Tua Ngoma
JF-Expert Member
- Apr 14, 2015
- 3,102
- 8,006
Katika hali ambayo haieleweki lengo lake ni nini,kumetokea kamatakamata ya wapinzani jijini Mbeya.
Juzi usiku aliyekuwa mwenyekiti wa BAVICHA Mbeya mjini aliandika kwenye group la chama Mbeya kuhusu oparesheni UKUTA. Jana jioni amekamatwa na hajulikani yupo Kituo gani hapa Mbeya japo taarifa zinadokezwa kuwa atasafirishwa kupelekwa Dar, juzi pia aliyekuwa katibu wa Moses naye amekamatwa.
Kuna kina mama walokomenti kuhusu operasheni UKUTA taarifa zilizopo wanatafutwa na polisi na wanaishi kwa kujificha mpaka saa hii, na cha ajabu zaidi simu ya Moses haipatikani ila WhatsApp anaonekana kuwa online.
Hivi hii kamatakamata ni kwa maslahi ya nani,nani anawatuma polisi?? Rais anajua kweli kinachoendelea kwa wananchi wake au polisi wanajiamulia tu?
Polisi mnapokamata watu hovyo namna hii mnajua mnachojenga mioyoni mwa ndugu,jamaa na rafiki zao?
Jamani tusifikishane huko, nchi haiwezi endelea kwa kuwekeana visa. Kama lengo letu ni kujenga nchi lazima tukemee huu uonezi, haiwezekani watu wazibwe midomo kwa njia za kikatili. Binadamu huchoka, tuchague kufuta vyama vingi au tuache watu wafanye siasa, tuache watu waongee.
Msije sema hatukuwahi onya haya mambo
Juzi usiku aliyekuwa mwenyekiti wa BAVICHA Mbeya mjini aliandika kwenye group la chama Mbeya kuhusu oparesheni UKUTA. Jana jioni amekamatwa na hajulikani yupo Kituo gani hapa Mbeya japo taarifa zinadokezwa kuwa atasafirishwa kupelekwa Dar, juzi pia aliyekuwa katibu wa Moses naye amekamatwa.
Kuna kina mama walokomenti kuhusu operasheni UKUTA taarifa zilizopo wanatafutwa na polisi na wanaishi kwa kujificha mpaka saa hii, na cha ajabu zaidi simu ya Moses haipatikani ila WhatsApp anaonekana kuwa online.
Hivi hii kamatakamata ni kwa maslahi ya nani,nani anawatuma polisi?? Rais anajua kweli kinachoendelea kwa wananchi wake au polisi wanajiamulia tu?
Polisi mnapokamata watu hovyo namna hii mnajua mnachojenga mioyoni mwa ndugu,jamaa na rafiki zao?
Jamani tusifikishane huko, nchi haiwezi endelea kwa kuwekeana visa. Kama lengo letu ni kujenga nchi lazima tukemee huu uonezi, haiwezekani watu wazibwe midomo kwa njia za kikatili. Binadamu huchoka, tuchague kufuta vyama vingi au tuache watu wafanye siasa, tuache watu waongee.
Msije sema hatukuwahi onya haya mambo