Acha ujinga kwani umeshindwa kusafiri? Mbona kuna nchi nyingi tu hazina ndege za Serikali?
Watu kama ninyi ndiyo hamfai kuwa viongozi kwa maana mna akili zisizoona mbali, hapo ningekuelewa kama ungesema kwamba umeshindwa kufika Dubai ilikubidi usafiri mpaka Kigali ndiyo uweze kupata ndege ya kwenda Dubai, lkn kama unaweza kusafiri ktk TZ mpaka Dubai kila siku tena mara mbili kwa siku kuna ndege tatizo liko wapi?
Mbona kuna nchi nyingi tu hazina ndege za Serikali? Marekani haina Kampuni ya ndege ya Serikali zote ni za watu binafsi, Nigeria haina shirika la ndege la serikali, nchi ya Uswisi hii ni nchi tajiri klk zote Duniani haina ndege ya Serikali (National airline) Swiss air ilifilisika ikanunuliwa na Lufthansa ya Ujerumani na hivi leo inamilikiwa na Ujerumani sasa kwanini kwetu iwe ishu?
Cha muhimu hapa kuna usafiri wa kuaminika unaounganisha TZ na Dunia? Hilo ndilo muhimu!