Hii inapendeza sana kwa wapenzi

Hata wanaume wamekuwa waoga sana na hawajiamini kabisaa ndio maana unaona %kubwa ya ndoa wanaume ndio wako juu kielimu/kiuchumi. Hii inamfanya ajifeel safe na mwenye mamlaka ndani ya nyumba.

Nimewahi shuhudia rafiki yangu(mwanaume) alimpenda binti aliyekuwa amemzidi kipato na elimu,na binti alikuwa mchakarikaji sana,binti pia alimpenda mnoo mshkaji na alijitahidi kumjali sana jamaa na kumsaidia hata alipokwama,alimheshimu ili asijifeel mnyonge. Ila jamaa alikuwa full kujistukia, akaamua kuachana na binti na kwenda kwa alokuwa amemzidi elimu na kipato. Nikamuuliza kwanini umemuacha binti? Jibu lake lilikuwa "kwakweli hajanikosea chochote na ni boonge la mwanamke ila siwezi kuwa nae kwakuwa kanizidi elimu/pesa".

Huko alikofikiri kunamfaa kulivurugika vibaya sana na kurudi ikawa too late maana yule binti mwingine alikuwa kishampata mwingine na walikuwa wako kwenye maandalizi ya ndoa.

Lakini pia niadmit kuwa wanawake tukishakuwa na kipato kikubwa au elimu kuna kakiburi fulani kanajengeka na kuona you can do anything bila mwanaume, "mwanaume kitu gani bwana"! Kumbe hatuwezi kupingana na nature maana no mater what bado tunahitajiana na kutegemeana,na ili hayo yawezekane lazima mmoja akubali kuwa chini ya mwenzie(mwanamke) ego ni mbaya sana na ndio inatucost wanawake wengi nowdays.

Unafiki nao umekuwa janga,hakuna genuine love watu tunapendana sababu ya vitu,ikitokea vitu havipo basi ndio mwisho wa huo upendo.
 
Hii inaleta shida sana. Unapenda na kujitoa kwa dhati, kumbe mwenzako kajiegesha tu.
Yaani usiombe hilo likukute,mtu anafanya short term plans kwenye long term plans zako.
 
Hii iko pande zote.
Ni kweli,mapenzi yamekuwa kizungumkuti. Lakini usikubali mtu akubadilishe ukawa worse kwakuwa tu kakuumiza, mwisho ukapishana na msr right wako.
 

Ebana mpendwa usemayo ni kweli asee wanaume nao tumekuwa na stereotype ya ajabu eti ukioa mwanamke unalingana nae au kukuzidi kipato na elimu ndoani atakusumbua pasipo hata kumchunguza kwanza huyo mwanamke kama kweli anaweza kuwa hicho kiburi unachokiogopa. Na hii imechangiwa na muamko wa kielimu kwa wanawake kwa miaka ya leo hii. Lakini huyo rafiki yako alikuwa ni bonge la kiazi(sorry kwa kukutukania rafiki)

Hizo paragraph zako mbili za mwisho zimemaliza mjadala sababu ndiko tulipokuwa tunaelekea... Ni ukweli usiopingika hatuwezi tukapingana na nature na kinachosababisha mvurugano wote kwenye mahusiano na hata wengi kukosa wengi ni kujaribu kupingana na nature hasa kwa wanawake, nature itabaki kama ilivyo mwanamke ni mali ya mwanaume lakini leo ni nadra kumkuta mwanamke msomi anaishi kwenye kauli hii tena kama ameolewa na mwanaume anamzidi kila kitu. Hii sio kwa waafrika tu hata wazungu ukweli huu wanaujua ila walichofanya kuuficha ni kuendekeza ndoa za mikataba. Nakazia kwa kusema kwamba hakuna ndoa yoyote iliyoimara kama mwanamke hatajishusha pale anapohitajika kujishusha period.
 
Sababu kubwa ya hili ni watu kutaka kuishi fake life, lakini wale ambao bado wanaishi kwenye reality wengi wao wana uvumilivu mkubwa tu.

Ni kweli. Uvumilivu umekuwa mdogo sana nyakati hizi.
 
Sababu kubwa ya hili ni watu kutaka kuishi fake life, lakini wale ambao bado wanaishi kwenye reality wengi wao wana uvumilivu mkubwa tu.
Hii ndiyo inaharibu sana. Wanaishi maisha yasiyokuwa yao.
 
Reactions: BAK
Dude even became chairman of Harvard Law Review, jmn he wasn't a nobody... Don get it twisted... He was somebody.. Miaka hio kusoma chuo tena Harvard afu blackii ilikua bongeee la dilii,
Ha ha kusoma Harvard walikuwa wanaangalia kichwa iliyotulia. Kama unapesa kichwani mnakitu unaishia kusikia tu kwenye santuli.
 
Hilo la kumuita "kiazi" walaa haujakosea ndivyo hata mimi nilimuita,na kumwambia atamkumbuka sana huyo binti,sadly mpaka sasa anajutia.

Nikagundua kuwa mwanaume akikosa pesa anakosa kujiamini pia,thats why huwa nahubiri wanaume kutafuta pesa,watu hunichukia lakini nawatafutia KUJIAMINI.

Kila maendeleo huja na faida na hasara zake,hivyo maendeleo ya hizi elimu hizo ndizo hasara zake. Mwisho yamekuwa ni mashindano,kuheshimiana,kupendana,kuchukuliana na kuvumiliana tena hakuna, kila mmoja anamuona mwenzie mbaya, wote tumekuwa familia ya kambale mama sharubu na baba sharubu .

Kuwa mbali na Mungu nayo inachangia hali hii,maana tukifuata maandaiko(kwa dini zote) sidhani kama tungekuwa na hizi tafrani. Teknolojia inatutawala badala ya sisi kuitawala.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…