Hichi ndicho kitafanya nimuache mke wangu

Hichi ndicho kitafanya nimuache mke wangu

Mi katika yote hayo naona hilo la kwanza ndio baya...hayo mengine mwache tu,kama anakagua we mwachie tu si yake bwana! Ila siku ukimfumania hakuna kuombana msamaha....
 
Baya hapo ni moja, hilo namba moja,
Dharau tafsiri yake hakubali kuongozwa na wewe na hawezi kuwa mtii,ni km vile serikali ambayo watu hawamkubali rais wao kinachofuata ni mapinduzi, ili nyumba iendelee lazima kiongozi akubaliwe na anaowaongoza,km hilo halipo tegemea lolote muda Wowote,dharau ndo mama wa uharibifu ktk ndoa, omba MUNGU ambadirishe vinginevyo kaa tayari
Hakuna kitu kinaboa kama mwanamke mwenye dharau. Kila ufanyalo hata liwe zuri kiasi gani ataweka ngumu tu. Inaumiza mno hasa kwa sie ME tunaojiheshimu.
 
Ndio maana ili ufaulu darasani unapewa mitihani lakin kwenye ndoa ni tofauti unapewa cheti cha kufaulu, mitihani utaikuta nyumbani
 
Tena Kwa taarifa yenu wanawake wakiwa wadogo huwa na heshima Sana maana anakuogopa wakiwa wakubwa huwa wanatuchukulia poa sana
Hili nakataa mkuu, mwanamke kuheshimu sio umri tu kuna mambo mengi sana nyuma ya pazia. Binafsi naona kuna makundi mawili makuu ya wanawake katika minajili ya heshima ndoani.

Kuna mwanamke anayekuheshimu kama unachangia pakubwa katika ustawi wa maisha yake. Mf. hana chanzo cha kipato, so ni lazima atakuvumilia mapungufu yako na atakuwa na adabu maana hana ujanja nawe ndio unamuweka mjini. Huyu heshima ni kwa sababu ila siku akijiweza utamtambua.Hii inajumuisha wale wanafiki waviziaji wa ndoa, wakiipata tu umekwisha. Team maslahi hawa na ndio type ya wanawake wengi wa kileo.

Kuna wengine ambao heshima imetokana na malezi ya nyumbani, wako so humble regardless ya wanacho au hawana. Wanatambua kumfanyia mtu dharau ni moja ya tabia mbaya na si ustaarabu toka wanakuwa. Huyu ukimpata dunia yote itakuwa yako na wengi si wavivu katika kujitoa kupenda kwa dhati.Hawa wengi ni old school na nadra kupatikana.

Kutokana na ongezeko la wanawake wasumbufu katika ndoa naona tatizo kubwa limekuwa ni sisi ME kutaka kuendesha nyumba kidemokrasia. Kushindwa kabisa kuwa na msimamo ni sumu mbaya sana na muarobaini wa tatizo hilo ni kidume kukaza tu. Kulia lia hakutasaidia kamwe na hakumfanyi KE kukuonea huruma. Kama utamtendea mtu wema halafu asijali lolote nawe onesha kutojali fanya mambo yako achana na habari za kumfuatilia na ujinga wake. Inaweza ikaonekana kama ajabu ila dawa ni kutoa ultimatum tu. Mwanamke huchelewa kuelewa kama anafanya upumbavu mpaka limkute akachekwe na ulimwengu. KE ni wa kuongozwa siku zote toka mwanzo.
 
Husika na kichwa cha habari hapo juu.Hii sio story ni mambo ambayo yanaendelea katika nyumba yangu kwa kweli niliowa kwa leo kwa kutegemea kuna vitu nitavikuta katika ndoa lkn imekuwa ni kinyume na matarajio yangu
1. Dharau
Yani siku nikinunua mboga ambayo haipendi lazima ataitupa au kuzila na hatopika na maneno ya kashfa hii haangalii tuko wapi.
2. Wivu uliopitiliza
Natoka alfajiri kwenda job narudi jioni kabisa kichwa kimechoka natarajia kutulizwa na kupewa pole ila ilo zogo home utatamani urudi job ila ndio washafunga.
3. Uaminifu
Yani inafika stage nikirudi kazini nivuliwa nguo nasuswa kama sijachepuka
Nikienda kwa rafiki nikirudi lazima ipigwe simu kujua kama nilikuwa hoko

Swali hivi ndoa ndio ziko hivi zote?
Kuna umuhimu gani wa kuwa kwenye ndoa na wakati humwamini mwenzio hata 1%!
Kibaya zaidi ukimkanya tu ananuna anenda beach. Alafu tuko nchi xa watu kwa kweli namrudisha.
Am out namuacha kwa kweli this is too much.
[emoji125] mm mbiooooo
Hujui Kama unapendwa lakini siku ukijua utakuwa umechelewa,anakunusa maana unamkuna vizuri,kuzira akizira we mpige miti tu!
 
Weeeeeeeee cheusi weweee
Mi naimba tu jamani, mtuchagueeee na kutuchambuaaa kama nyanya sokoni alafu bado tena mnung'unike!! Ifikie hatua tukubaliane na uhalisia kuwa hakuna binadamu mkamilifu, kila mmoja ana mapungufu yake. Hivyo basi badala ya kulaa tunahesabiana makosa tuuu hebu tuhesabu na mazuri ya wenzetu. Then hayo madhaifu mrekebishane taratibu huku mkiombeana kwa Mungu.
 
Tena Kwa taarifa yenu wanawake wakiwa wadogo huwa na heshima Sana maana anakuogopa wakiwa wakubwa huwa wanatuchukulia poa sana
[emoji3] [emoji3] [emoji3] [emoji3] [emoji3]
Sio anakuchukulia poa, anakuwa ashakomaa kwahiyo kukujua ni dakika tu.
 
Hayo ya kwako na madogo kuliko tunayopitia cc wenzio,ndoa yako ina muda gani kama ni changa hayo mambo ni yakawaida.jitahidi kumwambia nn unataka na usichopenda pia.mi mwenzio yalikuta kama hayo kuchunguza kwa makini nikagundua ana rafiki anayemshawishi nikamrekebisha hadi sasa tuna miaka 9 ndani ya ndoa na watoto wa2.
 
Kuna unalofanya ambalo lamfanya asiwe na Imani nawe, suala la dharau ni kuambizana tu yanarekebishika mkuu!!
Wivu kwenye mapenzi lazima uwepo tuu kama hamna wivu jua hupendwi!!
Kaeni chini myazungumze bwanaa
Wivu ganu huo wa kutupa mboga.
 
Back
Top Bottom