Hii ni kupeana hasara tu.

Hii ni kupeana hasara tu.

hatapata zawadi kutoka kwangu tenaaaaaaaaaaaaaa
eboooooooooo

Rafiki yangu mmoja namfurahia sana, ana mke na watoto 2 akiwatoa out, anawaambia waagize wanachotaka wakisha agiza na akajua walichoagiza kitawashinda yeye anaagiza kidogo, wakibakisha anakula chote cha mkewe na cha watoto pia.
 
ni kweli hii inakera sana, kitu si gharama shida ni kwann hamalizi? unakuta mtu kwao anapiga dona la kufa mtu tena na nyongeza juu akifika kwa hotel kama hivyo ati anaonyesha pozzi nyoooh! kama mm nimempeleka mtu akabakiza namuita mhudumu namuambia please naomba ukipashe then mfungie akamalizie hom. vilevile huwez jua budget ya mtu mwingine ndo anaimbisha mwenzio kajinyima yeye akakutoa out then unaleta pozi, halafu kuna wengine tena unaweza kwenda nae ukaagiza coke light, utasikia sminof, au wine au castle light, nyoooh na wakome, sazingine sikilizia mwenyej wako bana, kama kaagiza cha buku 3, na unatamani cha buk 5 muulize kwanza kama hana salio itakuwaje? na wadada wengi wanavyopenda dezo unakuta umemtoa out hana hata mia.
 
Dawa yake ndogo sana. Mkifika hoteli mwambie yeye aagize halafu we tulia na kinywaji tu, akijishaua unaingiza timu mwenyewe halafu unakuwa umesave money
 
Dawa yake ndogo sana. Mkifika hoteli mwambie yeye aagize halafu we tulia na kinywaji tu, akijishaua unaingiza timu mwenyewe halafu unakuwa umesave money

Atashutuka na kukuhoji, kwanini ale peke yake?
 
Jamani nanyie wanaume hamueleweki, ukibakiza kesi, ukila chote anakushanga ati hee umemaliza? anaanza kukuchombeza mmh kwel wewe kbko. teh yalishanikuta
 
Fikiria umempeleka mtu hotelini/mgahawa, ukamwambia aagize anachokitaka, akaagiza sahani ya chips, kuku nusu na soda, alafu katika vyote hivyo kila kimoja anatumia nusu nusu anaacha.

Hii tabia huwa inanikera sana, sijui wewe unasemaje kuhusu tabia hii.

Ehee, kama ulikuwepo vile yaliyonikuta. Si unafahamu samaki wa Mwanza kule jirani na uwanja wa CCM Kirumba (Villar Pack). Mtu wangu kaagiza samaki mzima na chips, nami kwa kuwa nilikuwa na hamu na samaki baada ya kuchoshwa na wa majichumvi nikaagiza hivyo hivyo, tukaanza kula kila mmoja kwenye sahani yake. Basi mtu wangu kanyofoa kipande kidogo upande wa tumboni tena kwa kutumia ncha za vidole, baada ya hapo akachukua vipande vinne vya chipus, halafu akajifuta kwa kutumia tissue ndio kashiba hivyo. Nikajiuliza kama alijisikia kushiba, kwa nini hakusema tungeshare kile chakula kuliko yeye kuagiza cha kwake mbali. Bili ilipoletwa 22,000/= ukiondoa vinywaji, Yesu yani Mfuko wa cementi na zaidi. Jamani Wadada tuoneene huruma pesa ni ngumu kutafutwa.
 
Jamani nanyie wanaume hamueleweki, ukibakiza kesi, ukila chote anakushanga ati hee umemaliza? anaanza kukuchombeza mmh kwel wewe kbko. teh yalishanikuta

Mimi napenda mtu anayemaliza chote, maana mimi huwa sibakishi hata punje, kama ni kuku au samaki mifupa tu ndiyo inabaki kwenye sahani.
 
Na ni ustaarabu sana kula chote ulichoagiza.... Hii inaonyesha unajifahamu kuanzia njaa yako na ulaji wako. kuna mijitu kuacha msosi ndo inadhani ni usasa, kumbe ujinga mtupu....
Bora huyo anayeagiza akaletewa ujazo wa sahani kwa mujibu wa mpango wa hotel husika, wapo watu kwenye bufee wanajipakulia chakula kingi kuliko uwezo wake, halafu anakula kidogo na kingine kinamwagwa. Unashindwa kuelewa nini maana ya self service!
 
Back
Top Bottom