kwa uhalisia ukawa hakuna mgombea mwenye ushawishi au mvuto wa kisiasa kwa sasa kwenye ngazi ya upresidenti.
Dr,prof,mbatia,mbowe na makaidi wanaweza kua na ushawishi mkubwa sana kwenye ngazi ya ubunge,ila kwenye urais wamepoteza sana ushawishi.
Mfano ikitokea ccm wakamsimamisha lowassa ambae kwa sasa anaonekana mwenye ushawishi mkubwa kwa watanzania(ingawa bunge liliwahi kuazimia kua ni mwizi hadi akajiuzuru) hakuna kiongozi wa ukawa anaweza kusimama nae.
Binafsi ningeshauri ukawa wasimamishe mtu mwingine kabisa ila hao viongozi hawana mvuto wala ushawishi wa kisiasa kiasi kwamba wanaweza kushinda urais,ila kama ni kuwasimamisha tu kwa ajili ya kuleta upinzani sawa vinginevyo hapana.