Said anataka Heche na Mnyika wapelekwe gerezani

Said anataka Heche na Mnyika wapelekwe gerezani

Mafyangula

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2025
Posts
557
Reaction score
1,039
Mawakili Gido Semfukwe na Shaban Marijani wanaowawakilisha aliyewahi kuwa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Zanzibar Said Issa Mohamed na wenzake wawili, kwenye kesi ya jinai namba 48250 ya mwaka 2025 walioifungua Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar dhidi ya vigogo wa CHADEMA wakiongozwa na Makamu Mwenyekiti wake wa Tanzania Bara John Heche, wamefunguka 'mahitaji' ya wateja wao kwenye kesi hiyo

Mawakili hao wamewaeleza Wanahabari leo kuwa wateja wao wanaimba Mahakama kutoa adhabu kali kwa washtakiwa kwa kukiuka amri ya Mahakama Kuu iliyotolewa Juni 10 mwaka huu, ambapo wamesema adhabu wanayoiomba ni wahusika kukamatwa na kupelekwa gerezani hadi hapo kesi ya madai inayohusu usawa kwenye mgawanyo wa mali ndani ya chama hicho kati ya Tanzania Bara na Zanzibar iliyofunguliwa Mahakamani hapo itakapofikia tamati

Kesi hiyo ya jinai ambayo imesikilizwa leo, Jumanne Oktoba 28.2025 Mahakamani hapo chini ya Jaji Awamu Mbagwa, itatolewa hukumu yake Novemba 04.2025

 
Mawakili Gido Semfukwe na Shaban Marijani wanaowawakilisha aliyewahi kuwa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Zanzibar Said Issa Mohamed na wenzake wawili, kwenye kesi ya jinai namba 48250 ya mwaka 2025 walioifungua Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar dhidi ya vigogo wa CHADEMA wakiongozwa na Makamu Mwenyekiti wake wa Tanzania Bara John Heche, wamefunguka 'mahitaji' ya wateja wao kwenye kesi hiyo

Mawakili hao wamewaeleza Wanahabari leo kuwa wateja wao wanaimba Mahakama kutoa adhabu kali kwa washtakiwa kwa kukiuka amri ya Mahakama Kuu iliyotolewa Juni 10 mwaka huu, ambapo wamesema adhabu wanayoiomba ni wahusika kukamatwa na kupelekwa gerezani hadi hapo kesi ya madai inayohusu usawa kwenye mgawanyo wa mali ndani ya chama hicho kati ya Tanzania Bara na Zanzibar iliyofunguliwa Mahakamani hapo itakapofikia tamati

Kesi hiyo ya jinai ambayo imesikilizwa leo, Jumanne Oktoba 28.2025 Mahakamani hapo chini ya Jaji Awamu Mbagwa, itatolewa hukumu yake Novemba 04.2025


Hivi huko serikalini hawa watu hawajui kuwa kuna retirement kwenye hizi kazi?
 
Watuambie anaishi wapi ili naye aonje machungu ya wananchi.
 
Back
Top Bottom