carmel
JF-Expert Member
- Aug 24, 2009
- 2,836
- 262
Jana nilikuwa naangalia movie moja inaitwa A diary of a tired black man, niliipenda na ikanifikirisha sana. inaelezea jinsi african-american women wanavyoharibu relationship zao kwa ajili tu ya matatizo waliyopitia katika maisha yao. Yani vitu kama kukosa malezi ya baba na mama (kwamba majority wamelelewa na mzazi mmoja hasa mama, so hawakuwa na father figure), pia previous relationship kama zilikuwa abusive, wanacarry that anger to a next relationship, na pia type ya marafiki wa kike walio nao, wengi wao ni ambao wamefail kwenye r/ship zao kwa sababu kama hizo na hivyo wanaadvise vibaya. Hii inasababisha hata kama mwanamke kapata mwanaume mzuri asiye na tatizo lolote kusuffer kwenye r/ship na kuamua kuondoka. Nimelileta hapa ili kupata mawazo ya wengine maana kwa mawazo yangu mimi nadhani hili linakuja kwa jamii yetu kwa kasi pia, tunashughudia divorce nyingi kwa sasa, na hata kama siyo divorce, ndoa nyingi zina migogoro, watu wanaishi kwa machale zaidi kila mtu akiwa mguu ndani mguu nje. Watu wengi waliokuwa wanahojiwa wamekubali kwamba wanawake wengi wana hasira au wana vitu wameficha ndani ya roho zao vinavyoleta anger attack unnecessarily. Hiyo imepewa jina la Angry Black Woman Syndrome (ABWS). Ningependa kila mtu ajiangalie je:
Kama wewe ni mwanamke;
ni mwanamke mwenye hasira,
je marafiki zako wa kike ni wanawake wenye hasira
nini kinachofanyaga mahusiano yako kuharibika?
Ukisema au kujiona strong woman, huwa unamaanisha nini?
Kama wewe ni mwanaume;
Ulishawahi kuwa na mahusiano na mwanamke mwenye hasira?
na kama jibu ni ndiyo, hali hiyo ikufanya ujisikieje?
Je hali hiyo ilikufanya uchoke?
Na kwa wote
Mnasolve vipi matatizo ya kimahusiano yanapotokea?
Mwisho atakaeyeweza kuipata hii movie aiangalie, inasaidia kukufanyia self- analysis na kujua uliposimama. (najua kuna watu wameshaiona hii mpvie/documentary). Ingine yenye theme inayokaribiana na hii ni "NOt easily broken", the same issues za marriage zinavyokuwa affected na kazi zetu hizi, wazazi etc.
Kama wewe ni mwanamke;
ni mwanamke mwenye hasira,
je marafiki zako wa kike ni wanawake wenye hasira
nini kinachofanyaga mahusiano yako kuharibika?
Ukisema au kujiona strong woman, huwa unamaanisha nini?
Kama wewe ni mwanaume;
Ulishawahi kuwa na mahusiano na mwanamke mwenye hasira?
na kama jibu ni ndiyo, hali hiyo ikufanya ujisikieje?
Je hali hiyo ilikufanya uchoke?
Na kwa wote
Mnasolve vipi matatizo ya kimahusiano yanapotokea?
Mwisho atakaeyeweza kuipata hii movie aiangalie, inasaidia kukufanyia self- analysis na kujua uliposimama. (najua kuna watu wameshaiona hii mpvie/documentary). Ingine yenye theme inayokaribiana na hii ni "NOt easily broken", the same issues za marriage zinavyokuwa affected na kazi zetu hizi, wazazi etc.