Manyerere Jackton
JF-Expert Member
- Dec 11, 2012
- 2,438
- 4,463
Ndugu yangu, Butiama imeharibiwa na wananchi wenyewe. Mimi ni mzaliwa wa Butiama. Kijiji cha Butiama kilishapiga hatua kubwa sana kimaendeleo, pengine kuliko vijiji vingi vya Tanzania-chini ya Mwenyekiti mahiri, Joseph Kizurira Nyerere (Kumurungu Kwata Obhike).
Butiama unayoiona sasa ni magofu kutoka na wizi na ufisadi wa viongozi wajinga. Butiama ilishakuwa na kiwanda cha useremala cha kisasa, kiwanda cha kushona nguo za kila aina, benki za Posta na NBC, Posta na Simu, ilishakuwa na combine Harvester, matrekta zaidi ya 15 au 20, Fiat 110 na 682 na tela; planters, shamba la ng'ombe waliokamuliwa kwa mashine, petrol station, mashine za kusaga na kukoboa, wanafunzi walipewa maziwa mara mbili -tatu kwa wiki, wanafunzi walishonewa sare na kugawiwa mbili hadi tatu kwa kila mmoja, madawati yote yalikuwa mninga, ilikuwa na malori yasiyo na idadi, bulldozer, hospitali yenye hadhi ya wilaya, nyumba ya kulala wageni (mwitongo), jumba la maendeleo, duka la kijiji, maji ya bomba kutoka Mugango hadi nyumbani kwetu Muhunda; na kila kitu kilichostahili kwa maisha ya mwanadamu.
Baada ya Mzeed Joseph kung'atuka, wapuuzi wameuza kila kitu, hadi mataili na vyuma chakavu. Wameng'oa hadi nyaya za umeme katika ofisi za umma. Kwa hali hiyo utamshutumu Mwalimu? Butiama ilikuwa na misitu. Lero miti inakatwa mkaa kana kwamba haina maana wala umuhimu. NI wajibu wa wana Butiama sasa kufaidi matunda ya uhalibifu wao. Mimi nyumbani kwangu ni maji ya kisima kirefu. Wananchi wanateka maji bure. Ni maji safi na salama kabisa. Asiye na maji, anakaribishwa kwangu.
Butiama unayoiona sasa ni magofu kutoka na wizi na ufisadi wa viongozi wajinga. Butiama ilishakuwa na kiwanda cha useremala cha kisasa, kiwanda cha kushona nguo za kila aina, benki za Posta na NBC, Posta na Simu, ilishakuwa na combine Harvester, matrekta zaidi ya 15 au 20, Fiat 110 na 682 na tela; planters, shamba la ng'ombe waliokamuliwa kwa mashine, petrol station, mashine za kusaga na kukoboa, wanafunzi walipewa maziwa mara mbili -tatu kwa wiki, wanafunzi walishonewa sare na kugawiwa mbili hadi tatu kwa kila mmoja, madawati yote yalikuwa mninga, ilikuwa na malori yasiyo na idadi, bulldozer, hospitali yenye hadhi ya wilaya, nyumba ya kulala wageni (mwitongo), jumba la maendeleo, duka la kijiji, maji ya bomba kutoka Mugango hadi nyumbani kwetu Muhunda; na kila kitu kilichostahili kwa maisha ya mwanadamu.
Baada ya Mzeed Joseph kung'atuka, wapuuzi wameuza kila kitu, hadi mataili na vyuma chakavu. Wameng'oa hadi nyaya za umeme katika ofisi za umma. Kwa hali hiyo utamshutumu Mwalimu? Butiama ilikuwa na misitu. Lero miti inakatwa mkaa kana kwamba haina maana wala umuhimu. NI wajibu wa wana Butiama sasa kufaidi matunda ya uhalibifu wao. Mimi nyumbani kwangu ni maji ya kisima kirefu. Wananchi wanateka maji bure. Ni maji safi na salama kabisa. Asiye na maji, anakaribishwa kwangu.