The Father of All
JF-Expert Member
- Feb 26, 2012
- 10,959
- 13,426
Wengi wanawalaumu bure watawala wetu kwa kusisitiza amani bila haki.
Wanawalaumu watawala bure kwa kushindwa kutatua matatizo ya kijamii kama vile upatikanaji wa maji.
Wanawalaumu kwa kutunyima haki lakini wakatupa amani huku tukisota na wao wakiishi kwa amani.
Tunababana kwenye misururu barabarani lakini tuna amani.
Heri kuwa na imani ya amani hata bila amani ya kweli lakini kukawa na amani.
Amani kwanza mengine baadaye.
Amani inaweza kuleta kila kitu hata kama ni ndotoni.
Adui wa amani ni mbaya kuliko adui wa haki.
Kukiwa na amani, kuna haki ila kukiwa na haki, amani itapotea.
Kwanini hatuwaelewi watawala wetu ambao sijui kama wanatuelewa?
Kukiwa na amani, mwenye njaa itamuuma kwa amani.
Kukiwa na amani mwenye chakula atakula kwa amani.
Amani ikosekana na haki ikatawala watu watakuwa na kiburi kama cha watawala ambao wana amani wanayosisitiza.
Kwa vile watawala wetu wanatuwakilisha, wakila na kushiba kwa amani, sisi pia tunaishi kwa amani.
Ukidai haki, ujue. Unatishia na kuvuruga amani.
Swali kuu, je, amani yetu ni ya nani na kwa ajili ya nani?
Napiga kelele kimya kimya na kuwaza kwa kutowaza.
Yote tukose ila si amani. Kwani, amani inaliwa, inavaliwa, inawekwa benki, na yote katika yote, amani ni uhai.
Wanawalaumu watawala bure kwa kushindwa kutatua matatizo ya kijamii kama vile upatikanaji wa maji.
Wanawalaumu kwa kutunyima haki lakini wakatupa amani huku tukisota na wao wakiishi kwa amani.
Tunababana kwenye misururu barabarani lakini tuna amani.
Heri kuwa na imani ya amani hata bila amani ya kweli lakini kukawa na amani.
Amani kwanza mengine baadaye.
Amani inaweza kuleta kila kitu hata kama ni ndotoni.
Adui wa amani ni mbaya kuliko adui wa haki.
Kukiwa na amani, kuna haki ila kukiwa na haki, amani itapotea.
Kwanini hatuwaelewi watawala wetu ambao sijui kama wanatuelewa?
Kukiwa na amani, mwenye njaa itamuuma kwa amani.
Kukiwa na amani mwenye chakula atakula kwa amani.
Amani ikosekana na haki ikatawala watu watakuwa na kiburi kama cha watawala ambao wana amani wanayosisitiza.
Kwa vile watawala wetu wanatuwakilisha, wakila na kushiba kwa amani, sisi pia tunaishi kwa amani.
Ukidai haki, ujue. Unatishia na kuvuruga amani.
Swali kuu, je, amani yetu ni ya nani na kwa ajili ya nani?
Napiga kelele kimya kimya na kuwaza kwa kutowaza.
Yote tukose ila si amani. Kwani, amani inaliwa, inavaliwa, inawekwa benki, na yote katika yote, amani ni uhai.