Lakini hapo ndipo Ujinga wetu Waafrika ulipo, kwa maana hapa ukiangalia Kiafrikaans ni lugha ya Wazungu Makaburu unaweza hata kukiita Kiholanzi na Wazungu hawa hawataki kuiacha lugha yao na kuchukuwa English ingawaje wewe unasema ni lugha ya Dunia lkn Mwafrika mweusi anapigania na yuko tayari kuharibu Miundo mbinu ya Chuo Kikuu iliyojengwa kwa fedha nyingi ili Kiingereza kifundishwe!
Sasa ni kwa nini Mzungu anapigania Kiafrikaans chake tena ndani ya Afrika lkn Mwafrika mweusi yuko tayari kufa kupigania Kiingereza na siyo Kizulu chake?
Kumbuka Wazungu (ukiondoa machotara/coloreds) wanaoongea Kiafrikaans kama lugha yao asili hawazidi milioni 2 wkt Kizulu kinaongewa na Watu milioni 11 au asilimia 22 (22%) ya wananchi wa AK, sasa kwa nini nguvu zao Waafrika weusi wasizielekeze hapa kwenye Kizulu badala ya Kiingereza?
Mkuu wale wameathirika na ukabila bora lugha ya malkia tuSawa nakuelewa lkn tupa kule ulete nini? Hicho ndiyo kitu ambacho nashindwa kukielewa!
Hata mimi napenda kukitupa Kiafrikaans kwa maana ni lugha ya kigeni lkn unapopigania kutupa Kiafrikaans lugha ya Kizungu na kutaka kuleta Kiingereza sasa ndiyo umefanya nini?
Mimi ningependa wapiganie kutupa Kiafrikaans na kuleta Kizulu, hapo ndipo Mwafrika ataheshimika kwani Dunia nzima binadamu wote hupigania lugha zao na Afrika kwetu tu tena siyo Afrika yote bali sisi weusi kwa maana hata Somalia na Ethiopia wanapigania Lugha zao ni sisi Wabantu ndiyo tunapigania kuwa na lugha ya kigeni yaani tuko tayari kufa, kuumizwa na Askari kwa ajili ya kupigania Kiingereza!
Ukombozi upi kijana??????siye watanganyika tulichokifanya hiyo miaka ya 60 ni kubadili white exploiters(colonialist) master to black exploiters tu and not otherwise......Mkuu...tanzania tulishapata ukombozi...ama kweli Benja hakukosea alivyowaita malofa na wapumbavu
Apartheid si neno tu bali ni mfumo wa kibaguzi uliopewa jina hilo. Mfumo huo haukuanzishwa na waingereza na ndiyo maana kuna wakati maalum wa kuanza na kumalizika, kuwa ni kuanzia mwaka 1948 hadi mwaka 1994. Unajua ni kwa nini wanasema ulianza mwaka 1948?
Nikweli kabisa, ni sawa na vile sultan alitawala Zanzibar kwa niaba ya uingerezaHaswa, Waingereza ndiyo Marchitect wa Ubaguzi wa rangi AK, neno Apartheid maana yake ndiyo hiyo ubaguzi wa watu kulingana na asili yao, na Waanzilishi ni Waingereza na siyo waanzilishi tu bali hata walioipa support Apartheid mpaka dakika ya mwisho ni Waingereza chini ya Churchil na Margaret Thatcher!
Walichofanya makaburu ni kuendeleza tu mfumo lkn uliasisiwa na Waingereza na hata walioufanya udumu mpaka miaka 90' ni Waingereza hao hao, wao ndiyo waliokuwa wanwakingia kifua makaburu miaka yoote!
Issue sio Rhodes alikufa mwaka gani, atuzungumzii mtu,tunazungumzia mfumo, ambapo Uingereza ndio sponsorAcha blah blah zako wewe, "Apartheid" imeanza mwaka 1948 hadi 1994 wakait Cecil Rhodes alikufa mwaka 1902. Kama kila ubaguzi unauita "Apartheid" basi hata Ubaguzi unaoendelea huko Marekani kwa Wazungu kuwabagua waafrika wewe na mfanano wako na yule "Kibajaji" wenu basi uite ubaguzi huo 'Apartheid" kama watu wenye kujua watakuelewa!
Kiingereza ni lugha ya dunia.Binafsi sielewi na bado sijawahi kuielewa reasoning yetu Waafrika hata siku moja. Huko nchini AK kumezuka fujo kubwa iliyopelekea wanafunzi kuchoma na kuharibu Miundo mbinu ya Chuo Kikuu wanachosomea, sasa kisa ni nini?
Ni kwamba Wanafunzi Waafrika (weusi) hawataki kufundishwa kwa lugha ya Kiafrikaans ambayo ni lugha rasmi ya Makaburu wanasema kwamba ni lugha ya Kikoloni na ya ukandamizaji na wanataka Vyuo vyao vifundishwe kwa kutumia Kiingereza, hapo ndipo nilipochoka ningeelewa kama wangegoma kufundishwa Kiafrikans na kutaka wafundishwe Kizulu, Xhosa , Kitwsana au hata Kiswahili kama shida ni lugha ya Kikoloni lkn wanataka Kiingereza sasa Kiingereza ni lugha ya nani?
Unakataaje Kiafrikaans kwa kigezo kwamba ya Kikoloni halafu unataka Kiingereza?
Inanikumbusha Raisi Kagame wa Rwanda alipoondoa Kifaransa kama Lugha ya Taifa na kuweka Kiingereza kwa nini asingeweka Kirundi/Kinyarwanda? Au Raisi Mugabe wa Zimbambwe anatukana Wazungu na kuwakebehi lkn kwa Kiingereza na nchi yake anatumia Kiingereza kwa nini siyo Kishona?
Kwa mambo kama haya Waafrika hatuwezi kuheshika Duniani kamwe kwani watu wa nje wanatuona hatuna akili, Dunia nzima binadamu hufanya Mapinduzi na kuweka lugha zao sasa tuko tayari kuharibu Miundo mbinu yetu kupigania Kiingereza, sasa Kiingereza kina tofauti gani na Kiafrikaans? Zote si ni lugha za Kikoloni pia!
Hata hapa nyumbani watu wengi wanaona na kuamini kwamba Kiswahili chetu ndiyo adui wa Maendeleo yetu nina uhakika ukifanya kura ya maoni ya kama Kiswahili kifutwe TanZania na kuwekwa Kiingereza au Kifaransa au hata Kireno zaidi ya asilimia 60 wataataka Kiswahili chetu kifutwe, na kama siyo kuwa Sera ya CCM Kiswahili kingekuwa kimeshafutwa kwani kwenye manifesto ya chadema walikwishakiondoa na kubakia somo tu!
Hii ni Afrika kwetu tu hakuna sehemu nyingine Duniani kuna binadamu wa aina kama yetu!
Hata Afrika Kaskazini hawako hivyo Gadafi mpaka anakufa anaongea Lugha yake!
Chini ni Uharibifu uliofanywa na Wanafunzi kwa kuchoma majengo ya Chuo chao kupinga Kiafrikaans na kutaka Kiingereza!
SABC News - UP student’s Afrikaans protest grows:Friday 19 February 2016
Ni wewe siyo mimi anayepaswa kusoma Historia. Ubaguzi upo wa aina nyingi. Kwa mfano kilichotokea Afrika Kusini Mwaka juzi na kinachotokea huko Ujerumani hivi sasa ni ubaguzi lakini hauitwi "Apartheid" bali "Xenophobia" na kihistoria makaburu hawazaliwi na Waingereza bali wanazaliwa na wadachi!!Ndiyo maana nimekwambia jaribu kwanza kujisomea Historia ili uelewe haya mambo na uache kulishwa!
3/4 ya watu wa SA..wanaongea lugha ya kiingereza..sasa linapokuja suala la kuwaforce wajifunze ki Afrikaans..inamaana unawakumpusha machungu ya nyuma..kwanza hiyo lugha ukiiangalia kwa umakini inakuwa sawa tu na lugha za kizulu,khosa na vikabila vingine vidogo..kwa nini ipaishwe hivyo na sio kizulu au khosa??kwanini wasitumie kiingereza ambayo ni international language..yenye faida luluki kuliko hiyo ya afrikaans ambayo ni local language!Kiingereza ni lugha ya dunia.
Ni wewe siyo mimi anayepaswa kusoma Historia. Ubaguzi upo wa aina nyingi. Kwa mfano kilichotokea Afrika Kusini Mwaka juzi na kinachotokea huko Ujerumani hivi sasa ni ubaguzi lakini hauitwi "Apartheid" bali "Xenophobia" na kihistoria makaburu hawazaliwi na Waingereza bali wanazaliwa na wadachi!!
Kusema kwamba Apartheid imeanzishwa na Waingereza ni utungaji usio na maana. Apartheid ulifanyika kuwa Mfumo pale sheria ya kuwaweka watu wa Afrika Kusini katika madaraja kwa kuzingatia Rangi zao na kuweka maeneo rasmi kwa ajili ya watu kwa kulingana na rangi zao.
Unawashauri wengine wakati kwenu lugha ya Universities ni hiyo hiyo English!Sawa nakuelewa lkn tupa kule ulete nini? Hicho ndiyo kitu ambacho nashindwa kukielewa!
Hata mimi napenda kukitupa Kiafrikaans kwa maana ni lugha ya kigeni lkn unapopigania kutupa Kiafrikaans lugha ya Kizungu na kutaka kuleta Kiingereza sasa ndiyo umefanya nini?
Mimi ningependa wapiganie kutupa Kiafrikaans na kuleta Kizulu, hapo ndipo Mwafrika ataheshimika kwani Dunia nzima binadamu wote hupigania lugha zao na Afrika kwetu tu tena siyo Afrika yote bali sisi weusi kwa maana hata Somalia na Ethiopia wanapigania Lugha zao ni sisi Wabantu ndiyo tunapigania kuwa na lugha ya kigeni yaani tuko tayari kufa, kuumizwa na Askari kwa ajili ya kupigania Kiingereza!
Ndugu yangu "Pass Law" na "Apartheid" ni vitu viwili tofauti kabisa!! Pass law hata hapa kwetu Tanzania zilikuwepo na madaraja pia yalikuwepo, watu walikuwa wanajua Bar za wazungu ziko wapi na za kwao waswahili ziko wapi, na hata Mwalimu Nyerere aliwahi kukataliwa kuuziwa bia kwenye baa iliyokuwa maalum kwa wazungu. Pia kulikuwa na maeneo ya wazungu wahindi na Waafrika, na ndiyo maana maneno kama "Uswahilini" "Uzunguni" na "Uhindini" yaliibuka. Lakini huwezi kuuita huo mfumo kwamba ni Apartheid ingawa ni Ubaguzi.pass law,partheid!
Ndugu yangu "Pass Law" na "Apartheid" ni vitu viwili tofauti kabisa!! Pass law hata hapa kwetu Tanzania zilikuwepo na madaraja pia yalikuwepo, watu walikuwa wanajua Bar za wazungu na hata Mwalimu Nyerere aliwahi kukataliwa kuuziwa bia kwenye baa iliyokuwa maalum kwa wazungu. Pia kulikuwa na maeneo ya wazungu wahindi na Waafrika, na ndiyo maana maneno kama "Uswahilini" "Uzunguni" na "Uhindini" yaliibuka. Lakini huwezi kuuita huo mfumo kwamba ni Apartheid ingawa ni Ubaguzi.
Inawezekana Pass Law ikawa ni kiashiria cha ubaguzi, lakini kunawezekana kusiwe na Pass Law na bado Apartheid ikawepo. Boston kwenye ule mgomo mkubwa wa wakazi wa mji ule uliotokana na kupinga madaraja kwenye Magari ya usafiri ambayo yalimbagua Mwafrika, lakini kulikuwa hakuna Apartheid!!