Parabolic
JF-Expert Member
- Dec 3, 2013
- 2,744
- 2,604
Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA (Bara), John Heche amezuiwa kushiriki kipindi cha Cafe Talk kitakachofanyika kesho Juni 22, 2025 jijini Dar es Salaam.
Taarifa kutoka kwa wanandaaji wa kipindi hicho zinasema wamepokea barua kutoka mahakamani ikiwaeleza kuwa CHADEMA imezuiwa kufanya kazi, hivyo kiongozi huyo hapaswi kushiriki.
Katika kipindi cha kesho, Heche ilikuwa akutanishwe na watendaji wa Serikali.
CHADEMA imezuiwa kufanya kazi hadi kesi ya madai iliyofunguliwa na aliyekuwa Makamu Mwenyekiti (Zanzibar), Said Issa Khamis na wenzake wawili itakapoamuliwa.
Katika madai yao, walalamikaji wanadai kutokuwepo kwa mgawo halali wa mali za chama hucho kati ya Bara na Zanzibar.