Hichi ndicho kitafanya nimuache mke wangu

Hichi ndicho kitafanya nimuache mke wangu

Kabla ya Kulalamika Jitafakari kwanza Wewe Mwenyewe, Je unatimiza wajibu wako kwake kikamilifu kama mume?

Sisi wanaume tu wepesi wa kulaumu kabla ya Kujitafakari kwanza sisi wenyewe.
 
Mbona hayo madogo yanarekebishika mkuu ebu pamabna kaa nae chin umueleze ataelewa tu acha kulia lia ww mtot wa kiume
 
Husika na kichwa cha habari hapo juu.Hii sio story ni mambo ambayo yanaendelea katika nyumba yangu kwa kweli niliowa kwa leo kwa kutegemea kuna vitu nitavikuta katika ndoa lkn imekuwa ni kinyume na matarajio yangu
1. Dharau
Yani siku nikinunua mboga ambayo haipendi lazima ataitupa au kuzila na hatopika na maneno ya kashfa hii haangalii tuko wapi.
2. Wivu uliopitiliza
Natoka alfajiri kwenda job narudi jioni kabisa kichwa kimechoka natarajia kutulizwa na kupewa pole ila ilo zogo home utatamani urudi job ila ndio washafunga.
3. Uaminifu
Yani inafika stage nikirudi kazini nivuliwa nguo nasuswa kama sijachepuka
Nikienda kwa rafiki nikirudi lazima ipigwe simu kujua kama nilikuwa hoko

Swali hivi ndoa ndio ziko hivi zote?
Kuna umuhimu gani wa kuwa kwenye ndoa na wakati humwamini mwenzio hata 1%!
Kibaya zaidi ukimkanya tu ananuna anenda beach. Alafu tuko nchi xa watu kwa kweli namrudisha.
Am out namuacha kwa kweli this is too much.
[emoji125] mm mbiooooo
Ukimuacha njoo kwangu raha siku 365 na robo
 
Hata kama ni dhalau "not no that extent"
pole ongea na mama yake atamchambaaa atanyooka
 
Baya hapo ni moja, hilo namba moja,
Dharau tafsiri yake hakubali kuongozwa na wewe na hawezi kuwa mtii,ni km vile serikali ambayo watu hawamkubali rais wao kinachofuata ni mapinduzi, ili nyumba iendelee lazima kiongozi akubaliwe na anaowaongoza,km hilo halipo tegemea lolote muda Wowote,dharau ndo mama wa uharibifu ktk ndoa, omba MUNGU ambadirishe vinginevyo kaa tayari
 
Kuna sehem pesa unapereka bila kumpa taarifa kama mwenza wako, jitazame kabla hujatazama.
 
Ulichukua hatua gani kurekebisha haya mambo uliyotueleza? Kumbuka hakuna binadamu aliyekamilika labda kama unampango wa kuwa baba paroko.
Kuna kutokamilika na kuna makusudi, yupo mambo mwanamke akikosa hafai kuwa mke,yapo mambo pia mwanaume akiyakosa hafai kuwa mume,
Mwanamke Mwenye dharau inamaana hana utii na hatambui uongozi wa mume, Sasa unakaaje na mtu asiyekutambua km kiongozi na mlinzi wa Familia, kukosa utii si tabia ya kimaumbile kiasi useme Hakuna alokamilika,hii ni kusudi, MUNGU hakuumba dharau ndani ya mwanamke, aliumba utii
 
Ulifikiri kuoa mteremko? Hilo ndilo jaribu la mume halisi unapigana unashinda wala ndoa haivunjiki na mke unambadili ananyoosha njia. Acha kulialia "be a man" na hapo hujapigwa makofi...ukimgusa yeye mke anakuwa na presha ghafla ya kulazwa ndiyo urapata akili. Tatua tatizo usikimbie mwanamume
Acheni kumsingizia Mungu,dharau ni jaribu?,ipo tofauti ya jaribu, pig na ufisadi, dharau ni ufisadi ndani ya ndoa, MUNGU hakuumba dharau ndani ya mke,aliumba utii, dharau ni makusudi, dharau ni gugu ndani ya ndoa, utamuongozaje mtu anaekudharau, hebu lifikirie neno dharau Kwa mapana
 
Siri ya mafanikio katika mahusiano yeyote ni mawasiliano mazuri, ukirudi nyumbani piga wa lazima uongee na mpenzi wako kuhusu yale unayoona yanakukera na mkimaliza mnasindikizia maongezi na tendo.
Lakini pia haya ni matokeo ya kuingia katika ndoa either kwa sababu ilikuwa ni lazima ili upate faida au kufanikisha jambo flani ama kuingia ktk ndoa kwa haraka kabla hamjajuana vema kuhofia mmoja wapo kuporwa na muoaji/muolewaji mwingine!

Kama mlikaa kwa muda wa kutosha ktk uchumba haya ni nadra sana kutokea, zipo changamoto za ndoa lakini za aina ya kisa hiki zinafungamanishwa na sababu nilizozitaja hapo juu!
 
Back
Top Bottom