sakapal
JF-Expert Member
- Apr 11, 2011
- 1,804
- 1,425
Habari yako wewe mama uliyefungua uzi huu kutaka kujua nini kilichojiri. Na wengine pia habari zenu :behindsofa: !!
Ni hivi msimu wa likizo na sikukuu ya kumaliza mwaka umewadia na muda huu mambo mengi huwa yanatokea kwenye familia. Wakati huu wa likizo wanafunzi walioko bording wanarudi majumbani na ndugui na jamaa wa vijijini wanataka kuja mjini kusalimia mjomba na shangazi. Wakati huohuo wakazi wa mjini wamepanga kwenda kula sikukuu kijijini ili watoto wale wanaosoma academy schools wajue walikotokea mababu zao. Basi mwezi huu unakuwa busy watu wakisafiri huku na kule wengine hata kusafiri nje ya nchi na familia nzima. Kutokana na purukushani hizi za hapa na pale matumizi huwa mengi na makubwa kwa mwezi wote huu wa 12 na hivyo mwezi unaoanza na mwaka mpya ada zinatakiwa kwa watoto kurudi mashuleni na hivyo matumizi kuendelea, nimeona mama kama msimamizi wa familia anawajibu wa kuhakikisha yafuatayo,
ANGALIZO: SI LAZIMA KUKARIBISHA WAGENI AMBAO HUTAWEZA KUWAHUDUMUA USIJEAIBIKA.
Huu ni mtazamo wangu, nmawe weka wa kwako kwa msimu huu wa sikukuu na likizo ambapo dunia nzima iko kwenye kusheherekea. Najua wajibu wa wababa pia upo ruksa kuwakumbusha wakina baba nini wanatakiwa kufanya msimu huu.
Nawakilisha.
Ni hivi msimu wa likizo na sikukuu ya kumaliza mwaka umewadia na muda huu mambo mengi huwa yanatokea kwenye familia. Wakati huu wa likizo wanafunzi walioko bording wanarudi majumbani na ndugui na jamaa wa vijijini wanataka kuja mjini kusalimia mjomba na shangazi. Wakati huohuo wakazi wa mjini wamepanga kwenda kula sikukuu kijijini ili watoto wale wanaosoma academy schools wajue walikotokea mababu zao. Basi mwezi huu unakuwa busy watu wakisafiri huku na kule wengine hata kusafiri nje ya nchi na familia nzima. Kutokana na purukushani hizi za hapa na pale matumizi huwa mengi na makubwa kwa mwezi wote huu wa 12 na hivyo mwezi unaoanza na mwaka mpya ada zinatakiwa kwa watoto kurudi mashuleni na hivyo matumizi kuendelea, nimeona mama kama msimamizi wa familia anawajibu wa kuhakikisha yafuatayo,
- Chakula kinakuwepo kwa msimu wote huu wa likizo hadi kufikia mwaka mpya.
- Kujua idadi ya watu wanaolala nyumbani kwake au kujua wageni atakaowapokea kipindi hiki
- Kuhakikisha watu wote walio nyumbani kwake wanakula na kupata mahali pa kulala
- Kama kunasafari ya familia hakikisha unabook ticket mapema au kuhakikisha usafiri mtakao tumia wakati wa kusafiri uko salama na wa uhakika
- Kuzingatia usafi maana kipindupindu huwa kinaanza msimu huu wa mwisho wa mwaka ambapo matunda ni mengi.
- Mama punguza matumizi yote ambayo siyo ya lazima kwa familia yako
- Kila hela unayopata mwezi huu weka asilimia 5 kama akiba ya mwakani kama si asilimia 10
- Hakikisha ada za watoto january ziko kibindoni kabla hamjaanza kusheherekea sikukuu za mwisho wa mwaka
- Kufurahia msimu huu wa likizo pamoja na watoto wako na mumeo na ndugu zako wa karibu.
ANGALIZO: SI LAZIMA KUKARIBISHA WAGENI AMBAO HUTAWEZA KUWAHUDUMUA USIJEAIBIKA.
Huu ni mtazamo wangu, nmawe weka wa kwako kwa msimu huu wa sikukuu na likizo ambapo dunia nzima iko kwenye kusheherekea. Najua wajibu wa wababa pia upo ruksa kuwakumbusha wakina baba nini wanatakiwa kufanya msimu huu.
Nawakilisha.