Katavi
Platinum Member
- Aug 31, 2009
- 41,983
- 12,701
Nipo kwenye daladala kuna mama anaongea na simu. Inaonyesha kazaa na wanaume watatu tofauti na huyu mwanaume wa mwisho inaonekana hatoi matunzo kwa mtoto wake. Sasa katika maongezi ya simu huyo mwanaume anaporomoshewa matusi ya nguoni hadi abiria wengine, hasa wa kiume tumeinamisha vichwa vyetu kwa aibu. Sentensi moja aliyoongea na nimevutiwa nayo ni hii:-
"we ni mwanaume gani ambae hujali mtoto, WANAUME wote niliozaa nao wanajali watoto wao, wa kwanza kamsomesha mwanae hivi sasa yupo form two, wa pili nae anamsomesha na anatoa matunzo na mtoto yupo darasa la sita, Ms.....(tusi) wewe mtoto wako hata chekechea unashindwa kumpeleka"
Akamaliza kwa kusema "Najuta kuzaa na wewe".
"we ni mwanaume gani ambae hujali mtoto, WANAUME wote niliozaa nao wanajali watoto wao, wa kwanza kamsomesha mwanae hivi sasa yupo form two, wa pili nae anamsomesha na anatoa matunzo na mtoto yupo darasa la sita, Ms.....(tusi) wewe mtoto wako hata chekechea unashindwa kumpeleka"
Akamaliza kwa kusema "Najuta kuzaa na wewe".