Hela ya mwanamke huliwa na nani?

Hawa jamaa wana ratiba nyingi mpaka basi! Wakati mwingine tuwaache tu. Kwanza ni viumbe wenye tamaa sana! Yaani akiona kitu halafu akakipenda, basi ni lazima tu atakinunua. Wana mahitaji mengi sana kuliko sisi wanaume! Mfano kwenda saluni, kupaka rangi na kusafisha kucha, nk.
Tuishi nao kwa akili au tuishi nao mbali?!
 
Hata wewe mkuu muda wa kujisifia bado haujafika.

Ungeishi ndani ya ndoa walau miaka 10 ndiyo uje utoe ushuhuda wa uliyoyatoa sasa!

Mitego na vishawishi vya ndoa ni vingi kuliko unavyovielewa wewe.

Kupewa pass word pamoja na kukabidhiwa fuba kabla ya kufunga ndoa vyaweza kuwa ni vishawishi vya kukuvutia uingie kichwa kichwa kwa furaha kabla rangi halisi haujaoneshwa.

Waulize wazoefu, kila mwanamke kabla ya kufunga ndoa, bila kujali umeishi naye kihawara muda gani, ni mjanja sana kwa kuonesha unyenyekevu na ushawishi akielewa kuwa kipindi hicho hajawa na mamlaka kamili juu yako.

Mkiisha kufunga ndoa ndiyo hujivua gamba na kuonesha sura na rangi yake halisi.
Inategemea na mwanaume unavyojiweka. Maisha ni mwandiko unaandika wengine wanakusoma

Sent from my VF-795 using JamiiForums mobile app
 
Wakuu poleni na majukumu ya siku nzima,

Asilimia kubwa ya wanawake hawalipi Kodi hawalipi ada za watoto wala bili ya aina yeyote ile japo kazi wanafanya.

Mbali na mahitaji muhimu ya nyumbani kuhudumiwa kwa pesa ya mwanaume, pia pesa ya saluni ya mwanamke inatoka mfukoni kwetu sisi wanaume.

Je pesa zao huwa wanapeleka wapi..?
Ingekuwa vizuri kama ungewauliza hao hao unaowajua. Maana kwa uzoefu wangu, wapo wengi wanaofanya hayo uliyosema hawafanyi mbali na kuwatunza watoto wa mama. Unadhani mashuga mami hawatumii siyo?
 
Wakuu poleni na majukumu ya siku nzima,

Asilimia kubwa ya wanawake hawalipi Kodi hawalipi ada za watoto wala bili ya aina yeyote ile japo kazi wanafanya.

Mbali na mahitaji muhimu ya nyumbani kuhudumiwa kwa pesa ya mwanaume, pia pesa ya saluni ya mwanamke inatoka mfukoni kwetu sisi wanaume.

Je pesa zao huwa wanapeleka wapi..?
Wanahonga wanaume wanaowapenda wao huko mitaani, watawapangia nyumba na kuwanunulia magari ili mradi tu naye ajisikie ana miliki serengeti boy. Si mnamuona Mama yake Diamond anavyotamba na mtoto wake, kila kukicha anambandika mitandaoni wakilishana mimate na kushikana makalio yaliyochoka huku akimtambia baba wa kambo wa Diamond.
 
Wakuu poleni na majukumu ya siku nzima,

Asilimia kubwa ya wanawake hawalipi Kodi hawalipi ada za watoto wala bili ya aina yeyote ile japo kazi wanafanya.

Mbali na mahitaji muhimu ya nyumbani kuhudumiwa kwa pesa ya mwanaume, pia pesa ya saluni ya mwanamke inatoka mfukoni kwetu sisi wanaume.

Je pesa zao huwa wanapeleka wapi..?
Muhimu kwenye ndoa ni COMMUNICATION. Kaa na mkeo mjadili na mgawane majukumu.
 
Vikoba ,harusi ,ubarikio,harusi ,sendoff ,safe,kukopesha wasiolipa,kula chips mayai mishikaki iliyopikwa side,mania,Adam nk,wachungaji,mitume na manabii,watengeneza kucha na waosha miguu ,kujenga kwao na kusaidia ndg sake nk nk
 
Tatizo la watu wakati wa kuanzisha mahusiano mnasikiliza sana watu.

Mara demu mmwenye tako,

Mara pisi kali,

Mara sijui nini?

Mwisho wa siku unaoa slay queen halafu unakuja kulalamika kindezi humu.

Mimi demu wangu kanipa mpaka password na mimi ndio naenda kutoa pesa.

Naal ameshasema tukianza kuishi wote, pesa zake zitakuwa za kula na zangu za kufanya mambo mengine.

Vijana acheni kujiingiza kwenye mahusiano ya kuridhisha walimwengu.
Nawe usisahau kumpa pw yako, ila utakapo lizwa kwa kukombwa hela yote kwenye account na akaenda kuolewa na mwingine usiishie kulia, lete mrejesho humu jf.
 
Hawa jamaa wana ratiba nyingi mpaka basi! Wakati mwingine tuwaache tu. Kwanza ni viumbe wenye tamaa sana! Yaani akiona kitu halafu akakipenda, basi ni lazima tu atakinunua. Wana mahitaji mengi sana kuliko sisi wanaume! Mfano kwenda saluni, kupaka rangi na kusafisha kucha, nk.

Ni watoaji wazuri wa sadaka kwa Manabii na Wachungaji uchwara ukilinganisha na sisi wanaume! Wana vikundi vingi vya kukopeshana na kusaidiana wenyewe kwa wenyewe!

Ni wepesi sana kwenye kusaidia familia zao mfano baba na mama zao, ndugu zao, nk zitokeapo changamoto za kifedha, au shida fulani nyumbani ukilinganisha na sisi.

Wanawake wengi hupenda kuishi na akiba ya fedha ndani ili ziwasaidie wakati changamoto zinapotokea nyumbani, tofauti kabisa na sisi wanaume ambao wengi hatupendi kuweka akiba. Hivyo unaweza kushangaa hela iko wapi, kumbe ameweka akiba sehemu ambayo kamwe mwanaume huwezi kuigundua.

Hao ndiyo wanawake bhana tunao takiwa kuishi nao kwa akili sana.
Kutoa sadaka hawajambo, hatoi kwa kupanga, bali kwa kuangalia jirani katoaje!
 
Wakuu poleni na majukumu ya siku nzima,

Asilimia kubwa ya wanawake hawalipi Kodi hawalipi ada za watoto wala bili ya aina yeyote ile japo kazi wanafanya.

Mbali na mahitaji muhimu ya nyumbani kuhudumiwa kwa pesa ya mwanaume, pia pesa ya saluni ya mwanamke inatoka mfukoni kwetu sisi wanaume.

Je pesa zao huwa wanapeleka wapi..?
Mtoboa Siri aliyasema sana haya. Wanaume tuna mioyo ya huruma. Tukiwa na motokaa kinadada twawabeba. Wao hata mvua inanyesha atakupita bila kujali. Kwa kweli wema wetu ni hasara. Mchana halo bebi hebu twende kwa lunch. Hata twendapo sinema ni sisi tu ndo tunatoboka. Hadi leo haijulikani ni lini hao wenzetu watatoboka!
 
Nawe usisahau kumpa pw yako, ila utakapo lizwa kwa kukombwa hela yote kwenye account na akaenda kuolewa na mwingine usiishie kulia, lete mrejesho humu jf.
Endelea kuishi na matatizo ambayo hayajakutokea.
 
Back
Top Bottom