LIKUD
JF-Expert Member
- Dec 26, 2012
- 15,202
- 27,325
- Thread starter
- #41
Midu was something elseJamaa alikuwa mwanangu kinoma. Wakati ule Ubungo panazingua foleni miaka ya 2005 nikiwa kwenye foleni asubuhi naelekea Mwenge niliibiwa Motorola yangu smartphone,nikamwambia konda fungua mlango nishuke,abiria walinishangaa sana wakasema wewe unapoteza muda wako na utaenda kupigwa bure huko,nikawajibu kuwa kesho asubuhi tukijaliwa kukutana nitawaonyesha simu yangu.
Basi bwana,nikashuka nikateremka na ile down ya darajani kama unaenda Chibuku,nilikuwa najua maskani yake Midu yapo wapi,nikafika nikamkuta ndio anaamka,nikamwambia bingwa hapa vijana wako wamepiga Motorola yangu muda huu huu,akaniambia unaelekea wapi nikamwambia Mwenge,akaniambia wewe nenda ukirudi pitia pale darajani kwa yule fundi saa utakuta simu yako,kweli baadae nilipomaliza mishe zangu nikapitia pale nikakuta simu yangu kama ilivyo. Kesho yake asubuhi nakutana na yule konda kituoni nikamwambia cheki mtambo huu hapa.