Heshima ya kipekee sana iwafikie Wanaume

Heshima ya kipekee sana iwafikie Wanaume

Carleen

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2018
Posts
8,407
Reaction score
28,839
Hi guys.

Naomba hizi baraka za dhati ziwafikie WANAUME, Hasa wale wanaume wanaosimamia na kutekeleza majukumu yao ipasavyo.

Nakumbuka muda mfupi uliopita I passed through a very rough road to hell. Kuna zile nyakati kwenye maisha unatamani kabisa kama ujikane nafsi, yote yanayokusibu yawe tu ni kama ndoto mbaya, unatamani uamke asubuhi uone like everything is real okaaaay, but that's next to never sababu hard times ndiyo zinaleta maana khalisi ya maisha.

Nakumbuka nililia na kulia mpaka machozi yakakauka, lakini chozi langu, halikubadili hata chembe ya ugumu wa mlima ule, na wakati nalia lile 'tatizo' liko palepale tena 'limekunja nne na kuchezesha mguu mmoja, linakuambia kabisa Carleen wewe lia tu, ukimaliza just come and face the reality'

Nilikuwa kwenye nafasi nzuri kabisa ya kukubali kuwa nimeshindwa, jamii ingenielewa sababu ningejificha kwenye mwamvuli wa 'uanamke', wangesema tu 'she's just a lady, amepambana lakini imeshindikana', lakini sikutaka kuruhusu wala kukubali that comfort zone, I said to myself sintokubali kuwa defeated, the word 'FAILURE ain't on my dictionary'

Mwisho wa siku Mungu alinionekania, alinisimamia kiume, and I passed through that challenge, Akanifanikishia kibabe sana

Wakati napitia that hard situation, nikawaza nafasi waliyonayo 'Wanaume', ambao hakuna namna jamii ama familia yake ingemuelewa kwamba kashindwa, yaani kashindwa? Kashindwaje? Tumejengewa kuamini they're like 'Undefeated Robots'..! Hakuna namna wataeleweka wasipotatua changamoto iliyopo mbele yao, na zaidi sana mwanaume utaishia kudharaulika na kuonekana mzembe, Man..! you're passing through hell of shi**s.

Na mbaya zaidi tunawabebesha mizigo mikubwa mikubwa ya matatizo bila kusahau 'misalaba mizito ya majukumu waibebe hadi Golgotha', na hatutegemei excuse yoyote kutoka kwao, kila tatizo walitatue haijalishi situation wako nayo ama ugumu uliopo, tunachojali tu ni solution imepatikana na maisha yanaenda.!! Huwa hatutaki kujua imekuwaje na wamewezaje, na mbaya zaidi tunaweza hata kuwaongezea tatizo lingine tena kwa juu walitatue, tunajua tu si 'Mwanaume bwana, atapambana tu'.

MEN, May God Bless you abundantly, you're real true heroes..! Hizi baraka kutoka ndani ya moyo wangu, ziwafikie wababa bora wote wanaopigana na (watakaopigana) kwa ajili ya familia zao, you're doing a very remarkable great job.

Blesses.
 
Uuuwiiii Uuuwiiii Uuuwiiii Uuuwiiii Uuuwiiii Uuuwiiii Uuuwiiii Uuuwiiii Uuuwiiii Uuuwiiii Uuuwiiii Uuuwiiii Uuuwiiii Uuuwiiii Uuuwiiii Uuuwiiii Uuuwiiii Uuuwiiii Uuuwiiii Uuuwiiii

Sent by IPhone
 
Ok
tapatalk_1589631556042.jpeg


Sent by IPhone
 
Kuna wanaume kweli wanapambana wanapopitia magumu, kuna wakati ukimuona magumu anayoyapitia unahisi hapa hatatoboa, unaona kabisa kanyonyoka hadi nywele kwa jinsi kichwa kinavyofanya kazi kufikiri na kutekeleza kile kilicho mbele yake. Lakini mwisho wa siku anatoboa.

Pole mamie, huwa ni kipindi tu cha mpito.
 
Oooh yeah!!
Ila mafurushi hawahusiki hapa.

Hawa viumbe(wanaojitambua) wana nafasi kubwa sana kwenye maisha yetu, Mungu awatunze tu kwaajili yetu. They go through alot na tumewaminisha kuwa lazima wapambane no matter what(ofcoz ni lazima jamani) hivyo masahibu yao wanakufa nayo "kiume".

Ila endeleeni tu kupambana jamani maana hamna namna, tupo kuwafariji.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom