Hela ya Tanzania yazidi kuporomoka!

3) Tuache bajeti tegemezi, tuache kutegemea wafadhili

4) Tufungue viwanda vingi sisi wenyewe, tujifunze ku-export ready made material, na siyo rawa materials,

5) Wananchi wanunue bidhaa za ndani , zilizotengenezwa humu humu, baada ya point ya nne kufanyika. viwanda vya ndani vitengenezewe mazingira mazuri ya kushindana na vya nje, to my surprise serikali wanapigana usiku na mchana kuweka mazingira mazuri kwa wageni!

6) point ya 4,5 ikishafikiwa, tuhamasishe matumizi ya fdha yetu ambayo inacirculate humu humu, kiasi ambacho itaongeza thamani ya fedha nje ya nchi.

inatokana na kuwa we have no say about our economy! piga ua!

when you talk about donors, katika nchi yenye kila sababu ya kuendelea yenye, maliasili za kumwaga, when you talk about them, you are confirming that, all these issues of inflation, or whatever may be Tanzania is not a country to talk about! we are exporting raw materials mkuu, thats wrong very very wrong.

waberoya

Waberoya:

Vitu ulivyosema vinawezekana kabisa kuvifanya lakini vinaweza kusababisha Social Upheaval kitu ambacho wanasiasa na nchi zilizoendelea hawataki kukiona kinatokea.

Kama bajeti yetu inategemea misaada kwa asilimia 40, ina maana wahisani wakiacha kutoa misaada basi serikali inashindwa kulipa mishahara ya wafanyakazi wake na kutoa huduma zingine kwa jamii.

Na serikali kushindwa kulipa mishahara kutaambatana na vurugu za kijamii ambazo zinaweza kufanya serikali ianguke na kusababisha matatizo yenye mfano wa Somalia.

Hakuna mwanasiasa ambaye anataka kuongoza nchi huku kukiwa na vurugu. Hata Nyerere mwenyewe hakuweza kukwepa misaada maana bila ya misaada hakuna ambaye angempa sikio la siasa za ujamaa.

Kwa mtaji huo haitoshi kusema kuwa sisi tuna maliasili za kutosha. Kinachotakiwa ni Innovative Approaches ya nchi kutoka kwenye misaada na madeni bila kusababisha matatizo ya kijamii.

Katika post yangu moja nilisema kipindi cha sasa ni kizuri kujifunza na kupata expertise kwa sababu tunaona jinsi gani nchi kama Marekani inavyoweza kutumia tools za kiuchumi kutatua matatizo yake. Hizi tools ni Innovative Approaches. Kwa mfano wana bail out makampuni, wanamwaga stimulus package baadaye wataingia kwenye fiscal responsibility.

I am curious na kitu kimoja kuhusu matatizo ya uchumi dunia yanayotokea sasa. Je watanzania tunawatizama wenzetu wanavyopambana na matatizo yao na wakifanikiwa tuendelee kuwaomba misaada au na sisi tunajifunza vitu fulani?

Hypothetically ningependa mtu atueleze katika kipindi cha miaka mitano zitumike Innovative Approaches zipi kuondoa misaada bila kushusha standard of living ambayo watanzania wanayo sasa.
 
Maswali yamekwenda chuo haya Mwanjelwa. Tuanze moja moja basi.



Fedha kuwa na thamani kuliko dola kamwe haina maana kwamba uchumi wa nchi umekuwa au unakuwa. Kwanini? Kwasababu thamani ya fedha ni kiashirio tu cha mwenendo wa shughuli za uchumi katika kipindi husika. Thamani ya fedha ya nchi, inaonyesha tu, kwa mfano, mtu anavyotembea kwa wakati husika, haionyeshi mtu huyo kafikia wapi. Uchumi mzuri unapimwa kwa kuangalia ongezeko la pato la taifa (GDP).



Pato la taifa (GDP) la uchumi uliowazi kama Tz linaundwa na factor kuu 4. Hizi ni national consumption, investment, government expenditure, na tofauti kati ya import na export). Shilingi yetu iki-appreciate (ikapanda thamani), manake wanunuzi wa pamba yetu waliokuwa wananunua kilo 100 kwa dola moja mwanzoni wanapata kilo 80 kwa dola moja sasa. Kwahiyo kama Tz tunauwezo wa kuendelea kuzalisha na kuuza kilo 100 baada ya appreciation, tunapata faida. Kwa kesi hii appreciation inasaidia uchumi.

Tatizo linakuja pale wauzaji wengi wa pamba wanapogongana na wauzaji wakibongo. Mfano kama shilingi yetu ime-appreciate wakati shilingi ya Uganda na Kenya bado iko constant, wanunuzi wa pamba wataacha kununua pamba yetu na badala yake watanunua pamba ya Kenya au Uganda, mana huko dola yao moja itaendelea kununua kilo 100, badala ya 80 Tz. Kwa kesi hii appreciation imefukuza wanunuzi wa exports zetu, na haisaidii uchumi. Ubaya wa appreciation unaweza pia kuja endapo wanunuzi wa pamba wamegundua bidhaa ya bei nafuu inayofanya kazi kama (au angalau) pamba yetu; kahawa ni mfano mzuri hapa..kugundulika kwa kahawa inayotengenezwa mahabara kunafanya wanunuzi wa kahawa yetu wanywe kahawa ya ya bei poa ya mahabara pale shilingi yetu inapo appreciate.



Ikumbukwe kwamba sio mungu anayepanga thamani ya fedha. Zipo nchi ambazo kwa makusudi zimeamua kupanga thamani ya ela yao. Kama waswahili wanavyosema kupanga ni kuchagua, nchi inapopanga thamani ya ela lazima ikubali hasara za uamuzi huu. Thamani ya fedha ni sawa tu na bei za bidhaa mbalimbali, katika uchumi huru bei ya chungwa lazima iwiane na gharama za kuzalisha chungwa na utayari wa mnunuzi kununua kwa bei hiyo (demand na supply). Chungwa likiuzwa bei ambayo mnunuzi hayuko tayari kununua litaoza, na likiuzwa bei ya chini kuliko gharama la kulizalisha halitazalishwa. Kwa hiyo nchi inapopanga thamani ya ela yake ina risk efficiency katika makuzi ya uchumi wake. Kadhalika nchi inaopoachia soko lirekebishe bei linayakubali mawimbi ya supply na demand...mawimbi ambayo sio mazuri nyakati zote. Zipo nchi ambazo zinaacha soko ipange thamani ya fedha na kuingilia tu pale mawimbi ya supply na demand yanapoharibu shughuli za uchumi kwa muda mrefu kiasi cha kuhatarisha.

Hitimisho, (i) appreciation kiuchumi inatuonyesha mwenendo wa bihashara/shughuli za uchumi, sio kipimo cha kukuwa kwa uchumi (GDP ndio kipimo cha kukuwa kwa uchumi); (ii) appreciation yaweza kuwa mzuri na mbaya kutegemea na mambo mengi kama vile umuhimu wa exports kwa wanunuzi, ubora wa exports katika soko, uwingi wa wauzaji wa export hiyo, kuwapo au kutowapo kwa bidhaa mbadala (a substitute good?), uwezo wa nchi kuzalisha exports...nk. (iii) nchi inaweza kujipangia thamani ya fedha yake, ili mradi tu inakubali hasara zake.


Asante sana ndugu. Nimekupata kwa kiasi changu kabisa. Kuhani na Mtindio wakitua pua zao tu hapa, nawakata shule ya nguvu!
 
Asante sana ndugu. Nimekupata kwa kiasi changu kabisa. Kuhani na Mtindio wakitua pua zao tu hapa, nawakata shule ya nguvu!

Kwa nini unasubiri ``wakitua pua zao`` hao wachangiaji wawili tu katika jamvi la watu maelfu?

Walikutenda nini hao jamaa?
 
Kwa nini unasubiri ``wakitua pua zao`` hao wachangiaji wawili tu katika jamvi la watu maelfu?

Walikutenda nini hao jamaa?

Hamjanitenda, hamuwezi kwa namna yoyote!. Mnahitaji sana elimu ili muendelee kuishi kwa matumaini muda mrefu zaidi. Nami nawajali kwa namna hiyo.
 
Back
Top Bottom