Here we Go-Mnyika na Nape live ITV

Here we Go-Mnyika na Nape live ITV

daaah nakosa uhondo wakuu.hii mikazi ya mpaka uck afu kina Pinda wanakula em zote hizo
 
Mnyika, anaulizwa kuhusu katiba anaongelea kuhusu Nyalali, nakwambia huyu kijana kidogo ana matatizo ya Kichwa.

Sasa anaongelea uchumi na ushindani na vyama vya ushirika. Nakwambia hata sielewi anaongelea nini?
 
Mnyika anadanganya eti tume ya Nyalali ilisema watu wanataka vyama vingi, wakati ukweli ni kuwa tume ya Nyalali ilisema 20% tu ndio wanataka vyama vingi na 80% walikataa vyama vingi.
\\\Nfikiri umemuelewa alichokuwa akikilenga
 
Jaman mimi ka ITV Kameshaniandikia No signal! Endelea kunipa updates
 
Nape sasa.......ANASEMA katiba iliyopo ni nzuri...inataka mabadiliko machache...imefanyiwa mabadiliko na nchi nyingi zinakuja kuiga...anasema tusiipuuze kwa sababu imetusaidia kufika hapa...tusiifanye katiba ya sasa kama takataka
 
Poor nepi anajisifia moja ya utekelezaji na maendeleo ya nchi ni kutoka mtwara mpaka mwanza kwa tax hahhaaa
 
leo mpaka sasa nimefurahishwa na nidhamu wote jj..nn na mtangazaji katulia
 
Anasema kwa spidi yao ya utekelezaji wa ilani,wako comfortable kuwa watatimiza...anakubali kuna tatizo kubwa la maji...anaongelea kuwa wametengeneza access kwenye elimu ingawa kunaweza kuwa na tatizo la quality....anasema yeye alifaulu wakiwa watatu katika darasa la watu 106...Hahahahahah...Nape ni janga
 
Nape anasema kipindi akisoma waalikuwa 106 ila walifaulu 3 tu
 
Miaka 50 ya uhuru anaongelea visima vya maji ambavyo wameomba world bank na wakapigwa changa la macho,na hii maana yake ni kwamba wanapeana posho na kununua magari ya kifahari halafu visima vya maji wanaenda kuomba,aibu gani hii...
 
Nape leo amekiri waziwazi kuwa serikali ya CCM haijaweza kutekeleza sera zake kwa ukamilifu. Hasa elimi, maji, ajira, barabara na mengineyo.
 
2015 hatupigi kura kwa fadhila ya nani kafanya nini ila kwa mipango mipya yenye muono wa utekelezaji na watu makini c c m isibweteke na mabarabara
 
Anasema wanapongezwa na dunia katika idadi ya hospitali..Vita ya UKIMWI..Anasema wao wanaridhika ingawa bado kuna maeneo yanahitaji juhudi za ziada...Mfano kwenye elimu wamejenga chuo kikuu dodoma ambacho hakikuwepo kwenye ilani...anasema kiongozi mzuri ni yule anaangalia mahitaji ya wakati....2005 walijenga shule nyingi wakajisahau kuhusu walimu
 
Jamaa ----- kweli anasema kuwa hata chuo kikuu cha Dodoma hakikuwa kwenye ilani ya uchaguzi ......
 
Mnyika anadanganya eti tume ya Nyalali ilisema watu wanataka vyama vingi, wakati ukweli ni kuwa tume ya Nyalali ilisema 20% tu ndio wanataka vyama vingi na 80% walikataa vyama vingi.

Hiyo 20% sio watu
 
Na wewe mpenzi, kila sehemu kubishana na Wanaume. Ungelikuwa Afghanistan..... Wajomba zako Taliban sijui wangelikufanyaje..... Wajionaje hali lakini kwa siku ya leo? Lazima nikiri kuwa unasaidia sana michango iwe mikali hapa JF. Keep doing what you are doing 🙂
Mnyika anadanganya eti tume ya Nyalali ilisema watu wanataka vyama vingi, wakati ukweli ni kuwa tume ya Nyalali ilisema 20% tu ndio wanataka vyama vingi na 80% walikataa vyama vingi.
 
Back
Top Bottom