HOJA BoT inaona freshi Watu kuuza chenji mtaani?

HOJA BoT inaona freshi Watu kuuza chenji mtaani?

Hoja ya Mdau inayopendekeza maboresho au mabadiliko ndani ya jamii, inayotakiwa kuangakiwa kwa mapana na Mamlaka husika

Club Mate

Member
Joined
Aug 1, 2025
Posts
25
Reaction score
86
Wadau, habari zenu.

Simaanishi kwamba biashara ya kuuza chenji ipigwe marufuku au wauzaji washughulikiwe. Hapana. Lakini ukweli ni kwamba, uwepo wa watu wanaofanya biashara ya kuuza noti ndogo na sarafu mtaani ni kiashiria tosha cha uhaba wa chenji kwenye mzunguko. Ni wazi kuwa wafanyabiashara wadogo, makonda wa daladala, bodaboda na madereva wa bajaji wamekosa sehemu rasmi za kupata chenji.

Ukichanganya hili na ile tabia ya wafanyabiashara wetu kutegemea mteja ndiye atafute chenji (aje na hela kamili), huu udhaifu wa BoT kwenye mzunguko wa pesa unageuka kuwa kero kubwa sana ya kila siku.

Zaidi ya hapo, ukosefu wa chenji unasababisha upandaji wa bei usio na mantiki pale gharama za maisha zinapopanda. Kwa mfano, inawezekana kupanda kwa bei ya mafuta kumeongeza gharama ya ruti ya bodaboda kwa Tsh. 200 tu, lakini kwa kisingizio cha "hakuna chenji," bei inapandishwa kabisa kwa Tsh. 500. Hata chapati mtaani kutoka Tsh. 500 inaruka hadi 1,000 kwa visingizio hivi hivi.

Hata kwenye ma-supermarket wanatumia mwanya huu huu. Badala ya kukupa chenji yako, wanaona ni bora wakupe pipi.

Mabenki na mawakala nao wanachangia sana hii shida. Mara nyingi ukienda ATM unatoa noti za 10,000 tu. Hivyo, pesa nyingi zinazozungushwa mtaani na wafanyakazi zinakuwa ngumu sana kuzitumia kwenye manunuzi ya bidhaa au huduma ndogo ndogo.

BoT inabidi ishughulikie hii ishu haraka sana. Imekuwa kero kubwa, na kusema ukweli ni aibu kwa Benki Kuu kuona hela yao inauzwa kwa faida mtaani bila wao kuchukua hatua yoyote ya msingi kuhakikisha chenji inapatikana kote.

Nawasilisha.
 
Ukweli ni kuwa sio kuwa kuna uhaba wa chenji.

Wanao chukua pesa Bank hawachukui sarafu. Na hakuna anayependa kutembea na silver zinachosha

So Kinachotokea ni kuwa hizo silver zinakosa rotation inayo eleweka.

Ni sawa kabisa ziuzwe
 
Sahivi mpaka wa masai wanauza chenchi.
Mazoea ya kiswahili TU, wanauza je hela , Wana vibali vya kufanya hivyo ? .

Na wale wanao nunua pesa , noti zilizo chakaa je .
Nani kawapa vibali vya kununua pesa chakavu ?

Ni mazoea TU ya kiswahili yenye madhara makubwa kwa jamii
 
Daaah usilo lijua nikama ucku wa GIZA. Hii ni bznes ya wafanya kazi wa B.O.T kiongozi. Wauza chenji wananguvu kuliko serikali. Hii inafanywa sana n mtoto w aliewahi kua waziri kipenzi wa Benja kwenye awamu zake zote. Rest in peace kiti.
Kazi ni kipimo cha utu
 
Wadau, habari zenu.

Simaanishi kwamba biashara ya kuuza chenji ipigwe marufuku au wauzaji washughulikiwe. Hapana. Lakini ukweli ni kwamba, uwepo wa watu wanaofanya biashara ya kuuza noti ndogo na sarafu mtaani ni kiashiria tosha cha uhaba wa chenji kwenye mzunguko. Ni wazi kuwa wafanyabiashara wadogo, makonda wa daladala, bodaboda na madereva wa bajaji wamekosa sehemu rasmi za kupata chenji.

Ukichanganya hili na ile tabia ya wafanyabiashara wetu kutegemea mteja ndiye atafute chenji (aje na hela kamili), huu udhaifu wa BoT kwenye mzunguko wa pesa unageuka kuwa kero kubwa sana ya kila siku.

Zaidi ya hapo, ukosefu wa chenji unasababisha upandaji wa bei usio na mantiki pale gharama za maisha zinapopanda. Kwa mfano, inawezekana kupanda kwa bei ya mafuta kumeongeza gharama ya ruti ya bodaboda kwa Tsh. 200 tu, lakini kwa kisingizio cha "hakuna chenji," bei inapandishwa kabisa kwa Tsh. 500. Hata chapati mtaani kutoka Tsh. 500 inaruka hadi 1,000 kwa visingizio hivi hivi.

Hata kwenye ma-supermarket wanatumia mwanya huu huu. Badala ya kukupa chenji yako, wanaona ni bora wakupe pipi.

Mabenki na mawakala nao wanachangia sana hii shida. Mara nyingi ukienda ATM unatoa noti za 10,000 tu. Hivyo, pesa nyingi zinazozungushwa mtaani na wafanyakazi zinakuwa ngumu sana kuzitumia kwenye manunuzi ya bidhaa au huduma ndogo ndogo.

BoT inabidi ishughulikie hii ishu haraka sana. Imekuwa kero kubwa, na kusema ukweli ni aibu kwa Benki Kuu kuona hela yao inauzwa kwa faida mtaani bila wao kuchukua hatua yoyote ya msingi kuhakikisha chenji inapatikana kote.

Nawasilisha.
Biashara nyingi wanaojitambua wanahitaji chenji huwa wanaenda bank asubuhi kutafuta chenji. Pia sio kila mtu anaweza kwenda bank kutafuta chenji watu wameona fursa.
 
Coins chache mtaani, unaenda dukani unataka maji ya 600 unampa 1000 anasema chenchi hana, na una kiu ! Itakubidi ununue na kitu kingine mfano pipi ili walau upate maji yako....tayari unnecessary cost
 
Kipindi kile tamasha la utumishi linafanyika Dar es salaam niliwauliza BOT kama hawajui madhara ya kuuza chenji mmoja akanibishia lakini mwenzake akanikubalia kweli chenji zinauzwa.
Hapo ndio unakubaliana na Magufuli BOT wamejaa madokta(PHD) wengi lakini hakuna wanachojua kuhusu uchumi.
 
Back
Top Bottom