Heche azuiwa kushiriki kipindi cha Cafe Talk

Heche azuiwa kushiriki kipindi cha Cafe Talk

View attachment 3377709

Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA (Bara), John Heche amezuiwa kushiriki kipindi cha Cafe Talk kitakachofanyika kesho Juni 22, 2025 jijini Dar es Salaam.

Taarifa kutoka kwa wanandaaji wa kipindi hicho zinasema wamepokea barua kutoka mahakamani ikiwaeleza kuwa CHADEMA imezuiwa kufanya kazi, hivyo kiongozi huyo hapaswi kushiriki.

Katika kipindi cha kesho, Heche ilikuwa akutanishwe na watendaji wa Serikali.

CHADEMA imezuiwa kufanya kazi hadi kesi ya madai iliyofunguliwa na aliyekuwa Makamu Mwenyekiti (Zanzibar), Said Issa Khamis na wenzake wawili itakapoamuliwa.

Katika madai yao, walalamikaji wanadai kutokuwepo kwa mgawo halali wa mali za chama hucho kati ya Bara na Zanzibar.

View attachment 3377804
Nchi ina watawala waoga sana.
Kama ulicho/ unachokitenda ni haki Unaogopa nn sasa???
 
View attachment 3377709

Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA (Bara), John Heche amezuiwa kushiriki kipindi cha Cafe Talk kitakachofanyika kesho Juni 22, 2025 jijini Dar es Salaam.

Taarifa kutoka kwa wanandaaji wa kipindi hicho zinasema wamepokea barua kutoka mahakamani ikiwaeleza kuwa CHADEMA imezuiwa kufanya kazi, hivyo kiongozi huyo hapaswi kushiriki.

Katika kipindi cha kesho, Heche ilikuwa akutanishwe na watendaji wa Serikali.

CHADEMA imezuiwa kufanya kazi hadi kesi ya madai iliyofunguliwa na aliyekuwa Makamu Mwenyekiti (Zanzibar), Said Issa Khamis na wenzake wawili itakapoamuliwa.

Katika madai yao, walalamikaji wanadai kutokuwepo kwa mgawo halali wa mali za chama hucho kati ya Bara na Zanzibar.

View attachment 3377804
Kwanini waandaaji hawajui kuwa kuna zuio la mahakama? Hii inchi kuwa watu wanapenda kuzua taharuki bila sababu.
 
Lakini bila shaka unajuwa.
Hili siyo la Samia peke yake, hili ni la GENGE zima linalo simamia ajenda ya kuiteka CCM, na Tanzania kwa ujumla.

Samia akifa leo, Genge hilo chini ya Kikwete litampata mwingine kwenye Genge lao kuendeleza haya tunayoyaona leo.

Pengine labda uombe Kikwete na Samia wote waondoke kwa mpigo, na Genge kusambaratika.
Anaweza Kuja kiongozi ambae achanga akili sio kama huyu
 
Kama ni kweli hio sababu inayotolewa sisi ngumbaru wa sheria tunabaki kushangaa.

Hili jambo la mahakamakukazia hukumu yenyewe limeanza lini? Au siku hizi mahakama.nayo inafungua malalamiko na kujitolea hukumu?

Vinginevyo ni nani huyo aliyekwwnda mahakamani kudai hili? Na ilikuwa lini? Lilisikilizwa na nani? Pande zote zilikuwepo?
 
Anaweza Kuja kiongozi ambae achanga akili sio kama huyu
Mkuu, naona hunielewi.
Genge ninalolizungumzia hapa linayo ajenda ya kipekee kwa taifa hili. Bila ya kulidhibiti Genge hilo; na hasa Kikwete, usitegemee kiongozi wa "kuchanga akili" toka kwenye Genge hilo!. Ajenda yao ni mbovu!
 
Kama ni kweli hio sababu inayotolewa sisi ngumbaru wa sheria tunabaki kushangaa.

Hili jambo la mahakamakukazia hukumu yenyewe limeanza lini? Au siku hizi mahakama.nayo inafungua malalamiko na kujitolea hukumu?

Vinginevyo ni nani huyo aliyekwwnda mahakamani kudai hili? Na ilikuwa lini? Lilisikilizwa na nani? Pande zote zilikuwepo?
Wakati huu kuna mambo ya ajabu sana.
Kwa hiyo John Heche amegeuka na kuwa "mali ya CHADEMA", inayo daiwa na wafungua mashtaka!
 
Wakati huu kuna mambo ya ajabu sana.
Kwa hiyo John Heche amegeuka na kuwa "mali ya CHADEMA", inayo daiwa na wafungua mashtaka!
Kwamba huyu Heche, hana maisha binafsi nje ya uongozi wa sasa wa chama chake?

Kwa hiyo chombo cha habari kikimnukuu Heche kama aliyewahi kuwa... pia ni kosa?

Na je kama mtu anayetoka eneo lenye madini, pia haruhusiwi kutoa maoni yake?
Ama kwa hakika amekuwa mali ya chama!
 
Kwanini waandaaji hawajui kuwa kuna zuio la mahakama? Hii inchi kuwa watu wanapenda kuzua taharuki bila sababu.
Lengo kuvutia watazamaji watakao click wapate viewers wengi

Si unajua watu wanalipwa kwa views nyingi

Si kuwa walikuwa hawajui ni makusudi wakati clicks zilishafanyika
 
Kwamba huyu Heche, hana maisha binafsi nje ya uongozi wa sasa wa chama chake?

Kwa hiyo chombo cha habari kikimnukuu Heche kama aliyewahi kuwa... pia ni kosa?

Na je kama mtu anayetoka eneo lenye madini, pia haruhusiwi kutoa maoni yake?
Ama kwa hakika amekuwa mali ya chama!
Linalo sikitisha ni kwa hawa wapumbavu kudhani kwamba waTanzania hawana akili!
 
Linalo sikitisha ni kwa hawa wapumbavu kudhani kwamba waTanzania hawana akili!
Kwa maneno ya Mwalimu Chachage aliitaja hali hii kama watanzania wamegeuzwa na kuweka katika hali ya " collective imbecile"
 
Wakati huu kuna mambo ya ajabu sana.
Kwa hiyo John Heche amegeuka na kuwa "mali ya CHADEMA", inayo daiwa na wafungua mashtaka!
Unajua rasilimali watu za chama? Unafikiri rasilimali ni majengo,magari na akaunti za benki tu? Mjinga wewe

Rasilimali ni pamoja na rasilimali watu Heche akiwemo .Ni rasilimali watu ya CHADEMA
 
Unajua rasilimali watu za chama? Unafikiri rasilimali ni majengo,magari na akaunti za benki tu? Mjinga wewe

Rasilimali ni pamoja na rasilimali watu Heche akiwemo .Ni rasilimali watu ya CHADEMA
Sasa mtu duni kama wewe, unataka unilazimishe kweli niwe na mjadala na wewe? Tutaanzia wapi wakati inajulikana kinachokupa msukumo hapa siyo maslahi ya taifa hili?

Huu upuuzi wote mnaoufanya kwa jina la "sheria" feki, mnafikiri utawafikisha popote?
Subiri hapo hizo sheria za kujitungia kulinda maslahi yenu zitakavyo wageukia nyinyi wenyewe.
Hivi bado hamjitambui jinsi mnavyo jionyesha kuwa majuha mbele za watu?
 
Back
Top Bottom