Helikopta za CCM na Chadema zaleta maafa

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,789
288,015
Helikopta za CCM na Chadema zaleta maafa
Makubo Haruni, Tarime
Daily News; Thursday,October 09, 2008 @20:02

WATU watano wamelazwa baada ya kukatwa mapanga katika ugomvi wa kugombea uwanja wa mpira mjini hapa kwa ajili ya kutua helikopta za kampeni za Chadema na CCM jana.

Vyama hivyo vinatumia helikopta katika hatua za mwisho za kampeni, Chadema ikiwa imeanza kuitumia kuanzia juzi, wakati ya CCM iliwasili kwa mara ya kwanza jana.

Watu waliokatwa mapanga ni Masanda Edward, Athuman Selemani, Mahende Daniel, Genya Sabai na Modesta Mwita ambao wamelazwa katika Zahanati ya Tarime mjini hapa.

Ugomvi huo ulitokea majira ya saa nne asubuhi uwanjani hapo baada ya wafuasi wa Chadema kutinga uwanjani kwa ajili ya kusubiri helikopta yao maarufu kama ya Mbowe, iliyokuwa itue kwa ajili ya kuwachukua viongozi kwenda kufanya kampeni. Habari kutoka uwanjani hapo zilizothibitishwa na Katibu Mwenezi wa CCM wilayani Tarime, Samwel Kiboye,

zilieleza kuwa uwanja huo ulikuwa umeombwa kwenye Tume kwa ajili ya shughuli maalumu kupokea helikopta ya CCM, na kwamba ugomvi ulitokea baina ya pande hizo mbili kutokana na wafuasi wa Chadema kugawa uwanja huo makundi mawili kwa ajili ya kutua helikopta hizo.

Hata hivyo muda mfupi kabla ya kufika kwa helikopta ya Chadema, kulitokea majibizano kati ya wafuasi hao na wanaodaiwa kuwa ni wa CCM, kuchomoa mapanga na kuanza kuwashambulia wenzao na kuwajeruhi.

Kitendo hicho kiliwavuta watu wengi na kufanya helikopta ya Mbowe isitue uwanjani hapo na rubani wake kulazimika kutafuta eneo jingine katika uwanja wa Kanisa la Anglikana ambako ilitua na kumchukua Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe na mgombea ubunge, Charles Mwera, kwenda kwenye kampeni. V

iongozi wa Chadema akiwamo Mkurugenzi wa Vijana na Mambo ya Nje, John Mnyika na mgombea udiwani wa chama hicho waliijia juu Polisi kwa kutowakamata watuhumiwa hao, licha ya wao kuwataarifu waliohusika na gari walilokimbizwa nalo.

Wakati hayo yakitokea katika kampeni za kumsaka Mbunge wa Tarime kumrithi Chacha Wangwe, aliyekuwa kada wa CCM aliyehamia Chadema amesema kuwa alifanya hivyo badala ya kusubiri kufukuzwa.

Kada huyo, Chacha Mwikwabe, ambaye aligombea ubunge wakati wa kura za maoni CCM, ameeleza kuwa kitendo cha kumtoa uongozi wa Katibu wa Umoja wa Vijana wa Mkoa na kwenda kuwa karani wa Mwenyekiti wa Taifa wa jumuiya hiyo, kingemfanya kuwa mpika chai.

Amesema ubaguzi aliofanyiwa na kuandamwa kutokana na kukemea mafisadi ndani ya CCM, kulisababisha kuchukiwa na Nchimbi na Yusuf Mkamba, hali iliyomfanya apatwe na wasiwasi na kuamua kutimka kabla ya kutimuliwa.

Ameiponda CCM kwa kile alichokieleza, kuiga Chadema kutumia helikopta katika kampeni huku akiapa kuongoza vijana wa Chadema kudai ushindi iwapo CCM itatangazwa mshindi hata ikibidi kumwaga damu.
 
Huu ni uhalifu; siyo wana CCM against wana Chadema. Tukishaweka jambo hilo clear tutaweza kuwawajijibisha watu.
 
Helikopta za CCM na Chadema zaleta maafa
Makubo Haruni, Tarime
Daily News; Thursday,October 09, 2008 @20:02

WATU watano wamelazwa baada ya kukatwa mapanga katika ugomvi wa kugombea uwanja wa mpira mjini hapa kwa ajili ya kutua helikopta za kampeni za Chadema na CCM jana.

Vyama hivyo vinatumia helikopta katika hatua za mwisho za kampeni, Chadema ikiwa imeanza kuitumia kuanzia juzi, wakati ya CCM iliwasili kwa mara ya kwanza jana.

Watu waliokatwa mapanga ni Masanda Edward, Athuman Selemani, Mahende Daniel, Genya Sabai na Modesta Mwita ambao wamelazwa katika Zahanati ya Tarime mjini hapa.

Ugomvi huo ulitokea majira ya saa nne asubuhi uwanjani hapo baada ya wafuasi wa Chadema kutinga uwanjani kwa ajili ya kusubiri helikopta yao maarufu kama ya Mbowe, iliyokuwa itue kwa ajili ya kuwachukua viongozi kwenda kufanya kampeni. Habari kutoka uwanjani hapo zilizothibitishwa na Katibu Mwenezi wa CCM wilayani Tarime, Samwel Kiboye,

zilieleza kuwa uwanja huo ulikuwa umeombwa kwenye Tume kwa ajili ya shughuli maalumu kupokea helikopta ya CCM, na kwamba ugomvi ulitokea baina ya pande hizo mbili kutokana na wafuasi wa Chadema kugawa uwanja huo makundi mawili kwa ajili ya kutua helikopta hizo.

Hata hivyo muda mfupi kabla ya kufika kwa helikopta ya Chadema, kulitokea majibizano kati ya wafuasi hao na wanaodaiwa kuwa ni wa CCM, kuchomoa mapanga na kuanza kuwashambulia wenzao na kuwajeruhi.

Kitendo hicho kiliwavuta watu wengi na kufanya helikopta ya Mbowe isitue uwanjani hapo na rubani wake kulazimika kutafuta eneo jingine katika uwanja wa Kanisa la Anglikana ambako ilitua na kumchukua Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe na mgombea ubunge, Charles Mwera, kwenda kwenye kampeni. V

iongozi wa Chadema akiwamo Mkurugenzi wa Vijana na Mambo ya Nje, John Mnyika na mgombea udiwani wa chama hicho waliijia juu Polisi kwa kutowakamata watuhumiwa hao, licha ya wao kuwataarifu waliohusika na gari walilokimbizwa nalo.

Wakati hayo yakitokea katika kampeni za kumsaka Mbunge wa Tarime kumrithi Chacha Wangwe, aliyekuwa kada wa CCM aliyehamia Chadema amesema kuwa alifanya hivyo badala ya kusubiri kufukuzwa.

Kada huyo, Chacha Mwikwabe, ambaye aligombea ubunge wakati wa kura za maoni CCM, ameeleza kuwa kitendo cha kumtoa uongozi wa Katibu wa Umoja wa Vijana wa Mkoa na kwenda kuwa karani wa Mwenyekiti wa Taifa wa jumuiya hiyo, kingemfanya kuwa mpika chai.

Amesema ubaguzi aliofanyiwa na kuandamwa kutokana na kukemea mafisadi ndani ya CCM, kulisababisha kuchukiwa na Nchimbi na Yusuf Mkamba, hali iliyomfanya apatwe na wasiwasi na kuamua kutimka kabla ya kutimuliwa.

Ameiponda CCM kwa kile alichokieleza, kuiga Chadema kutumia helikopta katika kampeni huku akiapa kuongoza vijana wa Chadema kudai ushindi iwapo CCM itatangazwa mshindi hata ikibidi kumwaga damu.


Hawa wamejitajidi kuirembe hii habari lakini wameshindwa, inaonyesha wazi CCM ndio wamewakata Chadema mapanga.
 
Hivi hao Polisi 400 wanafanya nini Tarime, it looks like hawana uwezo wa kuzuia jambo lolote; wanashindwa kuzuia mawe, wanashindwe kuzuia mapanga, wanashindwa kuzuia risasi, so what use are they?
 
Huu ni uhalifu; siyo wana CCM against wana Chadema. Tukishaweka jambo hilo clear tutaweza kuwawajijibisha watu.

Mkjj, kinachonisikitisha zaidi na kunitia hasira za hali ya juu wakati haya yote yanaendelea huko Tarime sijasikia kiongozi hata mmoja akikemea haya ya kukatana mapanga Watanzania kwa Watanzania. Halafu bila aibu hata haya wanapita huku na huko kujinadi kama wao ni viongozi wa Watanzania.

Utakuwaje kiongozi wa Watanzania unaona wananchi wako wanakatana mapanga na wewe umekaa kimya kama hakuna lolote lilitokea. Wameweka mbele maslahi yao binafsi na kusahau yale ya Tanzania kama nchi.
 
Hivi hao Polisi 400 wanafanya nini Tarime, it looks like hawana uwezo wa kuzuia jambo lolote; wanashindwa kuzuia mawe, wanashindwe kuzuia mapanga, wanashindwa kuzuia risasi, so what use are they?

Hao polisi ni kitengo cha CCM hivyo wako pale kutii amri za viongozi wa CCM na kuhakikisha CCM inaibuka kidedea kwa hali yoyote ile.
 
Hao polisi ni kitengo cha CCM hivyo wako pale kutii amri za viongozi wa CCM na kuhakikisha CCM inaibuka kidedea kwa hali yoyote ile.

Inaonekana viongozi wetu wamejisahau sana na hawataki kujifunza kutokana na historia. Hawajui kuwa kuna siku wananchi wakichoka na kuwatoa madarakani kwa sanduku la kura au hata nguvu ikibidi watatakiwa waende mahakamani wakajibu yote wanayowatendea wananchi maskini kwa sasa.


Viongozi wetu wamesahau yaliyowakuta kina Nicolae Ceaucescu na wengine wengi kwenye historia....Wao badala ya kujirudi na kutumikia wananchi wanalazimisha kila kitu kama wao wanavyotaka ili tu waendelee kuwa madarakani, hawajui kuwa kizazi cha watanzania waoga kinakwisha pole pole na kuja kizazi kipya chenye muono tofauti.
 
Helikopta za CCM na Chadema zaleta maafa
Makubo Haruni, Tarime
Daily News; Thursday,October 09, 2008 @20:02

WATU watano wamelazwa baada ya kukatwa mapanga katika ugomvi wa kugombea uwanja wa mpira mjini hapa kwa ajili ya kutua helikopta za kampeni za Chadema na CCM jana.

Vyama hivyo vinatumia helikopta katika hatua za mwisho za kampeni, Chadema ikiwa imeanza kuitumia kuanzia juzi, wakati ya CCM iliwasili kwa mara ya kwanza jana.

Watu waliokatwa mapanga ni Masanda Edward, Athuman Selemani, Mahende Daniel, Genya Sabai na Modesta Mwita ambao wamelazwa katika Zahanati ya Tarime mjini hapa.

Ugomvi huo ulitokea majira ya saa nne asubuhi uwanjani hapo baada ya wafuasi wa Chadema kutinga uwanjani kwa ajili ya kusubiri helikopta yao maarufu kama ya Mbowe, iliyokuwa itue kwa ajili ya kuwachukua viongozi kwenda kufanya kampeni. Habari kutoka uwanjani hapo zilizothibitishwa na Katibu Mwenezi wa CCM wilayani Tarime, Samwel Kiboye,

zilieleza kuwa uwanja huo ulikuwa umeombwa kwenye Tume kwa ajili ya shughuli maalumu kupokea helikopta ya CCM, na kwamba ugomvi ulitokea baina ya pande hizo mbili kutokana na wafuasi wa Chadema kugawa uwanja huo makundi mawili kwa ajili ya kutua helikopta hizo.

Hata hivyo muda mfupi kabla ya kufika kwa helikopta ya Chadema, kulitokea majibizano kati ya wafuasi hao na wanaodaiwa kuwa ni wa CCM, kuchomoa mapanga na kuanza kuwashambulia wenzao na kuwajeruhi.

Kitendo hicho kiliwavuta watu wengi na kufanya helikopta ya Mbowe isitue uwanjani hapo na rubani wake kulazimika kutafuta eneo jingine katika uwanja wa Kanisa la Anglikana ambako ilitua na kumchukua Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe na mgombea ubunge, Charles Mwera, kwenda kwenye kampeni. V

iongozi wa Chadema akiwamo Mkurugenzi wa Vijana na Mambo ya Nje, John Mnyika na mgombea udiwani wa chama hicho waliijia juu Polisi kwa kutowakamata watuhumiwa hao, licha ya wao kuwataarifu waliohusika na gari walilokimbizwa nalo.

Wakati hayo yakitokea katika kampeni za kumsaka Mbunge wa Tarime kumrithi Chacha Wangwe, aliyekuwa kada wa CCM aliyehamia Chadema amesema kuwa alifanya hivyo badala ya kusubiri kufukuzwa.

Kada huyo, Chacha Mwikwabe, ambaye aligombea ubunge wakati wa kura za maoni CCM, ameeleza kuwa kitendo cha kumtoa uongozi wa Katibu wa Umoja wa Vijana wa Mkoa na kwenda kuwa karani wa Mwenyekiti wa Taifa wa jumuiya hiyo, kingemfanya kuwa mpika chai.

Amesema ubaguzi aliofanyiwa na kuandamwa kutokana na kukemea mafisadi ndani ya CCM, kulisababisha kuchukiwa na Nchimbi na Yusuf Mkamba, hali iliyomfanya apatwe na wasiwasi na kuamua kutimka kabla ya kutimuliwa.

Ameiponda CCM kwa kile alichokieleza, kuiga Chadema kutumia helikopta katika kampeni huku akiapa kuongoza vijana wa Chadema kudai ushindi iwapo CCM itatangazwa mshindi hata ikibidi kumwaga damu.

Huyu Mwikwabe anashangaza sana, kwake hakuna kushindwa ni kushinda tu. Hizi sera za kumwaga damu hazitawafikisha kokote Chadema. Now I understand kwanini alitoka CCM kwake yeye madaraka ni lazima.

Hiki ni kitendo cha kukemewa na kila mpenda amani. Maneno haya yana hatarisha uwepo wa amani na ni kitanzi kwa demokrasia ya kweli. Lakini wana chadema wa jf wamelifumbia macho hili very sad...
 
Huyu Mwikwabe anashangaza sana, kwake hakuna kushindwa ni kushinda tu. Hizi sera za kumwaga damu hazitawafikisha kokote Chadema. Now I understand kwanini alitoka CCM kwake yeye madaraka ni lazima.

Hiki ni kitendo cha kukemewa na kila mpenda amani. Maneno haya yana hatarisha uwepo wa amani na ni kitanzi kwa demokrasia ya kweli. Lakini wana chadema wa jf wamelifumbia macho hili very sad...

Wewe mbona umefumbia macho hao makada wa CCM kuwashambulia watu kwa mapanga,acha unazi kijana
 
Back
Top Bottom