MVUMBUZI
JF-Expert Member
- Jan 8, 2011
- 5,182
- 2,304
Jana wakati wananchi wa Arusha na vitongoji vyake wanasubiri kwa hamu matokeo ya uchaguzi wa jimbo la Arumeru Mashariki ni kituo cha SUNRISE RADIO FM kilifanya kazi kilichopaswa kufanya kama chombo huru cha habari. Ni kituo hiki tu kilichoamua kuchukua jukumu la kurusha matangazo ya siku nzima bila kuchenga kutuhabarisha hatua kwa hatua kila kilichokuwa kinaendelea kule Arumeru Mashariki. Again ni kituo hiki kupitia watangazaji wake mahiri waliokuwa kila kona ya Arumeru leo asubuhi waliotangaza LIVE matokeo ya uchaguzi wa jimbo la Arumeru ambapo kijana mpiganaji na kamanda Nassari aliibuka kidedea.
Naomba nichukue fursa hii kwa niaba ya wasikilizaji na wananchi wengi wa Arusha mjini na vitongoji vyake kuushukuru na kupongeza uongozi na watangazaji woote wa kituo hiki kwa kuonyesha uzalendo usiopimika licha ya hujuma za kukatiwa umeme na TANESCO.
Uoga na ushabiki kwa CCM ulioonyeshwa na vituo vingi vya habari na kushindwa kuripoti ukweli kuhusu yaliyokuwa yakitokea nachukulia kama acid inayowamaliza wenyewe na ni wakati sasa wa ku-assess position zao kwa wananchi upya kabisa. Sunrise redio Arusha tunawapongeza na kuwatakia mafanikio mema naamini PAMOJA TUNASONGA MBELE KULETA MABADILIKO BILA UNAFIKI. CHEERS WOOOTE STUDIO
Naomba nichukue fursa hii kwa niaba ya wasikilizaji na wananchi wengi wa Arusha mjini na vitongoji vyake kuushukuru na kupongeza uongozi na watangazaji woote wa kituo hiki kwa kuonyesha uzalendo usiopimika licha ya hujuma za kukatiwa umeme na TANESCO.
Uoga na ushabiki kwa CCM ulioonyeshwa na vituo vingi vya habari na kushindwa kuripoti ukweli kuhusu yaliyokuwa yakitokea nachukulia kama acid inayowamaliza wenyewe na ni wakati sasa wa ku-assess position zao kwa wananchi upya kabisa. Sunrise redio Arusha tunawapongeza na kuwatakia mafanikio mema naamini PAMOJA TUNASONGA MBELE KULETA MABADILIKO BILA UNAFIKI. CHEERS WOOOTE STUDIO