Hii kauli ya Magufuli "Polisi ueni Majambazi", imenitisha sana

Leo katika shughuli ya ufunguzi wa kituo cha kisasa cha mawasiliano cha polisi katika kukabiliana na uhalifu, Mh. Rais Magufuli amewaagiza polisi kwa msisitizo kuwa mnapowakamata majambazi wenye Silaha muwe mnawakamata haraka huku akisisitiza nadhani mnanielewa.

Mimi binafsi nimefurahishwa sana na agizo hilo maana majambazi yamezidi kiasi kwamba inatishia usalama wa nchi.
 
na polisi akimpokonya jambazi silaha.. asipelekwe mahakamani.. bali apandishwe cheo
 


Huo msisitizo alioutoa akamalizia NADHANI MMENIELEWA kwa mtizamo wa jicho la 3. Inaonyesha kuna makubaliano ya awali baina ya rais na hao polisi
 
Mods mtaniua kwa ban haki ya nani, mbona comment mliyoshikilia ni ya kawaida sana.
Muwe na huruma jamani!
Juzi tu nimemaliza ban, leo mkinipiga tena si balaa!
 
Mmmm, isije ikawa hao anaowaambia wakamate majambazi haraka wakawa ndio majambazi yenyewe!
 
Ngoja tusubiri watetezi wa haki za binadamu watuambie hata jambazi ana haki ya kuishi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…