Heshima na Hongera SUNRISE RADIO FM Arusha

MVUMBUZI

JF-Expert Member
Jan 8, 2011
5,182
2,304
Jana wakati wananchi wa Arusha na vitongoji vyake wanasubiri kwa hamu matokeo ya uchaguzi wa jimbo la Arumeru Mashariki ni kituo cha SUNRISE RADIO FM kilifanya kazi kilichopaswa kufanya kama chombo huru cha habari. Ni kituo hiki tu kilichoamua kuchukua jukumu la kurusha matangazo ya siku nzima bila kuchenga kutuhabarisha hatua kwa hatua kila kilichokuwa kinaendelea kule Arumeru Mashariki. Again ni kituo hiki kupitia watangazaji wake mahiri waliokuwa kila kona ya Arumeru leo asubuhi waliotangaza LIVE matokeo ya uchaguzi wa jimbo la Arumeru ambapo kijana mpiganaji na kamanda Nassari aliibuka kidedea.

Naomba nichukue fursa hii kwa niaba ya wasikilizaji na wananchi wengi wa Arusha mjini na vitongoji vyake kuushukuru na kupongeza uongozi na watangazaji woote wa kituo hiki kwa kuonyesha uzalendo usiopimika licha ya hujuma za kukatiwa umeme na TANESCO.

Uoga na ushabiki kwa CCM ulioonyeshwa na vituo vingi vya habari na kushindwa kuripoti ukweli kuhusu yaliyokuwa yakitokea nachukulia kama acid inayowamaliza wenyewe na ni wakati sasa wa ku-assess position zao kwa wananchi upya kabisa. Sunrise redio Arusha tunawapongeza na kuwatakia mafanikio mema naamini PAMOJA TUNASONGA MBELE KULETA MABADILIKO BILA UNAFIKI. CHEERS WOOOTE STUDIO
 
Yaaap, watu wenye matangazo ya biashara huko A Town hii ndio radio ya kufanya nayo biashara kwani inawafikia wananchi bili upendeleo wala woga
 
hao ndio makamanda wa ukweli! Mwaka huu SUNRISE RADIO watapewa tuzo ya matangazo mazuri ktk nyanja za siasa na uhuru na ukweli wa mambo yalivyo! People's poweeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
hao ndio makamanda wa ukweli! Mwaka huu SUNRISE RADIO watapewa tuzo ya matangazo mazuri ktk nyanja za siasa na uhuru na ukweli wa mambo yalivyo! People's poweeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee!!!!!!!!!!!!!!!!!

Siipigii Chepuo ya bure ila ukweli wa mambo mimi ni msikilizaji ambaye nimeanza kuisikiliza jana tu na mpaka usiku hawakuboa na ilikuwa kana kwamba niko eneo la tukio yaani Usa River.
 
Nawapa hongera ya nguvu sana Makamanda mmenikuna.Ntawatafuta angalau mpate juice moja moja.
 
sasa nimeamini kwaba ile dhana ya kuwatisha wananchi kwamba wasipoichagua ccm kutatokea fujo si kweli hata 2015 changes to the highest level may happen if cdm will bring a wise man siyo yale ya mgombea mwenza anakuwa std 7 this tym viongozi jipangeni vizuri.
 
Hakika Radio ya Sunrise ndio radio ya Ukweli hapa Arusha. Hii ndio kazi ya Radio. Hongera sana Sunrise FM
 
Inapendeza sana sis watz kuamka na kuonesha wazi kuwa tunaweza kuikomboa nchi kutoka kwa wakoloni mafisadi wanaojipandikiza kana kwamba nchi hii wao ndo walizalïwa kwanza na kupewa madaraka ya kututawala. Bigup wana Arumeru.
 
Back
Top Bottom