Herdroth - Sehemu 1

Herdroth - Sehemu 1

plan z

JF-Expert Member
Joined
Jun 10, 2019
Posts
1,395
Reaction score
1,439
FB Group: STORIES

SEHEMU YA 01.

Katika falme ya Tardosen alikuja mtu kutoka falme ya mbali sana akiwa na farasi mweusi. Knights of Tardosen wakiwa juu ya minara ya ulinzi katika falme hiyo ya Tardosen walimwona mtu huyo akiwa anakuja kwa kasi akiwa amempanda farasi wake mweusi akiwa na ngao na upanga wake mkononi.(Knight ni majina waliyoitwa walinzi au mashujaa wa nyakati za kifalme, walikuwa hodari wa kupigana wakiwa wamepanda farasi)

Tardosen ilijengwa ndani ya jengo moja kubwa sana la kifalme, watu wote wa falme hiyo walienea ndani ya jengo hilo kubwa sana. Tardosen ilikuwa ni ghorofa kubwa sana yenye pande tatu, upande wa juu ndipo alipokaa mfalme na wakuu wake na watu wenye vyeo katika ufalme. Upande wa kati wa jengo hilo walikaa watu wa kati, na wafanyabiashara na matajiri, watu wa upande wa kati walikuwa ni watu wenye uwezo kiuchumi lakini hawakuwa viongozi. Upande wa chini ndipo walikaa masikini na watu wasiojiweza na tegemezi.

Tardosen ilikuwa ni falme tajiri na yenye kuheshimika kuliko falme zingine zote kwani ilikuwa na nguvu na mamlaka kubwa kutokana na nguvu ya kiuchumi na nguvu ya jeshi iliyokuwa katika falme hiyo ya Tardosen.

Mfalme "Strodgan Trosphontere" wa Tardosen alikuwa ni mfalme mwenye dharau kwa watu wake hata falme zingine alizidharau, na aliwabagua maskini na kuwaona hawana thamani.

Knights of Tardosen baada ya kumwona mtu huyo akielekea kulikabili lango ya mbele la kuingilia Tardosen walijipanga kupigana naye ili kumzulia. Mtu huyo alifanikiwa kuwaua wale walinzi na kuwashinda mpaka kuingia ndani kabisa hadi ilipokuwa ikulu ya mfalme.
"Wewe ni nani?", mfalme alimuuliza.
"Knight of Rodrino", alimjibu mfalme kisha akaitupa arm yake ya kivita akimaanisha anaomba mpambano. Mara moja knight mmojawapo wa Tardosen aliiokota arm hiyo akiashiria amekubali mpambano na mtu huyo.
"Lini?",mfalme alimuuliza mtu huyo.
"Kesho mchana", alijibiwa.

Rodrino ni falme ya mbali sana kutokea Tardosen. Miaka zaidi ya ishirini iliyopita, mfalme Strodgan Trosphontere aliishambulia falme hiyo ya Rodrino na kuangamiza jeshi lote katika falme hiyo na kujizolea utajiri mwingi wa falme hiyo. Watu waliosalia walikuwa wachache sana wale dhaifu.

"Mercuset" alikuwa mwana mama wa Rodrino mchawi. Wakati Tardosen ilipoivamia Rodrino alipoteza familia yake, waliuawa wakati wa vita akabaki yeye peke yake hali ya upweke huku akiwa na msiba wa wanawe pamoja na mumewe.

Mwana mama huyu alikuwa akitumia uchawi wa dini ya kizamani. Mercuset alikwenda katika makaburi ya mashujaa wa kizamani yaani Knights of Rodrino akamwamsha shujaa mmojawapo kwa maneno ya kichawi kwa lengo la kulipiza kisasi.

Wakati wa usiku watu wa Tardosen walishangaa kumwona Knight of Rodrino akiwa kwenye uwanja wa vita akusubiri mpambano wa kesho. Amesimama tu amechomeka mkuki wake chini akiwa amevalia koti jeusi refu mpaka miguuni. Hakai, halali, wala hali. Watu walimwogopa sana.

Wakati wa mpambano ulifika knight of Rodrino alimshinda knight of Tardosen na kutupa tena arm yake ya kivita kuomba mpambano mwingine. Alibaki pale pale uwanjani akisimama vile vile kusubiri mpaka kesho mchana. Hali, hakai wala halali. Na aliwashinda wote aliopambana nao. Lengo lake lilikuwa ni mpaka amuue mfalme Strodgan Trosphontere.

Safari hii mtoto wa mfalme ambaye ndiye mtarajiwa atakirithi kiti cha ufalme wa Tardosen aliamua kuiokota arm ile ya kivita kuashiria kukubali mpambano na mtu yule.
"Mimi Strodgento Trosphontere, nitapambana na wewe kesho", alisema maneno hayo huku akiokota arm ile. Mfalme alishtushwa sana na kitendo cha mwanaye kuchukua uamuzi ule. Ikumbukwe kwamba mpambano ni hadi kifo, kwani knight of Rodrino aliwaua wote aliokwisha kupambana nao. Ndiyo sheria za mpambano zilivyokuwa. Sasa wasiwasi ulikuwepo mtoto wa mfalme anakwenda kuuliwa na ni nani sasa atakuwa mfalme hapo baadaye.

Katika falme ya Tardosen kulikuwa na tabibu aitwaye Jaiden, alikuwa akitibu watu wote wa Tardosen na kutoa ufumbuzi wa matatizo mbalimbali yanayoikubwa Tardosen na amedumu kwa kipindi kirefu hivyo ni mtu wa makamo. Jaiden ni mtu wa busara sana.

Jaiden anaishi kwenye maabara yake pamoja na kijana aliyezaliwa na kipaji alichorithi kutokana na mama yake kuwa na asili hiyo. Yaani mama yake ametokana na "Teez".(Teez ni aina flani ya watu wenye uchawi wa asili. Kijana huyo anaitwa "Herdoth".

Usiku huo mfalme Strodgan Trosphontere alimwita Jaiden na kumuuliza kama ana lolote la kusema.
"Hii ni elimu ya dini ya zamani ya kichawi, huyu knight of Rodrino ni shujaa wa zamani ameamshwa kichawi naona anakuja kulipa kisasi", Jaiden alikuwa akitoa maelezo kwa mfalme.
"Ni kweli nilimuua, umepata wapi hizi taarifa?", mfalme aliuliza.
"Nimezipata maktaba", alijibiwa.

Tardosen kulikuwa na maktaba kubwa sana tangu enzi na enzi, tangu ufalme na ufalme. Kila tukio lililotukia lilikuwa likiandikwa na kuhifadhiwa katika maktaba hiyo pamoja na picha mbalimbali zilichorwa ndani ya vitabu hivyo.

Knight of Rodrino alikuwa na mkuki wenye pembe tatu zilizochongoka huku upande wa katikati wa mkuki huo ulikuwa mrefu zaidi.

Jaiden na Herdoth walipouona mkuki huo walienda maktaba na kugundua kuwa knight of Rodrino aliamshwa kichawi kwa lengo la kulipiza kisasi. Wakampa taarifa mfalme Strodgan Trosphontere.

Mfalme alimwita Jaiden peke yake na kumweleza kwamba kesho yeye ndiye atakayepigana ili kumnusuru mwanawe, Tardosen isije ikakosa mfalme hapo baadaye. Hivyo alimwambia ampe dawa ya usingizi mwanaye itakayomfanya alale kupitiliza mpaka pambano litakapoisha, ili mwanaye asife kwa ajili ya jambo alilolitenda mfalme. Kwani Strodgento Trosphontere, mtoto wa mfalme alikuwa mtu asiyekubali kushindwa. Hivyo waliamua watumie njia hiyo mwanaye asiende kupigana akauawa.

"Chukua hii dawa unywe, itakuondolea uchovu katika mwili wako", Jaiden alimpa dawa ile Strodgento.

Wakati wa pambano, mfalme alivaa mavazi ya kivita kupambana na knight of Rodrino huku watu wote wakiwa wanatizama. Jaiden na Herdoth pia walikuwemo. Mpambano ulikuwa mkali mfalme alimtoboa knight of Rodrino tumboni na upanga, lakini knight huyo hafi, hana tofauti na mizimu.

Mpambano uliendelea hatimaye mfalme aliangushwa chini. Knight of Rodrino akaunyanyua upanga wake akijiandaa kumuua kabisa Strodgan.

Hedroth alipoona hayo akabadilika macho yakawa ya dhahabu akatamka matamshi ya kichawi ya kuharibu nguvu ya uchawi aliyokuwa nayo Rodrino na kumwangamiza kabisa.

"Waan-ros dran patro swan hurto", Hedroth alitamka ndipo knight huyo akalipuka kama bomu akateketea pale pale ikawa ushindi kwa Strodgan Trosphontere.

ITAENDELEA.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
HERDROTH

SEHEMU YA 2.

Baada ya ushindi wa Tardosen dhidi ya Knight of Rodrino, Tardosen ilikuwa na amani watu wakiendelea na shughuli zao kama kawaida. Mercuset, yule mama aliyemwamsha Knight of Rodrino kichawi kwa lengo la kuilipizia kisasi Tardosen alikuwa akiitazana Tardosen kwenye maji kichawi. Mercuset akamwona mfalme na mwanawe wakila na kunywa na wakicheka kwa furaha. Mercuset hilo jambo hakulifurahia, akajiapiza bado ataishambulia Tardosen hadi ishike adabu.

Falme ya Tardosen ilipata ugeni kutoka falme nyingine ya jirani kidogo na Tardosen kwa ajili ya kuimarisha umoja na undugu baina ya falme hizo mbili. Falme hiyo inaitwa "Falme ya Drusilito".

Mfalme Gruseilo wa Drusilito alikuwa na binti yake anaitwa Nezandria alitaka atumie uchawi kuwafanya wapendane na Strodgento Trosphontere ili baadaye aje achukue utajiri wa Tardosen kwa kupitia binti yake, alikusudia pia kumwua mfalme na mwanaye endapo atamwozesha bintiye kwa Strodgento.

Mfalme Gruseilo na watu wake walipewa nyumba za wageni huko Tardosen. Wakati wa usiku mfalme Griseilo alimtuma mtaalamu wake kuchukua unywele wa kila mmoja wao. Alifanikiwa kuchukua unywele wa Strodgento kwa usiku huo kwa siri sana akiwa amelala.

Mtaalam wa mfalme Gruseilo alimloga Strodgento kwa kupitia unywele wake na akampenda sana Nezandria.

Herdroth na Strodgento ni marafiki na wamezoeana sana kutaniana tofauti ni kwamba Strodgento ni mtoto wa mfalme na Herdroth ni wa maisha ya chini isipokuwa Herdroth ana zawadi aliyozaliwa nayo, anaweza kutenda miujiza au uchawi wa asili na anautumia kusaidia, sio kuumiza au kuloga wengine. Ila kwa siri sana.

"Herdroth!", aliita Strodgento.
"Herdroth!"
"Herdroth!", aliendelea kuita bila mafanikio.

Ilibidi Strodgento kwenda kumuuliza Jaiden alipo Herdroth.
"Ameenda bar!", alidanganya Jaiden.
"Shit! Haiwezekani", alilalamika na kuondoka. Yani amemzoea sana Herdroth.

"Herdroth ulikuwa wapi?", Strodgento alimuuliza baada ya kumwona.
"Umm..."
"Aah.."
"bar!", alijibu kwa kujing'atang'ata.
"Siku nyingine ukiondoka bila kuniaga nitakutoa pua", alitishia Strodgento.

Strodgento alimweleza Herdroth jinsi anavyompenda Nezandria.
"Vipi kuhusu Janvrey", aliuliza Herdroth.(Janvrey ni mtumishi katika falme ya Tardosen, Strodgento na Janvrey walikuwa kwenye mahusiano lakini kwa siri sana maana ni aibu kwa mtoto wa mfalme kuwa kimahusiano na mtumishi)

"Saiv nampenda Nezandria", alijibu Strodgento.
"Siku mbili tu unampendaje mtu hata hujamjua vizuri", alijibu Herdroth.
"Siku nyingine ukiniuliza maswali sana nakunyoa kipara. Toka Hapa!", alifoka Strodgento na kumfukuza Herdroth.

"Herdroth!", aliita Stodgento masaa baadaye baada ya kumfukuza.
"Nipelekee haya maua kwa nimpendaye pamoja na barua hii umpe", Strodgento alimwagiza Herdroth.

Herdroth akapeleka yale maua na ile barua kwa Janvrey kumbe Strodgento alimaanisha yapelekwe kwa Nezandria. Janvrey akayapokea na kusoma ile barua iliyokuwa ikisomeka hivi:
" Jiandae badae jioni baada ya kikao nitakuja kwako"
Ni barua kama yenye amri flani hivi ukiitazama lakini Janvrey alielewa alishamzoea Strodgento kwani ukoo wa Trosphontere ni ukoo wa kifalme na hawajuagi kubembeleza.

Wakati wa Jioni Stodgento alikuwa akimshangaa Nezandria kama vile hajui chochote kinachoendelea, kampita tu. Strodgento alikuwa anajiuliza maswali mengi bila majibu.

Upande wa Janvrey alijipamba, akawasha mishumaa akawa anamsubiria Strodgento. Alisubiri sana mpaka usiku ukaingia akasinzia akaegemea meza aliyokuwa amekaa mbele yake, usingizi ukampitia.

Strodgento aliingia moja kwa moja kwenye chumba cha Nezandria kwa siri sana bila mtu yeyote kumwona.
"Unatafuta nini?", Nezandria aliuliza.
"Haujapata ujumbe wangu?", alijibiwa kwa swali.
Strodgento aliduwaa akawa akijiuliza inamaana Herdroth alimpelekea nani barua na maua. Ikabidia aanze kumsogelea, Nezandria akapiga ukelele uliosababisha watu wengine kuingia ndani, ikiwemo mtaalam wa mfalme Gruseilo ambapo katika purukushani alifanikiwa kuchukua unywele wa Nezandria, akaenda pia kuuloga ili wapendane. Ndipo lengo lao litimie.

Baada ya siku hiyo kupita Nezandria alimwomba Herdroth amweleze Strodgento jinsi anavyompenda.(baada ya kulogwa)
Hedroth alijiuliza sana inakuwaje.

Herdroth alifanya uchunguzi wa siri na akagundua chumbani kwa Strodgan na chumbani kwa Nezandria kuna mzizi umefungiwa unywele, katika vyumba vyao kila mmoja chini ya kitanda ndipo aliposhtuka uchawi umetumika.

Wakati huo Strodgento na Nezandria walikuwa wametoroka na farasi wameenda msituni sehemu iliyotulia kufurahia mapenzi yao. Kumbe walikuwa wakifuatiliwa.

Taarifa zilimfikia mfalme wa Tardosen Strodgan Trosphontere kuwa mwanaye Strodgento na Nezandria wamekutwa msituni wakiwa katika uhusiano.

Strodgento na Nezandria walilazimika kuoana huku Janvrey roho ilikuwa ikimuuma sana.
"Strodgento unakubali kumwoa Nezandria", aliulizwa.
"Ndiyo! Ndiyo!",alijibu haraka haraka.
"Je wewe Nezandria unakubali kuolewa na Strodgento"
"Ndiyo nakubali!", alijibu.
Walijibu haraka haraka kwani wamelogwa.

"whos krazuu ozdaar-troziyaa, trukanazoo ira stabaa-ntrayii, wozraa prastozee ristokirazantozinda", ilikuwa ni spell aliyoitamka Hedroth kuondoa nguvu ya uchawi rafiki yake Strodgento aliologwa nao baada ya kusoma vitabu. Huku macho yake yakibadilika rangi na kuwa ya dhahabu.

"Kuna yeyote mwenye pingamizi?", ndoa ilikuwa ikiendelea kufungwa.
"Subiri!", alisimamisha Strodgento.
"Nashangaa kwanini niko hapa, mimi simpendi Nezandria", aliongezea.
"Hata mimi sina hisia na Strodgento", alisema Nezandria. Hapo ni baada ya nguvu ya uchawi waliologwa nao kuondoka.

Watu walistaajabu kinachoendelea hawakujua nini kimetokea kati yao. Ndoa ikahairishwa na mfalme Gruseilo pamoja na mtaalamu wake wakaondoka Tardosen kwa aibu, hawakutimiza lengo lao.

ITAENDELEA.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
HERDROTH

SEHEMU YA 3.

Mfalme Gruseilo wa Drusilito baada ya kurejea kutoka Tardosen alikuwa akijiuliza sana ni kwanini alifeli kutimiza mpango wake wakati alijua fika kwamba falme ya Tardosen haikuwa ikiruhusu uchawi. Alijiuliza sana nini kilimzuia lakini hakuwa na majibu yeyote.

Mfalme Gruseilo aliwaita wachawi wote na waganga katika falme yake ya Drusilito na kuwauliza ni namna gani wanaweza kuishambulia Tardosen kwa kutumia uchawi maana kwa vita wasingeweza kwani falme ya Tardosen ni falme yenye nguvu sana kuliko falme zingine zote.

Gruseilo aliwaahidi donge nono kila mmoja wao, aliwahaidi angewalipa kwa dhahabu na kuwapa sehemu nzuri ya kuishi wao na familia zao.

Miongoni mwa wachawi wa Drusilito walioitwa na mfalme, alisimama mmoja wao aliyeitwa Chranchozki akaeleza kuwa hata yeye aliwahi kujaribu kuishambulia Tardosen kwa maslahi yake binafsi lakini hakufanikiwa. Alieleza licha ya Tardosen kupiga vita uchawi hata kuwahukumu kifo waliogundulika wakitumia uchawi bado inaonekana kuna anayeisaidia Tardosen kwani yeye mwenyewe alijaribu mara tatu kwa nyakati tofauti bila ya mafanikio.

Chranchozki alieleza kwamba katika falme ya Rodrino kuna mama anaweza akawasaidia jina lake anaitwa Mercuset, alieleza kuwa Mercuset uchawi wake ni wa dini ya kizamani, watu wanaotumia uchawi wa dini ya kizamani uchawi wao una nguvu.

Gruseilo alikubaliana na wazo la Chranchozki na akaamua yeye mwenyewe kwenda Rodrino kwa ajili ya kuzungumza na Mercuset kwa lengo la kupata msaada kutoka kwake.

Mfalme Gruseilo kesho yake alifunga safari pamoja na askari wake anaowaamini pia aliambatan na Chranchozki kuelekea Rodrino.

Hatimaye walifika Rodrino. Askari wa Rodrino walipowaona walijipanga kivita wakidhania wamevamia lakini mfalme Gruseilo alijitambulisha na kueleza amekuja kwa amani. Askari wakamkaribisha na kumpeleka kwa mfalme wa Rodrino aitwaye "Weinklove".

Weinklove alimfanyia sherehe Gruseilo pamoja na wote aliombatana nao kwani ni siku nyingi sana hawakuonana. Baada ya kula na kunywa Gruseilo alimweleza Weinklove nia yake ya kuja hapo Rodrino na pia alitaka kizungumza na Mercuset.

Mfalme Weinklove alimsaidia Gruseilo kukutana na Mercuset na Gruseilo akamweleza alichokiitaji. Mercuset alikubali kushirikiana na Gruseilo kwani na yeye pia alikuwa na kisasi na Tardosen vile vile.

"Dosh pien kalie, kroz dun wailon koshie, zii-nja, strivu lionee zindra", ilikuwa ni spell aliyoitamka Mercuset huku macho yake yakibadilika rangi na kuwa ya dhahabu. Ghafla akatokea simba mwenye mabawa anapaa na anatema moto. Mercuset alimtuma kiumbe huyo kichawi awe anaishambulia Tardosen wakati wa jioni na usiku huku yeye akiwa anatizama yanayojiri kwenye maji aliyoyaweka kwenye aina flani ya beseni.

Tardosen ilikuwa na amani, watu walikuwa wakila na kunywa na kufanya shughuli zao kama kawaida ghafla majira ya jioni yalipoingia walishangaa kumwona kiumbe wa ajabu akipita katika anga lao na kuwatemea moto na kushambulia maeneo mbalimbali ya Tardosen.

Kwenye maabara ya Jaiden majeruhi walikuwa wengi na watu hamsini walipoteza maisha waliposhambuliwa na kiumbe huyo. Wakati wa jioni ulipofika tena kiumbe huyo alifika tena na kuishambulia Tardosen jambo ambalo hata mfalme Strodgan mwenyewe alichanganyikiwa kuona ufalme wake ukiteketea. Mfalme alimwita Jaiden usiku huohuo na kumtaka atafute ufumbuzi wa jambo hilo kwa kuwa Jaiden ameishi miaka mingi na ameona mambo mengi hivyo mfalme aliamini Jaiden anaweza akampa ufafanuzi wa kiumbe huyo.

Jaiden na Herdroth walijadiliana namna ya kufanya huku wakiendelea kusoma vitabu mbalimbali wa kichawi kuona kama watagundua mnyama huyo anatokana na nini na ni jinsi gani watamdhibiti kwani alikuwa akizidi kusababisha madhara makubwa ndani ya Tardosen.

"Kiumbe huyu anaitwa Preskelin, ametengenezwa kichwawi kwa kutumia uchawi wa dini ya kizamani kwa kutumia spell yenye nguvu", yalikuwa ni maelezo aliyokuwa akiyatoa Jaiden kuhusu kiumbe huyo baada ya kumsoma kwenye kitabu na kwa kuona picha yake. Lakini kwakuwa mfalme Strodgan hakuwa akiamini uchawi alipuuza maneno ya Jaiden na badala yake alituma jeshi likapigane na kiumbe huyo pindi atakapotokea.

Herdroth alikuwa akihangaika kutafuta spell itakayo mwangamiza kiumbe huyo bila mafanikio kwani kila spell aliyoijaribu iligonga mwamba. Akapitia vitabu akagundua njia pekee ya kumwangamiza kiumbe huyo ni kwa kutumia moto.

Kiumbe huyo alijitokeza tena majira ya jioni askari wakajipanga kupigana naye walimtoboa na panga zao na mikuki yao bila ya kufanikiwa kumwangamiza mwishowe waliambulia kutemewa moto na kwa bahati nzuri walikinga na ngao zao ndo ikawa salama yao.

Kesho yake wakati knights of Tardosen wakijiandaa kumkabili kiumbe huyo, kuna knight mmoja anaitwa Razad. Knight huyo Herdroth alimfuata walikuwa marafiki.
"Razad nataka baadaye ukienda kupambana na kiumbe huyo tuongozane mimi na wewe", Herdroth alimwambia Razad.
"Lakini wewe sio mtu wa vita utafia huko, shauri yako", alijibu Razad.
"We twende wote, nikifa si basi", alijitetea Herdroth. Basi walikubaliana kwenda wote.

Wakati wa jioni kiumbe huyo akaja tena kama kawaida yake akaishambulia Tardosen, knights walijipanga kwenye kumshambulia, hadi Strodgento Trosphontere mtoto wa mfalme alikwenda ili kupiga na kiumbe huyo.

Kiumbe huyu anapoona anafatwa anatabia ya kujitokeza kupambana, yani haogopi vita na mkitaka kumshambulia yeye anajua na anajileta ili mpambane naye kama mtamweza.

Askari walipambana naye huku wameshika mapanga yao na mikuki yao pamoja na ngao zao na mienge ya moto kwa ajili ya mwanga kwani ni usiku. Ile mienge ya moto ndiyo iliyowasaidia wasishambuliwe na kiumbe huyo kwa haraka kwani licha ya kuwa kiumbe huyo anatema moto ila yeye mwenyewe anaogopa moto.

Askari walipambana naye na kiumbe huyo aliwachapa makofi na mabawa yake wakaanguka chini, hadi Strodgento alikuwa chini. Kiumbe huyo ndo alikuwa akijipanga kuwaanganiza kabisa kwa kuwatemea moto.

Wakati huyo Herdroth na Razad walikuwa wakija kwa kasi na farasi kumwelekea kiumbe huyo. Herdroth alipoona askari wanataka kutemewa moto na watakufa wote pia Strodgento naye atakufa alimwambia Razad aongeze mwendo kisha yeye akabaki nyuma kidogo ili apate nafasi ya kutumia magic yake kwa siri bila kugundulika.

Herdroth alitumia macho yake akamtandisha shoti kiumbe huyo ili kumzubaisha huku macho yake yakibadilika rangi kuwa ya dhahabu.

Razad alikuwa akikaza mwendo huku kaunyoosha mkuki wake mbele ili akifika amtoboe kiumbe huyo.
"zaan-ruto kurzairan wazi, ostodhee rinfoo shhh", Herdroth alitamka spell lakini haikuleta matokeo. Akaitamka mara ya pili pia haikuleta matokeo. Herdroth alikasirika akaitamka tena mara ya tatu kwa sauti ya juu "zaan-ruto kurzairan wazi, ostodhee rinfoo shhh", safari hii mkuki wa Razad uliwaka moto kwa mbele Razad akamtoboa nao kiumbe yule akafa palepale.

Strodgento akampandisha cheo Razad awe Knight mkuu wa Tardosen baada ya yeye kuwasaidia kumshinda yule kiumbe. Razad na Herdroth wakati wanapiga stori, Razad alimwambia Herdroth unayo magic nilikusikia ukiongea maneno ambayo sikuyaelewa. Herdroth alimwambia iwe siri yake asimwambie mtu kwani akigundulika atauawa hivyo wakafichiana siri.

ITAENDELEA.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
HERDROTH

SEHEMU YA 04.

Strodgento alitoka kwa siri kwenye jumba la kifalme la Tardosen kwenda kwa Janvrey, mwanamke aliyekuwa akimpenda. Hakutaka mtu yeyote ajue ili taarifa zisimfikie mfalme.

"Nenda msituni kanitafutie dawa mbali mbali nilizokufundisha kwa ajili ya matibabu", Jaiden alikuwa akimwagiza Herdroth.
Herdroth alikwenda msituni kumtaftia Jaiden madawa.
"Herdroth!", alisikia sauti ikimwita kwenye ufahamu wake, akageuka nyuma aone kama kuna mtu anamwita, hakuona mtu.

"Herdroth!", sauti iliendelea kumwita kwenye ufahamu wake pasipo kusikika kwa nje. Ikabidi aanze kuifuata ile sauti inapomwitia akaacha kuendelea kutafuta dawa alizotumwa na Jaiden.

"Janvrey unajua jinsi nnavyokupenda na nipo tayari kufanya lolote kwa ajili yako", Strodgento alikuwa akimwambia Janvrey.
"Wewe ni mtoto wa kifalme, na mimi ni mtumishi tu, tena nimetoka familia za chini, baba yako hawezi kubali unioe mimi tena akigundua ataniua", Janvrey alijibu.
"Sikia Janvrey, mimi ndo nitakuwa mfalme baada ya baba yangu, na nikishakuwa mfalme hakuna wa kunizuia mimi kukuoa wewe, naomba uniamini", Strodgento aliendelea kumshawishi Janvrey akubaliane naye.

Herdroth aliendelea kuifuatilia ile sauti hadi akaingia pangoni. Herdroth alimwona bibi ndiye aliyemwita. Bibi yule alikuwa ni "Teez" kama alivyo Herdroth. Teez wana nembo ya kuzaliwa nayo, wanakuwa na uchawi wa asili na pia wanaweza kuwasiliana kwa kutumia ufahamu bila kutoa sauti.

"Nakufahamu sana Herdroth, mungu wa mwisho wa Dragon baada ya baba yako kufariki miaka mingi iliyopita na wewe ndiye mrithi wake", bibi yule aliongea kwa sauti yake ya kizee ya kukoroma koroma. Maneno yale yalimfadhaisha sana Herdroth alisikia tu hadithi kwamba Dragon waliwahi kuwepo lakini hawapo tena.
"Huna sababu ya kuogopa Herdroth, hapa panaitwa Crystal Land na ndipo sehemu uchawi ulipoanzia na ndipo asili yetu ilipoanzia", aliendelea bibi yule kwa sauti ya kizee sana huku akimtizama Herdroth na macho yake yenye uono hafifu.
"Nipe mkono wako", bibi aliendelea. Herdroth akaunyoosha mkono wake wa kulia akampa bibi yule aushike.
"Nilikuwa nikitambua yuko mungu wa mwisho wa Dragon ajae na hatimaye baada ya kusubiri miaka mingi nimekuona, nilikuwa nimetabiriwa sitakufa mpaka nitakapo mweleza mungu wa mwisho wa Dragon sehemu mayai yalipo", bibi aliendelea kuongea kwa sauti ya kizee sana huku Herdroth akimtizama tu bila kusema neno lolote.

Bibi yule akambusu Herdroth mkono kisha akamwambia kwa sauti ya kizee ya kujitahidi sana.
"Nyuma yangu zaidi utaona mayai mawili nenda ukayatotoe"
"Nibusu kipajini Herdroth ndipo uende". Herdroth alimbusu na bibi yule akafariki pale pale, kumbe alitabiriwa mungu wa mwisho wa Dragon atakapombusu kipajini ndipo atakapo fariki.

Jaiden alikuwa akihangaika kumtafuta Herdroth, alianza kupatwa na wasiwasi kwanini amechelewa kurudi. Alienda chumbani kwake kuangalia kama atakuwa amerudi hakumkuta, akaenda msituni lakini pia hakumwona kisha akarudi huku akiwa na mawazo sana juu ya Herdroth.

"Nahaidi ntakuoa Janvrey, nitakapo kuwa mfalme hakuna atakaye nizuia, chukua na pete yangu hii hapa, lete kidole chako nikuvalishe", Strodgento aliongea maneno hayo na kumvalisha pete Janvrey.
Wote wakiwa wamesimama kisha Janvrey akapiga magoti kwa furaha kwa ahadi hiyo aliyoahidiwa ya kuolewa na Strodgento Trosphontere. Walifurahia mapenzi yao Strodgento akamkumbatia Janvrey na kumbusu mdomoni.

Herdroth alielekea huko alipoelekezwa na bibi yule akakuta kuna wadudu jamii ya ng'e wakubwa. Wadudu hao ndio waliokuwa wakiyalinda mayai hayo miaka yote. Lakini walipomwona Herdroth walimpisha.

"Zroos - patro hurto", Herdroth aliyawasha moto mayai, kwa spell ili ayaangue kwa moto na kwa haraka.

"Dragala de sandroo ze zikroo ashkanaal was hindro szeek waan book vouz dol zuan", aliongea hii spell na mayai yakaanza kujiangua.

Wakatoka Dragons wawili wadogo, mmoja mweusi mwingine mweupe. Herdroth akamwita yule mweusi "Drementa", yule mweupe akamwita "Krozdunn"

Akawasemesha, akaongea lugha ya kikwao ambayo Dragons wanaielewa.
"Kremen - waas patrino linko zii zaan zitra kwach hun listo drini lista mandra was dos kalie wan zus drila." Dragons wakawa wanamtii.

ITAENDELEA.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
HERDROTH

SEHEMU YA 05.

"Na hii itakuwa fundisho kwa watu wote waliopo katika falme ya Tardosen wanaotumia uchawi, binti huyu japo ni mdogo sana wa kama miaka nane namuhukumu kunyongwa kutokana na yeye kugundulika ana asili ya "Teez" hivyo akikua huyu atatusumbua", ilikuwa ni sauti ya mfalme Strodgan Trosphontere ambaye hakuwa na huruma hata kidogo kwa binti mdogo kabisa wa miaka nane na kumuhukumu kunyongwa.
"Binti huyu hajaanza kutumia uchawi ila ni lazima auawe kwa sababu atakuja kutulipizia kisasi kwa ajili ya "Teez" wengi waliouawa katika falme hii ya Tardosen na itakuwa tabu kwetu", Strodgan aliendelea kuhutubia na kisha baada ya hotuba akatoa amri binti akanyongwa.

Mfalme Stodgan baada ya kufanya lile tukio la kumuhukumu kunyongwa binti yule ambaye ni "Teez", mama yake na binti yule alikasirika sana na kuamua kulipiza kusasi.

Majira ya usiku mfalme Strodgan akiwa amelala na walinzi wakimlinda nje ya jumba lake la kifalme.( Ikubukwe kwamba falme ya Tardosen ilivyojengwa imejengwa kama jengo moja kubwa sana kupita maelezo na ina pade tatu, juu kati na chini, rejea sehemu ya kwanza. Kwahiyo hapa mfalme yuko upande wa juu). Ghafla kilipita kivuli ambacho hakina sura halisi kwa kasi ambayo walinzi hawakuweza kugundua ni kitu gani kimepita na kilipoelekea japo walisikia sauti ya mvumo kama upepo mkali kivuli kile kilipopita.

Kivuli kile kiliingia moja kwa moja hadi alipolala mfalme na kwa sauti ya kelele zile mfalme alishtuka kutoka usingizini na kukiona kile kivuli kama cha rangi ya kijivu na chenye kutoa mwanga.
"Mfalme Strodgan nataka kabla sijakuua nikufundishe ujue maana ya uchungu wa mwana ni nini. Yule binti uliyemhukumu kunyongwa ni mwanangu. Sasa nitakutesa mpaka ujue "Teez" hatuguswi", sauti ya kike ilizungumza na Strodgan Trosphontere mfalme.

Baada ya sauti hiyo kumsemea mfalme Strodgan, mfalme alitambua ni mama wa mtoto amekuja kulipiza kisasi. Mfalme alichapwa mfululizo usiku ule alivimba kila mahali. Na kivuli kile kikamuaga,
"Imetosha kwa leo nitakujia tena kesho usiku kuendelea kukupa adhabu na mwishowe ntakuua taratibu". Kisha kivuli kile kikaondoka kwa kasi pasipo kuonekana. Walinzi walisikia sauti kali kama imekatiza pasipo kutambua nini kimepita.

Mfalme kwa kuwa anamwamini sana Jaiden ni mzee wa busara alituma watu kumwita kulipopambazuka baada ya yaliyompata usiku na ahadi aliyoahidiwa kwamba kivuli kile kitamrejea tena usiku.
"Jaiden, kama unavyoona nilivyovimba na leo sijatoka nje kabisa kuepusha aibu itakayonipata watu watakaponiona na kunitangaza. Kiukweli baada ya kumuua binti yule, sasa mama yake amekuja kunilipizia kisasi na ameahidi atarudi tena na ameahidi ataniua taratibu. Hebu nitafutie ufumbuzi", mfalme alikuwa akimweleza Jaiden.
"Mfalme kwa kweli swala hilo ni uchawi ila mimi siwezi uchawi kabisa, mimi naweza madawa tu ya kitabibu mfalme. Ila nitasoma vitabu vyangu kama kuna dawa ya kumzuia au kupunguza maumivu nikutengenezee nikupatie", Jaiden alijibu, hakutaka kutumia uchawi kumsaidia japo angeweza sema naye anaogopa kuuawa vilevile. Jaiden naye ana asili ya "Teez", "Teez" wote wana nembo kwenye miili yao isipokuwa Jaiden na Herdroth pekee ndiyo hawana nembo.

Jaiden bado anamtafuta Herdroth bila mafanikio, ni siku ya tatu sasa tangu amemtuma Herdroth madawa hajarejea. Jaiden ameanza kuingiwa na wasiwasi wapi alipo Herdroth.

Kutokana na mfalme Strodgan Trosphontere kuendelea kuchapwa kila usiku. Jaiden anaamua kumsaidia mfalme kwa siri pasipo kugundulika anasoma vitabu vyake vya uchawi kutaka kujua ni uchawi wa aina gani anautumia mwanamke huyo. Katika kusoma kwake aligundua yule mama anatumia uchawi wa juu wa dini ya kizamani na Jaiden anagundua yeye hatoweza kumsaidia mfalme isipokuwa Herdroth tu ambaye ilitabiriwa ndiye mkuu kuliko "Teez" wote na nguvu zake ni zaidi( isipokuwa Herdroth hajijui kama ana nguvu za kutisha, anajidharau na kujiona kawaida). Basi Jaiden akamtengenezea mfalme dawa ya kutuliza maumivu tu baada ya kuchapwa awe anameza itampa utulivu.

"Kuna falme tatu zimeungana na zimeunganisha majeshi yao na tayari majeshi yapo njiani yanakuja kuishambulia Tardosen, falme ya Green Land, falme ya Trethe, na falme ya Brondon", mfalme Strodgan ameletewa taarifa hizo na askari wa zamu wa Tardosen na kuzidi kuwa na wasiwasi kutokana na taarifa hizo. Majira ya usiku mfalme Stodgan akafuatwa na kile kivuli na kuchapwa sana kisha kivuli kile kikamuaga na kumwahidi kitarejea tena kesho usiku.

Stodgento mtoto wa mfalme akaandaa jeshi la Knights of Tardosen kwenda kupigana na majeshi yanayokuja kabla hayajauvamia mji wa Tardosen na kuuharibu. Wakawahi nje ya Tardosen kwenye uwanja mkubwa na kuwasubiri maadui, uso kwa uso.

Knights of Tardosen walizidiwa sana vitani na wengi wakauawa hivyo waliamua kukimbia vitani wakamkamata Strodgento wakamfiche kwenye jumba la kifalme la Tardosen ili asiuawe maana alikuwa mbishi, alitaka aendelee
kupigana hivyo walimkamata kwa nguvu na kwenda kumficha, wasije wakakosa mfalme baadaye baada ya mfalme Strodgan.

Majeshi ya maadui yaliuvamia mji na kuuharibu pamoja na kuwaua watu ambao walijaribu kuwapinga pia waliteka watu mateka. Na Janvrey pia alitekwa kwa kuwa alikuwa upande wa chini wa Tardosen(upande wa watu wa maisha ya chini).

Stodgento akiwa kafichwa akapata taarifa Janvrey ametekwa (Janvrey ni kipenzi cha Strodgento rejea sehemu za nyuma). Strodgento akamwomba baba yake ampe jeshi aende akamkomboe Janvrey.
"Unataka uuawe wewe kwa sababu ya mtumishi, yule ni mtumishi tu hana thamani, siwezi kuendelea kupoteza jeshi langu kwa watu ambao hawana thamani yeyote", mfalme Strodgan alimjibu mwanaye Strodgento.

ITAENDELEA.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
HERDROTH

SEHEMU YA 06

Tardosen inazidi kuzidiwa sana inabidi mfalme Strodgan naye akafungiwe na Strodgento mwanaye maana walikuwa wabishi wanataka watoke wakapigane hawakuwa tayari kuona falme yao ikishambuliwa na kuhusuriwa mbele ya macho yao. Ilibidi knights wa Tardosen wawafungie wasimkose mfalme na mwanaye ambaye atarithi baada yake.

Usiku Strodgento alishuhudia kumwona baba yake akitembezewa bakora za kutosha na kile kivuli, na kitendo hichi kilifanya Strodgento azidi kuuchukia zaidi uchawi. Hii ni dalili mbaya kwa kina Herdroth kwani wakigundulika hawatosamehewa.

Falme zilizoishambulia Tardosen ni Falme ya Green Land, chini ya mfalme Corrama, Falme ya Trethe, chini ya mfalme Zamillo, na Falme ya Brondom chini ya mfalme Dunn.

Janvrey na wanawake wengine waliotekwa walipelekwa Green Land na kuteswa sana hata baadhi yao walibakwa, na kulikuwa na zamu ya kuchukuliwa mwanamke mmoja mmoja kwenda kubakwa na kila askari wa Green Land kisha kurudishwa akiwa hoi.

Mambo yote yaliyotendeka Tardosen, Herdroth ameyaona akiwa kule Crystal Land kwa kupitia kutazama zile Crystal zilizo kama mawe ya kioo, na ndipo uchawi ulipoanzia. Aliona pia jinsi Janvrey alivyotekwa kule Green Land na mambo wanayofanyiwa.

Herdroth akawafungia Dragons wake kule Crystal Land maana bado walikuwa wadogo, aliwapa nyama wakala, akawafungia humo wasitoke. Akaanza safari ya kwenda kuwashikisha adabu.

Tardosen vita vimeumana mji umeshambuliwa wamechoma moto baadhi ya maneno kila mtu amejificha askari nao baadhi yao wamekimbia kujificha kwani wameshaona hakuna kupona hapo.

Zamu ya Janvrey kubakwa ikafika, wakamchukua kwa nguvu wakimpeleka eneo la kifanyia tukio, wengine wakimpiga kofi makalioni na kuanza kumchania nguo kabla hata hawajamfikisha. Maskini Janvrey alijitahidi kufurukuta lakini hakufua dafu walimlaza chini kwa nguvu japo Janvrey alijitahidi sana kuwazuia ikashindikana, wa kwanza akaanza kujiandaa kumwingilia akampanua miguu ili amwingilie Janvrey. Ghafla alishangaa kujikuta amerushwa akabamizwa ukutani na kuanguka chini akiwa hoi. Askari sasa si ndo ikabidi wageuke wajue nini kimesababisha mwenzetu kurushwa ndipo wanakutana uso kwa uso na Herdroth, anawarusha kwa kutumia macho tu, kawabamiza wote ukutani akamchukua Janvrey, akawafungulia na wengine.

Janvrey alikuwa anaziba uso anamwonea aibu Herdroth kwa sababu Herdroth amemkuta akiwa kachaniwa nguo, Herdroth alikuwa amevaa koti lake refu limemfika magotini akalivua akamvalisha Janvrey ili kumsitiri.

Herdroth na Janvrey wanaingia kwa siri Tardosen huku vita inaendelea, Herdroth na Janvrey wanaelekea nyumbani kwa kina Janvrey ili akamfungie kwao ahakikishe usalama wake, kwa kuwa anajua ndiyo huenda akawa malkia baadaye endapo ataolewa na Strodgento mtoto wa mfalme japo kuna vikwazo vingi.

Wakiwa njiani kuelekea kwa kina Janvrey askari waliovamia walijaribu kuwashambulia Herdroth na Janvrey, Herdroth alifanya kuwafuta wote kwa kutumia macho yake tu. Janvrey alikuwa akiyaona yote hayo, akamuuliza Herdroth
"Kumbe na wewe una uchawi?"
"Ndiyo nimezaliwa nao, lakini nautumia kwa mazuri kwa kusaidia na kujisaidia mwenyewe, ila usimwambie Strodgento ataniua", Herdroth alijibu. Basi Herdroth na Janvrey wakatunziana siri. Herdroth alimfikisha Janvrey nyumbani kwao na kumwaga anaingia vitani. Basi Janvrey dirishani kwao akichungulia anaona ule uwanja waliokuwa wakipigana vita anauona kwa mbali japo anaona yanayoendelea, hivyo alijifungia akawa akitizama kwa dirishani aone Herdroth atawafanya nini.

Herdroth akawatokezea kwenye uwanja wa vita kwa juu ikiwa ni jeshi kubwa likiendelea kupambana na askari wa Tardosen waliobakia wakiwa wamezidiwa sana. Herdroth akawanyoishea mkono wake maadui akawatandika kwa radi vibaya mno. Kila mahali ni radi akawapiga jeshi lote kwa radi mpaka akahakikisha amewamaliza kabisa, wafalme wa falme hizo walipoona majeshi yao yanaangamizwa wakapanda farasi na kukimbia. Herdroth akatembea katikati ya vita kukagua kama kuna adui ammalizie. Razad pia aliona lakini hakusema ni nani aliyewasaidia, maana alikuwa akitambua Herdroth ana uchawi. Janvrey naye akiwa anachungulia dirishani kwa mbali yeye aliona radi tu akatambua Herdroth anafanya mambo.

"Ze rook ze teez kashpelie mando rinko zinto zitra zii", Herdroth aliongea spell ya kuua uchawi ya yule mama anayemtembezea bakora mfalme, kwa sababu aliyaona yote hayo akiwa kule Crystal Land.

Yule mama alipoona uchawi wake hauna nguvu akamfuata Herdroth amruhusu aendelee kulipiza kisasi. Herdroth akamkataza akamwambia mfalme akifa na Strodgento mwanaye akijua baba yake amekufa kichawi. Uchawi utapigwa marufuku kabisa hapa Tardosen, hivyo hakumruhusu kuendelea kumtesa mfalme. Vita ikaisha na mfalme akasalimika.

ITAENDELEA

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari mambo naitwa Mr Equator Nimeandika ujumbe huu kuku omba swala moja tu!
Mimi nimetengeza website ya ku share story ambayo ni http://www.equatorstory.com/
Je umekuwa ukipata tabu kupost story zako hapa?
Hili ndo suluhisho lako.
Mimi nataka nkupe nafasi ya kuwa mmoja wapo wa kwanza kutumia hii website
unda account yako na uweze kupost story yako mpya.
 
HERDROTH

SEHEMU YA 07


Ilipita miaka mitatu mizima tangu Tardosen ishinde vita yake dhidi ya falme zile tatu, falme ya Green Land, falme ya Trethe na falme ya Brondom. Kulikuwa na amani katika miji yote ya Tardosen, watu wakizifanya shughuli zao kwa furaha hku watoto nao wakicheza michezo mbalimbali wakiifurahia amani iliyotawala katika falme nzima. Hata raia wa Tardosen waliamini kuwa wao ndio raia bora katika falme bora kuliko falme zote, hivyo ikawa ni jambo la kujivunia kuwa raia wa Tardosen.

Strodgento Trosphontere pamoja na Janvrey bado waliendelea kupendana japo waliendelea kufanya siri wasigundulike kwa sababu Janvrey alikuwa kijakazi tu katika falme ya Tardosen hivyo isingewezekana mtoto wa mfalme kuoana na kijakazi kulingana na tamaduni zilizokuwepo ukizingatia ukoo wa Trosphontere ni ukoo wenye kushika madaraka na vyeo vya juu katika falme hiyo ya Tardosen na pia walikuwa na dharau, hivyo Strodgento alitambua kuwa ikijulikana kuwa anauhusiano na kijakazi ingeleta shida hivyo akafanya siri.

Herdroth naye aliwalea dragons wakawa wamezidi kukua kiasi cha kukaribia kabisa utimilifu wa ukuaji wao. Mojawapo ya malezi aliyowapatia dragons wake ni pamoja na kuwafundisha uchawi na vita, yote haya aliyafanya ili kujipa uhakika wa kukamilisha hatima yake hapo baadae. Dragon mweupe (Krozdunn) alifundishwa pia hekima ya kuishi na watu, ilhali dragon mweusi (Drementa) alifundishwa vita zaidi. Ijapokuwa drogons wote walikuwa wanaweza vita ila Drementa aliweza zaidi. Yote haya yaliwezekana kwa sababu Herdroth alikuwa ni mungu wa dragon na akawapa uwezo mbalimbali. Dragons pia walikuwa na hisia ya kutambua Herdroth alipo na kama yuko katika hali ya hatari au salama waliweza kutambua, pia walikuwa na uwezo wa kuwasiliana na Herdroth kwa umbali wowote ule kwa kutumia ufahamu tu na mawazo.

Kuna falme nyingine inaitwa Kinthor ilikuwa na Mfalme anayeitwa Billzarin na bintiye aliitwa Linetha. Billzarin na Linetha walikuja Tardosen kwa ajili ya mafungamano ya kiuchumi na kibiashara, ili kuunganisha umoja wa false hizo mbili. Walipokelewa vyema na walikubaliwa kuwa washirika, walikula na kunywa kwa siku sio chache na mazungumzo haya na yale yalifanyika baina yao.

Mezani pa chakula, meza kubwa sana ya duara waliketi familia za falme mbili, Tardosen na Kinthor. Linetha alipomtizana Strodgento alijikuta akimpenda na kuvutiwa naye. Muda ulivyozidi kusonga ndipo mfalme Billzarin alipoamua kurudi na wote alioambatana nao. Lakini Linetha yeye akapenda kubaki Tardosen ili awe karibu na Strodgento na apate nafasi ya kumvuta awe naye. Linetha akapewa chumba katika Kasri hilo la Tardosen, akapewa sehemu ya juu wanapokaa viongozi wa ufalme na watu wenye vyeo.

Linetha alijaribu kila awezalo kuhakikisha anauteka moyo wa Strodgento lakini hakuona matokeo yeyote. Alitafuta sana ni kwa sababu gani anashindwa kuuteka moyo wa Strodgento wakati anajijua kabisa kuwa yeye ni mwanamke mrembo na hana kasoro ya namna yeyote ile. Katika kujaribu kuchunguza kwa muda mrefu, siku moja aligundua siri inayomfanya asipedwe, siku hii ilikuwa ya maumivu sana kwa Linetha alipowaona Strodgento na Janvrey wakiwa wameketi kwenye garden wakicheza michezo mbalimbali ikiwemo kukimbizana, kufungana macho na kitambaa kisha kumtafuta mwenzako alipo na michezo mingine mingi wakifurahia mapenzi yao. Linetha akajaa wivu na kukimbia hadi chumbani kwake na kujifungia kisha kuanza kulia mfululizo na kwa kwikwi.

Siku moja Herdroth alimtembelea Janvrey jioni katika mji wa chini, hawa wote ni watumishi hivyo wamezoeana, wote wanakaa mji wa chini. Siku hiyo pia Linetha alikuwa ameshuka mji wa chini, alipowaona Janvrey na Herdroth aliwafuata hadi pale walipoingia nyumbani kwa kina Janvrey, Linetha akajibanza kwa dirishani kutaka kuona nini kinaendelea. Linetha alistaajabu kumwona Herdroth akiwa anamfurahisha Janvrey na kumfanya acheke muda wote kwa kuwasha mishumaa na kuizima kwa kutumia vidole na macho, na kwa vile Janvrey alitambua Herdroth ana magic, haikumpa tabu waliendelea kufurahi pamoja huku wakipiga stori mbili tatu.

Kutokana na Linetha kuwa na wivu, alienda kumpa taarifa mfalme Strodgan Trosphontere akiwa na mwanawe Stodgento Trosphontere kuwa amemwona Herdroth anatumia magic (uchawi). Mara baada ya mfalme kupewa taarifa ile alimwuliza Linetha kama ana ushaidi wa kuthibitisha, ndipo Linetha akatoa wazo la kwenda kufanya upekuzi anapoishi Herdroth. Herdroth kwa kulitambua hilo alienda kuficha vitabu vyake vya uchawi nyumbani kwa kina Janvrey.

Msako mkali ukapita nyumbani kwa wakina Jaiden na Herdroth kutafuta signal aunt vitabu vya uchawi ili iwe ushaidi, walipekua kila mahali na hawakupata chochote, taarifa zikamfikia mfalme, Linetha akaonekana mwongo, Linetha hakukubali kushindwa akatoa wazo pakapekuliwa nyumbani kwa kina Janvrey. Walipopekuwa vikapatikana vitabu vya uchawi ndipo Janvrey akakamatwa na kuwekwa sero. Strodgento alijaribu kuzuia lakini ilikuwa ni amri ya kifalme na hakuwa na namna. Kwa upande wa Linetha, ilikuwa ni siku ya furaha sana kwake huku Strodgento akiugulia machungu kwani atakuwa amempoteza ampendaye kwa sababu adhabu yake ni kunyongwa ifikapo kesho yake asubuhi.

Usiku huo Strodgento alijaribu kuongea na baba yake kumbembelea amwachilie Janvrey na kufanya siri isitangazwe katika ufalme lakini msimamo wa mfalme ulikuwa pale pale, alitamani amwambie Janvrey ni mpenzi wangu lakini aliogopa itazua balaa lingine. Baada ya kumbembeleza sana bila mafanikio alizira hata kula usiku huo, huku baba yake akimshangaa kitendo cha mwanaye kumwonea huruma kijakazi tu ambaye hana thamani yeyote.

Usiku huo huo Herdroth naye alikwenda sero kumtia moyo Janvrey. Akatumia magic yake kuwapiga usingizi walinzi kuwafanya wasikumbuke chochote, wajihisi walikuwa wanaota. Akaenda kuzungumza na Janvrey kwa marefu sana na kumtia moyo lipo tumaini la yeye kusalimika asijali. Janvrey wakati wote alikuwa akilia tu asijue la kufanya.

Kesho yake Janvrey alitolewa na kufungwa kuwekwa kwenye kinyongeo huku watu wakimsikitikia, wengine walisupport kitendo hicho ili kutokomeza uchawi Tardosen. Strodgento kutokana na vurugu alizoleta mfalme aliamuru askari wamfungie ndani akawa akuchungulia kwa dirishani. Mfalme akawa anahutubia na kutoa hukumu, ndipo Javrey akakokotwa ili akanyongwe. Wakati wakiyafanya hao ndipo umati wa watu ulistaajabu kuwaona dragons wawili wakija wakawateketeza askari waliomshika Janvrey ili kutekeleza hukumu, kisha dragon yule mweupe akambeba Janvrey na yule mweusi aliendelea kuwapulizia moto askari waliojaribu kuwashambulia. Wakambeba Janvrey na kuondoka naye pasipo kufahamika wanampeleka wapi.

ITAENDELEA
 
Back
Top Bottom