Heche Vijana wanahitaji ajaira si kubeti

Heche Vijana wanahitaji ajaira si kubeti

1000482441.jpg
 
Tayar katupiga marufuku kumpigia kura kwa ujinga hu0
 
Hapo yuko sahihi, kutia watu umasikini sio kazi hii kamari athari yake ni kama muuza madawa ya kulevya
 
Ndio maana hatutawapigia kura sisi tunataka kubeti, tumeridhika na hali ya maisha yetu 😏
 
Betting zimeajiri watu Wanalipwa mishahara na wanalipa kodi iweje sasa isiwe ajira
 
Huku kwenye kuchana mikeka angeachana napo kabisa hii ni ajira kamili
 
Hivi Heche anajua Katiba ya Tanzania na Uhuru wa Kufanya Kazi yoyote ili mradi hauvunji Katiba ya nchi? Au ndio wanataka kuleta Udikteta

Mtu kama Makalla (Amos Makalla, Katibu Mwenezi wa CCM Taifa) ambaye anawasababisha mnakuwa masikini, utajiri wenu wanawagawia wachina na waarabu anakuja kuwaambia Heche, anapinga betting. Mimi ninataka betting isifanyike, mmiliki uchumi wa nchi hii kwasababu wote mnaweza kuwa matajiri, wote mnaweza kufanya kazi ya kuzalisha.

Wakati hawa watu (CCM) wanawaambia vijana mfanye betting si kulikuwa na kiwanda cha kukata almasi, si kilikuwa kinawaajiri nyie, wameua kile kiwanda kisiwaajiri nyie halafu wanawaambia mkafanye betting. Uhimilivu wa betting ni nini? Ukizeeka utapata mafao kwenye betting? Ukiwa umejiriwa ukizeeka si utapata mafao? Makalla anaongea kitu gani huyo?

Haya magodauni yaliyopo hapa nchini si ya National Milling? National Milling iliajiri watu wa Iringa, halafu nyinyi wanawaambia mfanye betting. Hawa watu wanawaambia vijana wa Tanzania wafanye betting wakati wanaagiza kutoka nje ngano ya Shilingi bilioni 504. Vijana wa Tanzania wanachohitaji uwape trekta, uwape mashine za kuvuna, mbegu, soko, waunde vikundi, waingie kulima ngano, uwape soko wauze wawe matajiri siyo unawaambia kwamba wafanye betting wakati unaagiza ngano kutoka Ukraine, unachukua fedha za ndani unapeleka Ukraine kuagiza ngano"
Shida hujamulewa M/mwenyekiti ,mtu abet kama sehem ya burudani ila sio kama mfumo wa ajira rasmi
 
Back
Top Bottom