Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 92,231
- 113,598
Moja ya malalamiko ya kipumbavu kabisa yaliyokuwepo enzi za utawala wa Rais Magufuli ni kuwa eti hela hazikuwepo mtaani.
Sijui ni lini hasa Tanzania hii ambapo hela zilikuwepo bwerere mtaani! Kwa sababu, Tanzania ni nchi maskini. Ni nchi ya ulimwengu wa tatu.
Vipato vya wananchi wake ni vya chini sana. Si nchi nyingi ambazo nchi yetu imezipita kwa vipato vya wananchi.
Na tumekuwa nchi ambayo wananchi wake ni wa kipato cha chini tokea tuwe taifa na nina uhakika kabla hata ya kuwa taifa.
Lakini katika utawala uliopita tuliaminishwa mzunguko wa hela umebanwa na hivyo kupelekea kutokea upungufu wake mtaani/ mitaani.
Baada ya kumpata huyu Rais wetu mpya, aliye mpole na msikivu, mwenye kuongea Kiingereza kizuri kabisa 😉, tukaambiwa sasa mzunguko wa hela utarudi na hela zitakuwepo mtaani kama ilivyokuwa kabla ya kuja kwa dikteta Magufuli!
Sasa niaje raia? Mama kesharudisha hayo mahela mitaani?
Kama hayo mahela yamesharudi mitaani kwa nini mnalialia kuhusu vijitozo vya shilingi 100 mtumapo hela kwenye Em Pesa?
Kwa mnaojua hayo mahela yalipo, msiwe wachoyo. Tauambieni na sie wengine tuje tuyaokote bana.
Vilivyo vizuri kuleni na sie ndugu zenu.
Tuendelee kuupiga mwingi 😉.
Sijui ni lini hasa Tanzania hii ambapo hela zilikuwepo bwerere mtaani! Kwa sababu, Tanzania ni nchi maskini. Ni nchi ya ulimwengu wa tatu.
Vipato vya wananchi wake ni vya chini sana. Si nchi nyingi ambazo nchi yetu imezipita kwa vipato vya wananchi.
Na tumekuwa nchi ambayo wananchi wake ni wa kipato cha chini tokea tuwe taifa na nina uhakika kabla hata ya kuwa taifa.
Lakini katika utawala uliopita tuliaminishwa mzunguko wa hela umebanwa na hivyo kupelekea kutokea upungufu wake mtaani/ mitaani.
Baada ya kumpata huyu Rais wetu mpya, aliye mpole na msikivu, mwenye kuongea Kiingereza kizuri kabisa 😉, tukaambiwa sasa mzunguko wa hela utarudi na hela zitakuwepo mtaani kama ilivyokuwa kabla ya kuja kwa dikteta Magufuli!
Sasa niaje raia? Mama kesharudisha hayo mahela mitaani?
Kama hayo mahela yamesharudi mitaani kwa nini mnalialia kuhusu vijitozo vya shilingi 100 mtumapo hela kwenye Em Pesa?
Kwa mnaojua hayo mahela yalipo, msiwe wachoyo. Tauambieni na sie wengine tuje tuyaokote bana.
Vilivyo vizuri kuleni na sie ndugu zenu.
Tuendelee kuupiga mwingi 😉.