Hii misemo imenichosha!

stevoh

JF-Expert Member
Joined
Dec 5, 2011
Posts
2,921
Reaction score
1,106
kwel mimi nakithamini sana kiswahili ila misemo yake inanchosha sana tena si kidogo! Utakuta msemo huu unasema
¤haraka haraka haina baraka, mwingine
¤polepole ndio mwendo, mwingine
¤ngojangoja yaumiza matumbo, mwingine
¤chelewa chelewa unamkuta mwana si wako. Nimekanganywa nayo! Mwenzangu wew waonaje?
 
Kwanini imekuchosha? Ni vizuri kutoa ufafanuzi kidogo.
 
Yote hiyo hutakiwi kuichukulia literal.
Unatakiwa uangalie situation uliyopo kisha upime kama kusubiri ni bora kuliko kuharakisha,ama kuharakisha ni bora kuliko kuchelewesha.

Pia kila kimoja kinatakiwa kifanyike kwa kiasi, ndio maana siku hivi tunasema mvumilivu hula mbivu au mbovu.

Hivyo kama utakua mjanja na kujua kwa muda gani usubiri faida itakua kwako, ila ukizidisha hasara ni yako wewe.
 
Haaaaa nadhani umesahau ule msemo
Mtaka nyingi na saba upata mwingi msiba
 
This is among the Reason i LOVE mY Bible " KILA JAMBO NA WAKATI WAKE"
 
Kwanini imekuchosha? Ni vizuri kutoa ufafanuzi kidogo.

ukilalia kwenye moja nyingine inakuganda nashindwa kutumia kwan nikitumia mmoja mwingine unaupinga
 

ilo nalo neno
 
daah! Ipo mingi sana mingine ndo naijua na kuiona leo ila lugha gongana cjui maana ya mingine
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…