mtu awe na kosa au hana alafu anapotoka wanakula kichwa either kwa lazima au kujifanya kama amekusaidia na wewe unaingia kingi unampa ahsante huku kichwani unaetoa ukiamini kwamba ipo siku ukiwa na tatizo la kipolisi atakusaidia, kutokana na hiyo hali kujengeka miaka na miaka imewafanya wawe na tabia hiyo ya kuomba omba. Hizi kazi wakati mwingine zinatubadili kama vile watu wa kada flani ambao wanaongoza kulalamika kama vile mshahara wanaolipwa ni kidogo
 
Tarehe 16 may nilikua nafanya safar ya kutoka Dar nikiwa naelekea Tunduma Mbeya. Nilikua naendesha gar ya rafiki yangu ambae ni raia wa zambia na tulikubaliana nilisogeze mpaka mpakani yeye atalichukua kwanzia Tunduma. Katika hali isiyokua ya kawaida kwangu nimesimamishwa na askari wa barabarani mara 4 kama ifuatavyo.

Wa kwanza : checkpoint kabla ya misugusugu; aliomba lesseni nikampa akakagua gar na baadae akanambia anaomba hela anunue maji. sikumpatia nikatimka baada ya kuchukua leseni yangu.

Wa pili: Hii ilikua Maseyu Moro. Yeye akanichana live akasema naomba hela njaaa inauma sana. Huyu wa kiume. Nikasema sina na gari inanisumbua nikasepa.

Wa tatu : Doma Morogoro tena huyu alikua mmama anatochi akakuta nina nyama ya mbuzi ndani huwezi kuamini kaiomba mpaka nikamkatia kipande. Akataka na hela nikaruka kama swala.

Mikumi ndani mbugani nikakutana na wengine hawa hawakua na madhara sana nikiwapiga sound wakaniacha. Sikua na kosa kwani gar yangu ilikua na king'amuzi.

Wa mwisho alieniua ni huyu wa nne: huyu nimekutana nae hapa chekpoint ya kuingia Mbeya kanisimamisha akasema "naomba japo buku mbili si unaona baridi hili?" nikamtosa nikimwambia sina hata kumi. Akasema poa nikasepa.


Hii haina maana hakuna wengine walionizingua kama pale check point Iringa ila hawa wa kuomba live live ndo noma.

Nikajiuliza: hawa jamaa wanashida gani?

Wamekula maharage gani?.

Hawaoni aibu?

Dah. Nilitaman kuwarekodi ila nilishindwa.

Ngoja nimalize safari.

Asanteni.


matatizo ya kukodiwa kulinda ccm waendelee kuwa madarakani kwa nguvu huku wakilipwa posho badala ya mishahara. Next time weka kamera ndogo kwenye gari, itegeshe iwaone vema mpaka sura zao na sauti zao zisikike kisha rusha live. Technolojia inaruhusu.
 
We mtoa mada ni mgeni barabarani? acha ujinga unatusiribia madereva, wangekuandikia ungesemaje?
 
Kuna siku, mmoja maeneo ya bomang'ombe mkoani Kilimanjaro alinipigia magoti. Tena askari wa kiume, dah ilibidi nimtoe elfu mbili.

Hawa watu wana njaa sana.

Arusha wanakuomba mpaka hela ya petrol ya magari yao waliyokuja nayo checkpoint

Wapeni tu kama mnazo...........wangekuwa nazo wasingewaomba..........mbaya ni kuomba rushwa..........polisi wa bongo ndio hivyo walivyo siku zote..........
 
Back
Top Bottom