Hii tabia ya Polisi Tanzania imenishtua

Hii tabia ya Polisi Tanzania imenishtua

Dawa yao ni kuwanyima tu. Ukiwapa unaendekeza upumbavu. Mimi sijawahi kuwapa pesa hawa watu. Watanzania nchi hii tunaijenga wenyewe na kuibomoa wenyewe.
Big up mleta uzi. Lakini isije kuwa uliwapa hapa unakataa!!
 
Hii ndio tz

Na Usishangae mijitu mizima itatetea polisi kuomba omba hela
 
Nikiwa natoka zangu likizo Mwanza kurudi dom, nimepigika vibaya.

Mida ya sa mbili usiku karibia dodoma nakutana na askari wa doria, baada ya maswali kadhaa na kukagua ndani ya gari, mmoja akasema tunaomba utugawie chochote ulichotoka nacho safari hata mchele au viazi......i was lyk ayaaaaaaaa...kiukweli askari wanajiaibisha sana. Baada ya kung'ang'ana sana nikawapatia 1000.
 
Sasa mkuu umeshasema ilikuwa tarehe 16, tarehe hizo hali kwa wafanyakazi wa umma zinakuwa tete! Walioko huko wanajua. Kwa maaskari muda mwingine Mshahara wanapata kuanzia trh 20, sasa ikifika trh 16 mwezi unaofuata unadhani atakuwa na kitu?

Sikuona haja ya wewe kuja kuwananga hapa, labda km wewe ni mzambia na hujui hali za watanzania.

Ninapoenda hata kupata msosi kwenye restaurant, wahudumu wananiomba hela ya maji au chakula. Kama bajeti yangu iko poa nampa tu, mtu kukuomba buku 2 au jero sio sbb ya kumleta hapa na kumnanga.

Hilo la wao kukagua gari ni wajibu wao na siyo kwamba anatafuta kosa. Akikuacha ukapata tatizo huko mbele utakuja kumsema tena.

Isome vizuri jamii yako, na utaweza kwenda nayo sambamba. Amani!
 
Sasa mkuu umeshasema ilikuwa tarehe 16, tarehe hizo hali kwa wafanyakazi wa umma zinakuwa tete! Walioko huko wanajua. Kwa maaskari muda mwingine Mshahara wanapata kuanzia trh 20, sasa ikifika trh 16 mwezi unaofuata unadhani atakuwa na kitu?

Sikuona haja ya wewe kuja kuwananga hapa, labda km wewe ni mzambia na hujui hali za watanzania.

Ninapoenda hata kupata msosi kwenye restaurant, wahudumu wananiomba hela ya maji au chakula. Kama bajeti yangu iko poa nampa tu, mtu kukuomba buku 2 au jero sio sbb ya kumleta hapa na kumnanga.

Hilo la wao kukagua gari ni wajibu wao na siyo kwamba anatafuta kosa. Akikuacha ukapata tatizo huko mbele utakuja kumsema tena.

Isome vizuri jamii yako, na utaweza kwenda nayo sambamba. Amani!

kwanza mimi ni mtanzania, sijaja kumnanga mtu.

Unachotoa hotelini ni tip.... ambayo inaruhusiwa. Sasa nimpe askari tip kwa lipi?.

Pole kama post hii imekuboa ila wajirekebishe....
 
kwanza mimi ni mtanzania, sijaja kumnanga mtu.

Unachotoa hotelini ni tip.... ambayo inaruhusiwa. Sasa nimpe askari tip kwa lipi?.

Pole kama post hii imekuboa ila wajirekebishe....

Lakini mkuu!!.kama huna si unamwambia huna then unasepa!!!.

kuja kuandika humu tunatafsiri kuwa unawaponda polisi wana njaa ya ajabu wakati wewe unayo ya ajabu zaidi kushindwa kuwapa buku mbili.

Huna kausha mpaka tujue ulikosa buku mbili ya kuwapa jamaa!!!!
 
Nikiwa natoka zangu likizo Mwanza kurudi dom, nimepigika vibaya.

Mida ya sa mbili usiku karibia dodoma nakutana na askari wa doria, baada ya maswali kadhaa na kukagua ndani ya gari, mmoja akasema tunaomba utugawie chochote ulichotoka nacho safari hata mchele au viazi......i was lyk ayaaaaaaaa...kiukweli askari wanajiaibisha sana. Baada ya kung'ang'ana sana nikawapatia 1000.

We endelea kuona aibu,kwa niaba ya askari polisi wote.

Wenzio wamekatwa mishipa ya aibu depo.wanachoangalia wao 30per day.
 
Huyo aliye taka Kipande cha nyama ya mbuzi ndy kaniacha hoiiii hehehehe
 
Dogo wewe kumbe hujatembea,,, ingekua Kenya wangekuomba LIVE ukileta za kuleta wanakubambikia mwende kituoni, huko ile subiri kidogo gari ingekaa siku tatu. Hawa wangekuzushia urongo sasa hivi ungesema.. SI WANGEOMBA TU.
 
Waoneeni huruma angalia ubungo mataa wanavoteseka kampuni ya strabag inashindwa kufunga temporally trafic lights ubungo mataa askari wanateseka sana pale
 
Ungewapa kaka.
Mi niendapo masafa marefu kama hayo nikiona wamezubaa sana kwenye kituo fulani huwa nasimamisha gari na kupozi nao kidogo wananieleza mavitu kibao ya kwenye kampuni yao kisha nikiwa salama mfukoni nawafuta machungu kiaina. Naelezwa mengi sana nahao jamaa kwa mtindo huo
 
Afadhali hao walikuomba live sasa kutana na wale ambao njaa imefungua turbo.Atakagua gari wee akikuta kila kitu kipo utasikia huu muungurumo sio wa hii gari yaani ilimradi tu apate kosa na akupige hela.
 
kwanza mimi ni mtanzania, sijaja kumnanga mtu.

Unachotoa hotelini ni tip.... ambayo inaruhusiwa. Sasa nimpe askari tip kwa lipi?.

Pole kama post hii imekuboa ila wajirekebishe....

jambo lingine hiyo tarehe 16 walinda amani woote wa Tanzania kuanzia police, jawtz, magereza mpaka zima moto wanakuwa wameshapewa posho ya katikati ya mwezi ambayo haipungui laki na nusu sasa hizo njaa zinatoka wapi??

Tatizo watanzania tunawaendekeza hawa Askari njaa kwa kuwapa hela ndiomana hawakomi kuomba.

Jeshi la Police libadilike dunia ya sasa sio ya mwaka tisini. Inatia aibu sana Askari anakuomba buku wakati mwisho wa mwezi analipwa mshahara na kila katikati ya mwezi anapokea posho ya laki na nusu.

Tatizo la nchi yetu karibu kila mtumishi wa umma ni fisadi /mwizi kuanzia juu kabisa mpaka chini kabisa.

Wanatofauriana tu kwa namna ya kuiba na kiasi wanachoiba.
 
jambo lingine hiyo tarehe 16 walinda amani woote wa Tanzania kuanzia police, jawtz, magereza mpaka zima moto wanakuwa wameshapewa posho ya katikati ya mwezi ambayo haipungui laki na nusu sasa hizo njaa zinatoka wapi??

Tatizo watanzania tunawaendekeza hawa Askari njaa kwa kuwapa hela ndiomana hawakomi kuomba.

Jeshi la Police libadilike dunia ya sasa sio ya mwaka tisini. Inatia aibu sana Askari anakuomba buku wakati mwisho wa mwezi analipwa mshahara na kila katikati ya mwezi anapokea posho ya laki na nusu.

Tatizo la nchi yetu karibu kila mtumishi wa umma ni fisadi /mwizi kuanzia juu kabisa mpaka chini kabisa.

Wanatofauriana tu kwa namna ya kuiba na kiasi wanachoiba.

Acheni askari wetu waishi, aibu,? unataka wafe njaaa?? Mbona umekosa Ustaarabu? Mshahara wa Kumfanya askari awe mwaminifu hapa Tanzania ni Shillingi ngapi?? Watu wote wangekuwa kama mtoa maada ingebidi ujambazi uongezeke maana kusema ukweli laki na nusu inatosha kuishi siku moja au mbili tuu! Tuwapiganie wenzetu mishara ipande, maana hawaruhusiwi kwa sheria zetu hata kugoma, wamefungiwa uzio. Nchi hii hamna equity, hela zipo kwa akina chengeiba.
 
Back
Top Bottom