Katika umri wangu huu nimekutana na changamoto zote ulizozieleza. Lakini nimejifunza kuwa positive. Mwenye ubaya ana uzuri wake pia, hata kama ni kidogo. Bahati mbaya umechagua kuona ubaya wao.
Ukweli usioweza kuruka ni kwamba udugu ni hazina. Ndiyo maana ukifa, au ukaumwa na kulazwa muda mrefu hospital, umepata ajali huna fahamu nk, washikaji zako pamoja na yote mema watayokufanyia watakurudisha kwa ndugu zako. Na iwe kwa masingo au ukarimu ndugu watakupokea TU.
Hili la mwisho linadhihirisha kuwa nduguzo ni kama kivuli chako, huwezi kukikwepa. Jifunze namna ya kuishi na ubaya haulipwi kwa ubaya. Kufanya hivyo unakuwa sehemu ya ndugu wenye matatizo. Show the difference
Dah basi mzee kama umepitia kuna kipande cha somo haujakielewa au pengine uliwachukulia tofauti hawa ndugu zako kwa namna ambavyo ulipitia.
Nadhani kuna level ya maisha ukiwapo unajua kwamba hapa siwezi wategemea hawa ndugu zangu maana si watu wenye uwezo wa kunitoa au kunisapoti nilipo halafu kuna level unaona kabisa huyu hapa anaweza nisaidia hiki kipo ndani ya eneo lake na hashindwi ila kaamua kutochukulia serious issue yangu kwasababu zake personal aidha uoga wa maisha, hataki kukudhamini sababu haoni impact au matokeo ya kile anachotaka kufanya na kadhalika.
But unamuona anafanya jambo kama lile kwa watu wengine na hakuna uzito. Ntakupa mfano, una labda kaka yako mkubwa, unamuomba akusapoti kiasi cha laki 5 au milioni na ni pesa ambayo utarudishia sio kuichukua.
Halafu anakwambia mimi kwa sasa sina hiyo pesa. Halafu wewe unachat na mkewe anakupa story kuwa amemkatia tiketi ya ndege yeye na watoto wanakwenda Dubai vacation au kutembea Serengeti kwa muda wa wiki mbili kula bata. Ukipiga hesabu za haraka hiyo hapo ataspend si zaidi ya 3milion. Na hapo huyo shemeji yako anazungumza haya na wewe ni mieze labda miwili baade baada ya kumpelekea shida zako kaka yako na hajui chochote kuwa una hizi taarifa.
Unaamua kukubali kuwa kila mtu kwenye maisha ana mipango yake na pesa zake na halazimishwi kupangiwa matumizi.
Fast-forward miaka kadhaa mbele, kwanza unashangaa huyu kaka yako anakutafuta halafu anakuwa kama analaumu mbona haumtafuti siku hizi. Halafu unakuja kusikia analeta story za wewe hauhudhurii vikao au msiba wa ndugu (kumbuka kuna misiba mingi umeenda na yeye haukumuona na kama ipo uliyokosa ni ile ilikukuta upo safari labda au mbali na eneo la msiba).
Mara kutokee harusi yeye akutafute muende wote kwenye kikao au atengeneze mazingira ya kutaka mkutane pub mpate kinywaji.
Mara usikie kuwa anakusema kuwa unaharibu pesa (ambazo hajui wala hana taarifa nazo[emoji23][emoji23][emoji23] anahisi tu kuwa unazo sababu aidha picha anazoona au kukuona sehemu fulani).
Mara aseme tuanzishe michango ya familia tuwe kama na mfuko wa kuchangia. Sasa unamuuliza tuchangie mfuko wa kazi gani kwani hapa sisi ni watu Baki si ni familia wewe ukiwa na shida bi mkubwa si huyu hapa au si utumie akiba zako. Anaanza kulaumu na kusema wewe hauna umoja na wenzako. [emoji23][emoji23] Sasa unajiuliza umoja gani huo ambao mwanzo haujaona umuhimu wake ila saa hii unaufosi tena kwa nguvu. Mimi siutaki maana nilipouhitaji haukuwapo so kama mtaunda umoja pambaneni nao mimi simo mimi ninao umoja wangu huku nje na nimeridhika nao maana nimeshasota sana sikuona faida ya umoja huu wenye sifa kama za Umoja wa Africa.
Kimsingi mtu anakuwa kama anakutafuta maneno na ukorofi ila unaamua kukausha unakaa mbali sasa anateseka sana. Sasa huyu ni m'moja na kuna dogo wa kike yeye ana akili za kifeminist mwehu si kidogo na nisivyowapenda wale wadudu ndio dogo anazidi kunichefua.
But watoto wao nipo nao vizuri na ndugu wapo ambao tunaelewana na hawana itikadi za kikuda na tunaishi fresh tu tukikutana amani imetawala. Shida ni ile unashangaa hawa wafamilia moja halafu wanaleta mambo meusi hii imekaaje.