ni kweli lowassa hajajipanga
Nikiona hivi naona CCM ovyo sana.. bado nikigeuka huku kwingine EL ambavyo hajajipanga napata homa kabisa... Pande zote mbili zina disadvantages za hatari
hajajipanga kivipi mkuu?
alijipanga kuwa raisi kwa tiketi ya ccm kugeuza maneno na ajenda kazi sana mkuu hasa kwa cheo cha uraisi na ndio maana kama unasikiliza vizuri ajenda zao zinalandana na hazina mashiko
Hizi AJENDA, SERA na sijui nini ni UPUUZI mtupu. Nikisikia tu napata kichefuchefu.
CCM kila baada ya miaka 5 wanakuja na Sera na Ajenda zako unazozitaka nzuri tu na wanakuwa wamejipanga kwelikweli washinde ila wakishashinda, wanaifanya Kigoma kuwa Dubai.
Nafikiri ni muda ufike sasa tumpe ambaye hajajipanga na wala hana AJENDA.
Ajenda yake iwe moja tu, MAISHA BORA KWA WATANZANIA. Mengine Watanzania hawajali atafanyaje.